Kumdai boyfriend ni vibaya?

Kumdai boyfriend ni vibaya?

Furahatuu

Senior Member
Joined
Apr 11, 2013
Posts
115
Reaction score
40
Naombeni ushauri kama ni sahihi

Nilikuwa na rafiki wangu wa kiume ambaye tuliachana zaidi ya mwaka mmoja uliopita. sasa wakati tukiwa kwenye mahusiano yeye alikuwa chuo anasoma ila alikuwa ameajiriwa na mimi nilikuwa nimeajiriwa. kwa kuwa tulikuwa na mipango mingi ya kimaisha nilikuwa mamshirikisha mipango yangu naye ananishirikisha ya kwake. kuna kipindi nikawa nimefunga biashara yangu na fedha ikawa ipo tu benki sasa akaniambia kwa kuwa hufanyi biashara kwa sasa nipe hiyo fedha niongezee kwenye biashara yangu then ukishafikiria biashara ya kufanya nitakupa fedha yako, mimi nikampa hiyo fedha. ila baada ya kumaliza chuo na kurudi kazini kwake mawasiliano nami yakaanza kupungua na baada ya muda tukawa tumeachana ila hakukuwa na sababu ya msingi ya yeye kuachana na mimi ila akaniambia usijali fedha yako nitakupa sitakurusha. baada ya hapo akanipa asilimia 75% ya hiyo fedha. nilipomuambia kiasi kilichobaki akawa hapokei simu na hata siku moja akampa mwanamke simu anitukane.nilipata maumivu sana sijui kama nilikosea kudai fedha yangu au nilitakiwa nisimdai kwani makubaliano yalikuwa nikibuni biashara anipe fedha. ushauri maana tangu nitukanwe sijampigia tena simu.
 
Hamna ubaya kumdai ila kuna ubaya kukabidhiana pesa nyingi bila makubaliano ya kimaandishi.
 
Endelea kukaa kimya hivyo hivyo, kama una haki malipo ni hapa hapa duniani
 
Naombeni ushauri kama ni sahihi

Nilikuwa na rafiki wangu wa kiume ambaye tuliachana zaidi ya mwaka mmoja uliopita. sasa wakati tukiwa kwenye mahusiano yeye alikuwa chuo anasoma ila alikuwa ameajiriwa na mimi nilikuwa nimeajiriwa. kwa kuwa tulikuwa na mipango mingi ya kimaisha nilikuwa mamshirikisha mipango yangu naye ananishirikisha ya kwake. kuna kipindi nikawa nimefunga biashara yangu na fedha ikawa ipo tu benki sasa akaniambia kwa kuwa hufanyi biashara kwa sasa nipe hiyo fedha niongezee kwenye biashara yangu then ukishafikiria biashara ya kufanya nitakupa fedha yako, mimi nikampa hiyo fedha. ila baada ya kumaliza chuo na kurudi kazini kwake mawasiliano nami yakaanza kupungua na baada ya muda tukawa tumeachana ila hakukuwa na sababu ya msingi ya yeye kuachana na mimi ila akaniambia usijali fedha yako nitakupa sitakurusha. baada ya hapo akanipa asilimia 75% ya hiyo fedha. nilipomuambia kiasi kilichobaki akawa hapokei simu na hata siku moja akampa mwanamke simu anitukane.nilipata maumivu sana sijui kama nilikosea kudai fedha yangu au nilitakiwa nisimdai kwani makubaliano yalikuwa nikibuni biashara anipe fedha. ushauri maana tangu nitukanwe sijampigia tena simu.

Dah umenikumbusha mbaliiiii, hilo ni kosa ambalo sitakuja kulifanya tena kwenye maisha yangu 'KUMKOPESHA PESA BOYFRIEND'!!!! . Hata wewe nakushauri usije kulifanya kosa la aina hiyo tena, MWIKOOOO!!!!. Nikirudi kwenye mada yako una haki zote za kumdai X-wako hela ulizomkopesha, kwa sababu mlikubaliana kwamba takurudishia. Tatizo linalokuja ni kwamba hakuna ushahidi wowote/ mtu aliyeshuhudia wakati ukimpa hizo hela, hivyo inakuwa ngumu. Sikulaumu kwa nn hamkuandikishiana, nafahamu mwanamke anapokuwa kwenye mapenzi huwa tunawaamini sana wapenzi wetu kwa kiwango ambacho utafikiri uko kwenye mahusiano na malaika kumbe ni MAGUMEGUME yetu haya yasiyojua kupendwa. Yaani hao watu hawana maana yoyote, unatakiwa uishi nao kama mgeni aliyekuja mara moja kesho anarudi kwake.

Ili uendelee kuwa na amani na kwa kuwa ameanza kuwatumia wanawake wakutukane anaonekana sio mstaarabu. Achana naye hautapungukiwa na kitu. Halafu Mwanaume anayejitambua huwa hakopi kwa girlfriend wake hata siku moja hapo umeingia kwenye choo cha shimo kilichajaa. Yaani siku hizi hakuna wanaume jamani, mpaka mnafikia hatua ya kutapeli vijisenti vya wanawake, Tumekwisha! teh teh teh.
 
kama haiathiri maisha yako,achana nayo,pia kama una mwanaume mwingine inaweza isimpendeze hayo mawasiliaano yenu,coz mtagombana afu baadae mje mseme mnahisi kupendana
 
Dah umenikumbusha mbaliiiii, hilo ni kosa ambalo sitakuja kulifanya tena kwenye maisha yangu 'KUMKOPESHA PESA BOYFRIEND'!!!! . Hata wewe nakushauri usije kulifanya kosa la aina hiyo tena, MWIKOOOO!!!!. Nikirudi kwenye mada yako una haki zote za kumdai X-wako hela ulizomkopesha, kwa sababu mlikubaliana kwamba takurudishia. Tatizo linalokuja ni kwamba hakuna ushahidi wowote/ mtu aliyeshuhudia wakati ukimpa hizo hela, hivyo inakuwa ngumu. Sikulaumu kwa nn hamkuandikishiana, nafahamu mwanamke anapokuwa kwenye mapenzi huwa tunawaamini sana wapenzi wetu kwa kiwango ambacho utafikiri uko kwenye mahusiano na malaika kumbe ni MAGUMEGUME yetu haya yasiyojua kupendwa. Yaani hao watu hawana maana yoyote, unatakiwa uishi nao kama mgeni aliyekuja mara moja kesho anarudi kwake.

Ili uendelee kuwa na amani na kwa kuwa ameanza kuwatumia wanawake wakutukane anaonekana sio mstaarabu. Achana naye hautapungukiwa na kitu. Halafu Mwanaume anayejitambua huwa hakopi kwa girlfriend wake hata siku moja hapo umeingia kwenye choo cha shimo kilichajaa. Yaani siku hizi hakuna wanaume jamani, mpaka mnafikia hatua ya kutapeli vijisenti vya wanawake, Tumekwisha! teh teh teh.

asante madameA kwa ushauri nimekoma kwani hata saikolojia yangu imeharibika kuamini watu mamshukuru mungu kwani nilitaka nimpe zaidi ya hiyo niliyompa lakini nikasita nafikiri alikuwa Roho wa Mungu.
 
.. akanipa asilimia 75% ya hiyo fedha. nilipomuambia kiasi kilichobaki akawa hapokei simu na hata siku moja akampa mwanamke simu anitukane..
Na jeje wewe hakuna anachokudai? Maana inawezekana anafanya hivyo kama compensation! Na hiyo 25% ni kiasi gani in shillings? Kama sio material kivile unaweza kuipotezea tu!
 
dah mapenzi ni karaha mie mbele ya pesa namfungia safari ntamchamba kila atokeapo naaingiliapo hata kama ni oficini namtukania huko atachoka kero atanilipa hela yangu ***** zake
 
Na jeje wewe hakuna anachokudai? Maana inawezekana anafanya hivyo kama compensation! Na hiyo 25% ni kiasi gani in shillings? Kama sio material kivile unaweza kuipotezea tu!

mimi anidai chochote kwani mimi nilikuwa namsaidia sana wakati akiwa chuo kwani alikuwa anajigharamia mwenyewe na kuna kipindi alikuwa akikwama mamsaidia lakini mshahara ndo yaliyonikuta.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Na jeje wewe hakuna anachokudai? Maana inawezekana anafanya hivyo kama compensation! Na hiyo 25% ni kiasi gani in shillings? Kama sio material kivile unaweza kuipotezea tu!
hiyo 25 aliwekeza eeee not simple like that
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Na jeje wewe hakuna anachokudai? Maana inawezekana anafanya hivyo kama compensation! Na hiyo 25% ni kiasi gani in shillings? Kama sio material kivile unaweza kuipotezea tu!

mimi anidai chochote kwani mimi nilikuwa namsaidia sana wakati akiwa chuo kwani alikuwa anajigharamia mwenyewe na kuna kipindi alikuwa akikwama mamsaidia lakini mshahara ndo yaliyonikuta.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
hiyo 25 aliwekeza eeee not simple like that
I agree! Lakini si ni lazima kupima pia implications za yeye kudai? Isije kuwa mtu anataka "kuuza ngombe kugharamia kesi ya kuku"!
 
Ni haki yako kudai haki yako japo sijui kama kuna sehemu mliandikishana au kuna shahidi.
 
Labda kama hamuishi eneo moja, lakini wote tuko mwanza lol! mbona utaitoa hela yangu bila kupenda lol, hela ya mwanamke ni ngumu jamani halafu baba mzima unanidhulumu, yaani utaitoa tu
 
Back
Top Bottom