Hahahahahaaaa!!!!!
Mwansheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema akipoza koo lake kwa kunywa maji baada ya wabunge kukataa kupitisha muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali wa mwaka 2011, mjini Dodoma jana.
Vipi hakuwa na sime na rungu kiunoni? Maana hao jamaa huko kwao ndiyo zao, hadi disco na rungu na sime!!!Baada ya kubanwa sana na pia kuzomewa na wabunge jana jioni wakati akitetea hoja ya marekebisho ya sheria mbalimbali aliyowasilisha bungeni, alianza kutoa vitisho kuwa hajafukuzwa ujaji huko akitoa macho kama kuku aliyekabwa na mfupa wa samaki!
Baada ya kubanwa sana na pia kuzomewa na wabunge jana jioni wakati akitetea hoja ya marekebisho ya sheria mbalimbali aliyowasilisha bungeni, alianza kutoa vitisho kuwa hajafukuzwa ujaji huko akitoa macho kama kuku aliyekabwa na mfupa wa samaki!
Alikuwa anaangalia mabenchi ya CDM kama nyati aliyejeruhiwa!
Ukweli nakereka sana na huu mfumo wa mwanasheria mkuu wa serikali kulumbana na wabunge. Ni mfumo mbovu mbovu mbovu sana. Bunge ni sehemu wa wawakilishi wa wananchi, mwanasheria mkuu anatafuta nini bungeni? Katiba mpya iseme kabisa bunge ni wa wabunge tu, wengine wote watakaa maofisini mwao na kama watahitajika basi utaratibu mwingine utumike, kwa mfano mwanasheria mkuu angeitwa (kama wanataka maelezo yake) kwenye vikao vya kamati za kudumu za bunge. basi.
Kimsingi mimi nakubaliana na utaratibu wa AG kuwepo bungeni lakini wajibu wake uwe kutoa tafsiri na miongozo ya kisheria pale wabunge wanapokosea au kuteleza katika kutoa tafsiri ya kanuni za bunge. Hivyo yeye ni mtu muhimu sana kuwezesha majadiliano ya hoja kujadiliwa bila kupindisha Katiba, Sheria, Kanuni na maadili ya Taifa.