Kumbe Wanawake Wameanza Kupendana

big-diamond

JF-Expert Member
May 23, 2009
421
551
Kwenye harakati za kupunguza zile kauli kupata tabu sana na biti za watembea na ilani basi jioni hii najirudisha uswekeni kwenda kujificha hadi hapo kesho (Maana kuna watu huenda kulala na wengine kijificha)

Hapa nipo kwa daladala iliyojaa ile kisawa sawa, basi kuna Mama tumepanda nae daladala akiwa na mtoto mgongoni kwenye kitenge(Heshma zenu wamama wote mliolea na kupenda watoto wenu)

Basi mtoto akaanza kulia kwa kulalamika huku mama akihangaika kumbembeleza huku kashikilia bomba,(wale wa mbagala wananielewa hapa), tumeendelea na safar bas imefika sehem foleni ikawa kubwa(nahisi kuna Mamajusi wameenda kuona mtoto), bas mtoto analia na mama anahangaika ili asiwe kikwazo kwa wana daresalama.

Ni kama malaika alimwambia dada mmoja aliyekuwa amekaa kwenye kiti(Makonda huita sofa) kuwa yule mwanamke mwenzie na mwanae wanahitaji msaada, bas akamwita yule dada na kumwambia aje akae na mwanae pale alipokuwa yeye, na yeye kushika bomba(kupaka rangi).

Hili tukio limenifanya nimtazame mara mbili mbili huyu dada na kwakweli nisingekuwa nimeoa Mama Nyonzo wangu pale Itinde bas leo ninge propose...

Heshma yenu wanawake na madada wote mnaopendana na kusaidiana kwenye mazuri..

Ora Et Labora..
 
Wanaume ndio chanzo kikubwa cha minyukano ya wanawake.
Otherwise, wanawake wanapendana kwa dhati kuliko sisi wanaume
 
Wanaume ndio chanzo kikubwa cha minyukano ya wanawake.
Otherwise, wanawake wanapendana kwa dhati kuliko sisi wanaume
Yani mkuu nilipata amani saaana.

Kama sisi ndio chanzo ninaapa leo ntamuogesha mahaba Mama Nyonzo hadi aumwe baridi yabisi
 
Hawa wanapendana mda mwingine ila wakianza kuvurugana bora wanaume ntapatana ila sio hawa uwachukua mda sana.
 
Kuna siku, miaka ya nyuma, wakati ule fasheni mpya ilikuwa gari nyingi zikirudi reverse zinakuwa na mlio wa kutoa ishara gari inarudi, ili kuepusha ajali, kulikuwa na gari moja ina mlio wa kipekee kidogo.

Gari ile ilikuwa ikirudi reverse, ina mlio kama mtoto analia.

Basi mimi sikushangaa sana, niliona hivi ni vituko vya Dar es salaam tu, ukishangaa shangaa hutafika unakokwenda.

Wakati gari lile linarudi nyuma hivyo, kulikuwa na mama mmoja, yule mama alitukana sana kitendo kizima cha kufanya sauti ya mtoto kuwa ni alarm ya gari.

Akafoka sana, akasema sana, akasema hawa watu wengine kama wachawi, nini kuweka sauti ya mtoto kuwa kama alarm hivyo.

Akasema kwake yeye kama mama akisikia sauti ya mtoto vile inamuumiza mpaka moyoni, bila kujali ni alarm au vipi.

Nikaona kweli kuna watu tumeumbwa tofauti.

Wakati wewe unaweza kusikia sauti ya mtoto analia ukaona karaha tu, kuna watu inawachoma mpaka moyoni kabisa.

Sasa mtu kama huyo akiinuka na kutoa siti ili mtoto anyamaze, siwezi kushangaa.
 
Kuna siku, miaka ya nyuma, wakati ule fasheni mpya ilikuwa gari nyingi zikirudi reverse zinakuwa na mlio wa kutoa ishara gari inarudi, ili kuepusha ajali, kulikuwa na gari moja ina mliowa kipekee kidogo.

Gari ile ilikuwa ikirudi reverse, ina mlio kama mtoto analia.

Basi mimi sikushangaa sana, niliona hivi ni vituko vya Dar es salaam tu, ukishangaa shangaa hutafika unakokwenda.

Wakati gari lile linarudi nyuma hivyo, kulikuwa na mama mmoja, yule mama alitukana sana kitendo kizima cha kufanya sauti ya mtoto kuwa ni alarm ya gari.

Akafoka sana, akasema sana, akasema hawa watu wengine kama wachawi, nini kuweka sauti ya mtoto kuwa kama alarm hivyo.

Akasema kwake yeye kama mama akisikia sauti ya mtoto vile inamuumiza mpaka moyoni, bila kujali ni alarm au vipi.

Nikaona kweli kuna watu tumeumbwa tofauti.

Wakati wewe unaweza kusikia sauti ya mtoto analia ukaona karaha tu, kuna watu inawachoma mpaka moyoni kabisa.

Sasa mtu kama huyo akiinuka na kutoa siti ili mtoto anyamaze, siwezi kushangaa.
Sure thing mkuu..hii spirit ni kwamba ilikuwepo saana kipindi hicho,

Utandawazi umeondoa mengi na kuja na mengi pia, japo bado mabinti waliolelewa kwenye mazingira bora na wanauendeleza huu utamaduni

Ora Et Labora...
 
Back
Top Bottom