Kumbukumbu yangu fupi ya Mohammed Seif Khatib

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,850
30,193
KUMBUKUMBU YANGU FUPI YA MOHAMMED SEIF KHATIB

Mara yangu ya kwanza kukutana na Mohammed Seif Khatib uso kwa macho ilikuwa Makka wakati wa Hijja mwaka 1998.

Balozi Ramadhani Dau alinichukua kwenda kumsalimia Mzee Aboud Jumbe ambae alikuwa amefikia kwenye nyumba za wageni wa Mfalme wa Saudi Arabia.

Mzee Jumbe alifurahi sana kutuona.

Tulipokuwa tumekaa tunazungumza na Mzee Jumbe, Mohammed Seif Khatib akaja na kundi dogo la Wazanzibari kumwamkia Mzee Jumbe.

Furaha ya Mzee Jumbe ikazidi kwani Mohammed Seif Khatib akawa anatuzungumzisha akijaribu kutia maneno ya Kiarabu katika kuusifia utukufu na ukarimu wa serikali ya Saudia inavyokirimu wageni wake. Tukawa sote tunamsikiliza na kucheka.

Mara ya pili kukutana na Mohammed Seif Khatib ilikuwa mwaka wa 2007 Kilimanjaro Kempiski Hotel alipoalikwa na Oxford University Press (OUP), Nairobi kuja kuzindua Kamusi ya Kiswahili pamoja na kitabu changu, "The Torch on Kilimanjaro."

Katika sherehe ile Mohammed Seif Khatib alipokaribishwa kuzungumza na kuzindua vitabu hivi viwili aliomba radhi kuwa hatokizungumza "The Torch on Kilimanjaro," kwa kuwa hamfahamu mwandishi wake. Lakini mimi nikimfahamu yeye vyema kwa ajili ya ile staili yake ya uandishi wa makala zake katika Mzalendo, gazeti la CCM.

Katika timu ya OUP iliyokuja kutoka Nairobi kuhudhuria uzinduzi ule alikuwapo Sheikh Abdillah Nasir. Mohammed Seif Khatib alimsifia sana Sheikh Abdillah Nasir akasema alimsaidia katika uhariri wa mswada wa kitabu chake kimoja ambacho OUP walikichapa.

Mohamed Seif Khatib alipomaliza kuzungumza OUP waliniomba nikizungumze kitabu changu.

Hii ndiyo kumbukumbu yangu ya huyu ndugu yetu aliyetangulia mbele ya haki.

Allah amfanyie wepesi katika safari yake hii.

1613380108157.png
 
Mzee wetu una hazina ya kutosha sana.

Siku moja tulikaa mimi na mwenzangu tukawa tunafikiria namna gani mchango wako unaweza kuhakikishwa haupotei tukakosa majibu.

Mola akulinde na naamini unalifikiria hilo kila uchao
 
Mohammed Seif Khatib aliwahi kuandika makala ya kibaguzi kuhusu wenyeji wa kilimanjaro na harakati za uraisi wa Tanzania. nilishangaa sana kiongozi muandamizi wa ccm, na mtu aliyekuwa akisimamia zoezi la kutafuta mgombea uraisi kwa tiketi ya ccm, kuwa na mtizamo wa aina ile, pamoja na ujasiri wa kuuweka wazi ktk vyombo vya habari.

Mohammed Seif Khatib ametutoka. Nawapa pole familia yake, ndugu, jamaa, na marafiki kwa msiba huu. MUNGU ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi.
 
Nakumbuka wakati nipo UDSM nikisoma gazeti maarufu la RAI NGUVU YA HOJA Lile la jenrali ulimwengu enzi zile.
Gazeti lilisheheni makala za moto haswa.
Mwandishi mmoja aliandika " mohd seif khatibu" hathubutu kuighani fungate"
Fungate ni jina la kitabu alichoandika huyu marehemu akikosoa mamlaka. Alipopewa uongozi aliishia kwenye fungate kama watawala....
Pumzika kwa amani bwana bilali msalimie ndugu BENJAMIN MKAPA
 
Nadhani nahitaji kujifunza upya maana ya neno utukufu.

saudi arabia hii inayofadhili ugaidi. Saudi hii inayomchinja na kumkatakata Vipande mtu inawezaje itwa serikali tukufu!?
 
Nadhani nahitaji kujifunza upya maana ya neno utukufu.

saudi arabia hii inayofadhili ugaidi. Saudi hii inayomchinja na kumkatakata Vipande mtu inawezaje itwa serikali tukufu!?
Distant...
Usihangaishwe na maneno haya kwani daima watu wataghitilafiana.
Hii ni taazia na taazia kwa kawaida haijibiwi.
 
Kwa wale waliosoma Kiswahili sekondari watakumbuka kitabu cha WASAKATONGE ktk Fasihi ya Kiswahili. Mtunzi kaondoka ila kumbukumbu lake linasalia.
 
Mzee wetu una hazina ya kutosha sana.

Siku moja tulikaa mimi na mwenzangu tukawa tunafikiria namna gani mchango wako unaweza kuhakikishwa haupotei tukakosa majibu.

Mola akulinde na naamini unalifikiria hilo kila uchao
Relief...
Nashukuru sana kuwa kila nilichaondika nimekihifadhi.

Unaweza kuanza na hapa: mohamedsaidsalum.blogspot.com.

Unaweza kunitafuta kwa sauti yangu na picha You Tube kwa name search.
Ingia JF, FB.

Unaweza kunitafuta katika magazeti ya Rai, Mtanzania na Raia Mwema ingawa huko utafiti utakuwa mgumu wa kupinda mgongo.

Mwisho Prof. Google na Library of Congress, Washington.

Hii picha niko Library of Congress.

1613418167729.png
 
Naomba kuelimishwa mzee wangu.
Aboud jumbe nachofahamu kuwa aliwekwa House arrest na mwalimu na hayakuwahi kufutwa maamuzi hayo. Kwa ufahamu wangu huo uko sahihi, ni kwa vipi aliweza hudhulia hijja?
 
Mohamed kwa ukaribu wako na wakina Sykes na Mwapachu, nilitegemea ungeandika Tanzia ya marehemu kaka yao marehemu Bakari? Pengine umeiandika sijaiona!!!
 
Mohamed kwa ukaribu wako na wakina Sykes na Mwapachu, nilitegemea ungeandika Tanzia ya marehemu kaka yao marehemu Bakari? Pengine umeiandika sijaiona!!!
Bulesi,
Nikimjua Bakari Mwapachu lakini si kwa kiasi cha kuweza kumweleza.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom