Kumbe walimu nanyi mnapenda starehe?

Kumbe walimu nanyi mnapenda starehe?

binti wa kirombo

JF-Expert Member
Joined
May 17, 2016
Posts
847
Reaction score
967
Habari za kazi wana JF,

Leo katika pilika zangu za ujenzi wa taifa kama mwl. Mkuu nikapita ofisini kwa walimu wenzangu kuwasabahi kama ilivyo dada.

Mwl mmoja akasema mkuu unaonaje kabla ya kufunga Ijumaa sisi walimu wote tukajumuika na wenzi wetu tukasherekea kumaliza mwaka wa masomo salama? nikamjibu haiwezekani! Kwa gharama ya nani?

Akasema watachangisha mchango kila mtu elfu 50 nikasema hapana ile namaliza kujibu walimu wote wameinuka nakunishambulia kwa maneno, ooh mkuu acha ubahili, unatubania riziki watu tunastress tunataka tukatoe stress na maneno mengine kibao.

Wakaanza wachaga bwana ubahili umewazidi, nikawaambia kama mnatakuorganize fanyieni nje ya eneo la shule na chochote kitakachotokea sitawajibika juu yenu.

Hawakuamini majibu niliyoyatoa mwalimu mmoja ambae ni rafiki yangu akaropoka hana wakuja nae INJINIA WAKE ALIMWACHA TANGU ILE JANUARY, aisee nilichotaka kumjibu huyu mwalimu Mungu aliniziba mdomo hakika.

Nikaondoka huku wakicheka sasa kwa tarifa yao hakuna cha sherehe wala nini! Ijumaa skuli itafungwa watu waende makwao wakapumzike. Sasa na sijui hela ya likizo atamsainia nani huyo mropokaji.🙄😎😎
 
Hakuna asiyependa starehe, hela itafutwe kwa shida halafu iliwe kwa shida..?
Ungeorganise mkafanya picknik, kwa hiyo bk50 mbona mambo yangefana tu!
 
kwa uandishi huo wa m' mkuu tutawalaumu wanafunzi wanaohitimu bila kujua kusoma na kuandika?
 
Kwa hio unataka kumlipa nae kwa kutomsainia from ya likizo?!! Duh!!
Hii ni hatari kiuongozi.
Waruhusu watu wasocialize ni moja ya njia ya kuimalisha mahusiano mazuri katika staff
 
Mwalimu huenda shuleni
Mwanafunzi huenda shuleni

Mwalimu husimama mstarini
Mwanafunzi husimama mstarini

Mwalimu huingia darasani
Mwanafunzi huingia darasani

Mwalimu husimama darasani
Mwanafunzi hukaa darasani

Mwalimu huandika notes
Mwanafunzi huandika notes

Mwalimu hula wakati wa mapumziko
Mwanafunzi hula wakati wa mapumziko

Mwalimu huenda nyumbani akisikia kengele
Mwanafunzi vivo hivyo.
 
inaonekana na ww ni miongoni mwa wakuu wanoko na wakola mashuleni. kuna mmoja kama ww ilibaki kdg tu nimshushi kosovo la nguvu ofcn kwake tukiwa wawili tu .

Elewa kuwa na ww ndali anakusaka kwa kuzolotesha elim nchni. Huwezi kuwanyima watu uhuru wa kusocialize kwa gharama zao na mbaya zaidi et usimsainie mtumishi barua ya rikizo kisa kakuchana ukweli!!!!! shame on you madam!!
 
Back
Top Bottom