Kumbe mabinti ndivyo mlivyo?

Kumbe mabinti ndivyo mlivyo?

J C

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2013
Posts
3,139
Reaction score
2,635
Za mida wajumbe?

Kuna friend of mine hapa ananipa mchapo akitaka kujua afanye nini.

Ana binti aliyenaye katika mahusiano kwa miaka kadhaa sasa. Kijana anasoma ila ana gratuate this year. Binti kamkaba jamaa wafunge ndoa jamaa naye kaona ni sawa kwani kaona binti amepass viwango kuwa naye kimaisha ila jamaa anakwama sehemu moja ana ajira somewhere ya mkataba na analipwa 80% ya mshahara kwa mwezi kwa sababu kiwango chake cha elimu hakijafikia lengo la mshahara kamili.

Kwa hili binti akamtia moyo kuwa asijali kabisaaa kwani kwao mahari anataja binti na akamhakikishia kuwa haitazidi laki tano ama sita jamaa kwa kuona hivyo na kwa kuzingatia umri wa ampendaye unamtupa mkono akajitosa binti akawakusanya ndugu zake wengi kuwapa taarifa kuwa amepata mchumba in short jamaa anamuuliza binti ampe siri ndg wanataka kiasi gani ili awaelezee washenga watakapo kwenda wajue kiasi binti anamwambia jamaa ajiandaye kwa milioni moja na nusu khe jamaa kasara mbaya ukitegemea ni miezi kama mitano tu imebaki kwao kufunga ndoa.

Binti ni form four failure ila anakibarua mkoa mwingine mbali jamaa mawasiliano ni Simu tu. Jamaa akawa kimya akajikunja kwani wazazi wa binti waligomea hapo hawataki chini ya hapo.

Jamaa amekubali. Sasa wameenda kwenye swara la Pete ya engagement binti anataka ya dhahabu si chini ya gramu mbili jamaa anamsihi amsaidie japo kidogo binti anagoma kwa kusema nini maana ya kuwa engaged?. Anamwambia wanunue Pete ya silver anamwambia ataiweka kwenye kidole cha nani?

Sasa hivi wamebakiza siku chache jamaa akatoe hiyo mahari anamwambia binti amsaidie pesa kidogo za kununulia vitu vya kuwapa wazazi wake kama blanket na kanga binti anawaka ile mbaya kuwa hata kuwa na amani kabisa akiwa ndani ya ndoa akifanya hivyo.

Jamaa hana hamu naye ananiomba ushauri hapa kwani kaamkia kwangu asubuhi hii akitaka kuniuzia boda boda yake ama niichikue bond. Ushauri tafadhari Wajumbe.

Mnisamehe kwa uandishi sio mzuri.
 
anaburuzwa huyo jamaa mpaka huruma
atamuua kwa presha huyo bint
 
  • Thanks
Reactions: J C
Duuh lakini huyo jamaa ni bendera fata upepo cha msingi atulize akili, kwanini asifunguke kwa wazazi wa demu,kama vipi akache ndoa kwanza mpaka atakapo jiweka pouwa, kwani hapo kalazimishwa na niwangapi wanavalishwa pete na wanaachana hata kabla hawajafunga ndoa?
Na atataka kukuuzia boda boda sindio kurudishana nyuma kimaendeleo huyo demu ni zero brain!!
 
  • Thanks
Reactions: J C
Kiukweli mi sidhani kam huyo binti anampenda jamaa toka moyoni kwasababu angekua na mapenzi ya kweli lazima angeona jinsi ya kumsaidia na si kumwacha aumie kiasi hicho.
Ushauri wangu kwa huyo jamaa ni kwamba anatakiwa afikiri kwa undani na afanye maamuzi yenye busara kama mwanaume alafu kama mtu aliye elimika.
Kama mtu leo hii hamjafunga hata ndoa anakusumbua je mtakapo funga hiyo ndoa yenu itadumu kweli? Au ndo ile mwezi mmoja tu mnachokana na kila mtu anatafuta uelekeo.Asiangalie muda gani wamekua na hayo mahusiano aangalie afya ya hayo mahusiano yao iko vipi.
Ni mtazamo wangu tu.
 
Heee anataka binti ampe hela? Ili akajichumbie????

Huyo rafiki yako nae, anajijua uwezo hana kwa sasa kwa nini apelekeshwe?
 
Duuh lakini huyo jamaa ni bendera fata upepo cha msingi atulize akili, kwanini asifunguke kwa wazazi wa demu,kama vipi akache ndoa kwanza mpaka atakapo jiweka pouwa, kwani hapo kalazimishwa na niwangapi wanavalishwa pete na wanaachana hata kabla hawajafunga ndoa?
Na atataka kukuuzia boda boda sindio kurudishana nyuma kimaendeleo huyo demu ni zero brain!!

Mshikaji alitaka kumwona Baba mtu binti akagoma akisema kuwa baba yake hausiki anayehusika ni baba yake Mkubwa naye ndiye mtoa maamuzi yote. Pia unamaanisha nini kusema bendera fuata upepo?. Ila binti ndio kabadilika sana hasa kipindi an achoona ndoa iko mlangoni demand zinakuwa nyingi ka anaolewa na riz moko.
 
Za mida wajumbe?. Kuna friend of mine hapa ananipa mchapo akitaka kujua afanye nini.
Ana binti aliyenaye katika mahusiano kwa miaka kadhaa sasa. Kijana anasoma ila ana gratuate this year. Binti kamkaba jamaa wafunge ndoa jamaa naye kaona ni sawa kwani kaona binti amepass viwango kuwa naye kimaisha ila jamaa anakwama sehemu moja ana ajira somewhere ya mkataba na analipwa 80% ya mshahara kwa mwezi kwa sababu kiwango chake cha elimu hakijafikia lengo la mshahara kamili. Kwa hili binti akamtia moyo kuwa asijali kabisaaa kwani kwao mahari anataja binti na akamhakikishia kuwa haitazidi laki tano ama sita jamaa kwa kuona hivyo na kwa kuzingatia umri wa ampendaye unamtupa mkono akajitosa binti akawakusanya ndugu zake wengi kuwapa taarifa kuwa amepata mchumba in short jamaa anamuuliza binti ampe siri ndg wanataka kiasi gani ili awaelezee washenga watakapo kwenda wajue kiasi binti anamwambia jamaa ajiandaye kwa milioni moja na nusu khe jamaa kasara mbaya ukitegemea ni miezi kama mitano tu imebaki kwao kufunga ndoa. Binti ni form four failure ila anakibarua mkoa mwingine mbali jamaa mawasiliano ni Simu tu. Jamaa akaa kimnya akajikunja kwani wazazi wa binti waligomea hapo hawataki chini ya hapo.
Jamaa amekubali. Sasa wameenda kwenye swara la Pete ya engagement binti anataka ya dhahabu si chini ya gramu mbili jamaa anamsihi amsaidie japo kidogo binti anagoma kwa kusema nini maana ya kuwa engaged?. Anamwambia wanunue Pete ya silver anamwambia ataiweka kwenye kidole cha nani?. Sasa hivi wamebakiza siku chache jamaa akatoe hiyo mahari anamwambia binti amsaidie pesa kidogo za kununulia vitu vya kuwapa wazazi wake kama blanket na kanga binti anawaka ile mbaya kuwa hata kuwa na amani kabisa akiwa ndani ya ndoa akifanya hivyo. Jamaa hana hamu naye ananiomba ushauri hapa kwani kaamkia kwangu asubuhi hii akitaka kuniuzia boda boda yake ama niichikue bond. Ushauri tafadhari Wajumbe. Mnisamehe kwa uandishi sio mzuri.
Mwanangu we ni mwanaume mchulie jamaa kama ni ndugu yako....je ungemuacha amuoe huyo binti?
Kiukweli hapo hamna ndoa na atamsumbua sana huyo jamaa!
 
  • Thanks
Reactions: J C
mkuu kiukweli jamaa atulie afanye maisha mengine ampe binti mda ni fedheha kwake.... binti anataka kulazimisha ndoa alafu maujanja ya kufanya hivyo ajui
 
hapo hamna mke kaka,mshkaji wako amebug.Hicho anachokionesha sasa huyo binti ndo tabia yake halisi,na huenda hajayakunjua full makucha yake,kimbembe akishafunga naye ndoa.Aachane na mipango hyo kwa sasa,ajijenge then atafute mwanamke mwingine wa kuoa,SIO HUYO TENA!
 
  • Thanks
Reactions: J C
Unamaanisha ampe demu kibuti au?.

Naomba kuuliza hivi mahari kubwa hivyo ni ya nini,unanunua ng'ombe?wanaume nyie sijui mnaakili gani!!mi sioni sababu ya kupigwa mahari kubwa kiasi hicho,halafu huyo msichana hampendi mwenzie anataka sifa wakati mwanaume wake hana kitu,kwani akimuacha hatapata mwanamke mwingine au huyo ndo mwanamke mwisho????haaaa!!
 
  • Thanks
Reactions: J C
JC Kaaah!! mshikaji naye hang'astuki tu amuone baba mkubwa kwani baba /mzazi hayupoi hai? na siku baba mtu akisema sikutambui kama mkwe wangu mshikaji atafanyaje coz baba mtu ndo mzaa chema na yupo hai na mshikaji nae hadauti kwanini demu anakataa asimuone baba mzazi wa demu? sas binti kabadilika kuona toi ipo mlangoni JE? akiingia ndani kabisa itakuaje mwambie mshikaji aweke demu kapunu huyo hafai kwani aibu itakuwa kwa nani demu au mshkaji?
Mshikaji alitaka kumwona Baba mtu binti akagoma akisema kuwa baba yake hausiki anayehusika ni baba yake Mkubwa naye ndiye mtoa maamuzi yote. Pia unamaanisha nini kusema bendera fuata upepo?. Ila binti ndio kabadilika sana hasa kipindi an achoona ndoa iko mlangoni demand zinakuwa nyingi ka anaolewa na riz moko.
 
Last edited by a moderator:
misschagga na ataumia vibaya ngoja uone mtu mzima anaingia choo cha watoto anakalia poti sasa ivi ndo yale lara1alikua anasema kuusu ndoa teh teh@Lara1 embu ukuje uku uone mambo yandoa haya fanya shuta!!
jamaa anataka kuangukia pua
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom