Kumekucha CCM vs UKAWA

Pole mkuu, naona unatetea ugali, ila in a mattee of time, ikishaingia kwenye social circle ikaeleweka mtaelewa maana yake.
Siasa ina nguvu sana hapa duniani na kwa jamii, busara ni muhimu, udongo uwah ungal maji
 
Watanzania tuombe mungu atujaalie amani na upendo na kwa uwezo wake auzime huu Moshi unaofukuta...Aaamin
 
Unamsemea na Nani hapo?labda familia yako tu
 
Hiyo misuguano yenu isije kutusumbua tusiokuwa na kadi,maana mmeshajiona sasa ndio wenye nchi wakati watanzania zaidi ya million 30 hawazijui hata kadi za vyama.

Usiwe na shaka sisi hii haituhusu, unadhani konda gani atakaepandisha abiria kwenye Daladala kwa kuonyeshwa kadi ya chama siasa, au mangi auze duka lake kwa kuonyeshwa kadi.

Mmachinga au bidhaa za kwa kuonyeshwa kadi, wauza maji barabarani waonyweshe kadi, baar zihudumie kwa kadi za siasa, kwa mama muuza tuhudumiwe kwa kadi.

Haiwezekani labda hao hao wanachama wenu, sisi tusiokuwa wanachama wa vyama vyenu mtupandishe mabasi ya mikoani kwa kuonyesha kadi ya cha siasa, gesti tuingie kwa kadi ya siasa, feli huduma samaki tuipate kwa kuonyesha kadi ya siasa hii haiwezekani.

Kwa sababu mimi sina kadi na sifirii kuchukua kadi ya chama, bali nitabaki mpiga kura, mtakachoweza nikifa muisusie kuizika maiti yangu, lakini hamtaweza maana nitanuka mtanizika tu, haijalishi nitazikwa na watu wangapi maana maiti haioni fahari, hata azikwe na walimwengu wote.

Na sema hii huku kwetu imedunda ikajalibiwe kwingine. Yote kwa yote wotd mnahusika na vyama vyenu CCM na UKAWA kaa muangalie watanzania kwanza, lolote likalotokea watanzania watawalilia.
 
Mimi natangaza rasmi kuvunja uhusiano wa aina yoyote na mwana ccm, hata kama ni ndugu wa damu tusijuane kuanzia sasa.
 
Pole mkuu, naona unatetea ugali, ila in a mattee of time, ikishaingia kwenye social circle ikaeleweka mtaelewa maana yake.
Siasa ina nguvu sana hapa duniani na kwa jamii, busara ni muhimu, udongo uwah ungal maji
Hapa natoa darasa ili tupunguze wajinga. Wewe huenda umeelewa. Ndio ninavyopunguza wajinga hivyo.
 
sijali sana kuhusu matokeo ya huu uamuz,, iwe yataleta madhara au la!!......

lkn jambo moja li wazi kabisa, umoja wetu unapitia jaribio kubwa kisa tu wanasiasa wachache wanafanya maamuzi wanayoyajua wao!!

hili si jambo la kulishangilia au kubeza,, hizi mbegu sio salama kwa ustawi wa taifa letu!
 
Mke wangu tunatofautiana itikadi za vyama lakini ananipa haki yangu kama kawaida...kwa maana ushirikiano upo na amechukia sana ukawa kususa bunge na inshaallah keshokutwa namvisha kijani...

Nyie endeleeni kutoa matamko...chama kinapoteza umaarufu wake kwa kasi ya ajabu.
 
Upinzani haukuanza leo nchini, na miaka yote Wabunge wa upinzani na wale wa CCM wameshirikiana katika mambo mbali mbali kama Watanzania. Cha kustaajabisha ndani ya miezi minane tu ya Serikali hii ya awamu ya tano kumejengeka chuki za kutisha kati ya Wabunge wa upinzani na wale wa CCM. Wabunge wa CCM wamekuwa wakiwatusi Wabunge wa upinzani kwa matusi ya nguoni mara kwa mara bila ya kuchukuliwa hatua zozote za kinidhamu na hiyo inayoitwa kamati ya Bunge ya maadili. Kwa maneno mengine wajumbe wa kamati hiyo ya maadili wameridhia Wabunge wa upinzani kutukanwa matusi ya nguoni.

Sasa chuki inaongezeka hata kuanza kutosalimiana na chuki hii haitaishia kwa Wabunge tu bali inaweza kabisa kusambaa miongoni mwa Watanzania. Tutafakari kwa kina na kukemea huu upandikizaji wa mbegu za chuki za kutisha unaofanywa ndani na nje ya Bunge kwa kasi ya kutisha. Tukikaa kimya na kuwaacha hawa wapandikizaji wa mbegu za chuki waendelee na mradi wao basi siku za usoni nchi yetu itaingia kwenye giza nene sana kwa sababu tu wapandikizaji chuni nchini hatukuwakemea mapema na kwa nguvu zote matokeo yake mbegu zao za chuki mizizi yake itakuwa imetambaa nchi nzima.
 

Inanikumbusha Pemba kuna mnunuzi wa samaki ambae ni kada wa CCM kwenye mnada wa samaki alifika bei ya 170,000 kwa tenga na kufaninikiwa kushinda .Lakini mchuuzi akamwuzia mnunuzi aliefika bei ya 70,000 ambae ni kada wa CUF mwenzie.

Kada wa CCM alipohoji nae akajibiwa na yule mchuuzi wa CUF kwamba mbona na sisi tukishinda uchaguzi hatupewi madaraka
 
nimeipenda hiii...
 
Umeongea kama nilivyokuwa nawaza......True story
 
Haya ndio matokeo ya kuwa na mfalme anayeongoza nchi kwa chuki.
Mimi nnauhakika Tanzania ikipata janga kubwa, huko CCM hakuna wa kuwaunganisha wananchi.
Hii awamu hakuna busara ya uongozi!
 
Huo ndio msimamo wa bavicha, upende husipende na watu tupo tayari kujiunga na ushauri wao, we nani hadi unawasemea watanzania?
Na hao Bavicha nani ata wawasemee watanzania au siku hizi vijikundi vya siasa vina power ya kuwasemea watanzania? kuwa kimawazo wewe dogo.
 

Huku Kwetu Kuna MwanaCCM mmoja alikuwa ni mwathirika wa UKIMWI kwa muda Mrefu na alikuwa akifuata dawa za kuongeza siku za kuishi makao makuu ya Wilaya ambapo kutoka kijijini kwetu hadi wilayani(Hospitali ya wilaya) nauli ya BUS ni Tsh 10,000/= kwenda na kurudi.

Sasa baada ya kumalizika uchaguzi kukatokea utengano wa kiwango cha juu sana, na kwa vile jamaa alikuwa anachangiwa nauli na marafiki zake ambao ni wana CDM wakakata huo mrija na ndugu yetu huyo akawa ameshindwa kuendelea na dozi kwa kukosa nauli ya kwenda kuchukua dawa, Jamaa AFYA yake ikawa mbaya sana na kupelekea kufariki.

Bad enough baada ya kufariki watu waligoma kumzika pale kijijini kwa sababu hakuwa na eneo la ardhi yoyote, ilibidi wananzengo watoe taarifa police ndo waliokuja kuuchukua mwili wake na kwenda kuuzika wanakojua wao.

Jamani hili Tamko cyo la kupuuzia hata kidogo kwa sababu baadhi ya watu hasa wana CCM ndo wahanga wakubwa sana wa hili tamko.Kwa MTU asiyejua kinachoendelea sehemu nyingi hapa Tz hasa vijijini anaweza akasema ccm inapendwa lkn ukijitambulisha kuwa wewe ni mwanachama au mshabiki tu wa ccm, watu wanakuona kama vile ni shetani flani hivi.

CCM hili tamko ni baya sana kwa usitawi wa watu wenu I mean wanachama wenu kuweni makini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…