MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,185
- 24,055
Lowassa tunayeambiwa ana maono, anawaagiza eti watanzania wote wakasome hotuba yake kuhusu maona yake ya Tanzania aitakayo kwenye tovuti ya CHADEMA. Kweli?
Lowassa hafahamu kuwa, kwa mujibu wa data kutoka TCRA na NBS, Watanzania zaidi ya milioni 35 hawana internet access kutokana na umasikini na ukosefu wa umeme wa uhakika katika maeneno mengi hasa vijijini. Lowassa anayedai anafahamu matatizo ya Watanzania hafahamu ni watanzania wachache wanaweza kuisoma hiyo hotuba yake.
Lowassa hafahamu kuwa gharama ya kununua smart phone ni anasa isiyowezekana kwenye familia nyingi nchini.
Kumbe kupanda daladala na kuongea na Mama Lishe haukuwa usanii bali alikuwa kweli anataka kufahamu matatizo ya msingi ya Watanzania pamoja na kuwahi kuwa Waziri Mkuu.
Ukweli ni kwamba, Lowassa hana maono na hana hata msingi mmoja anaousimamia. Historia haimuonyeshi kuwa ni nabii ingawa baadhi ya watu wamempa unabii na amekuwa ni kama ideology kwa sasa.
Lakini hawa Watanzania wanaomshabikia Lowassa wamekuwa sawa na wale watu wazima wanaohubiriwa na mchungaji mmoja huko Afrika Kusini na bila kufikiri kukubali kula majani, nyoka, na hata kuvua nguo! Hawana tofauti na wafuasi wa Kibwetere waliochomwa moto na kufia kanisani.
Kwa maono haya haishangazi kuzisoma data zinazoonyesha Monduli ni moja ya Jimbo masikini sana kiuchumi na kijamii nchini.
Hivi karibuni niliwauliza watu wanaomshabikia swali hili: Lowassa amefanya nini kwao Monduli akiwa Mbunge wa miaka zaidi ya 30, Waziri na Waziri Mkuu? Je, Monduli kajenga shule za kutosha, kawaletea maji ya kutosha, kajenga kiwanda cha nyama? Kajenga kiwanda cha maziwa au jibini? Jibu ni hapana.
Wamasai wa Monduli ni wafugaji; je amewabadilisha kiasi cha kuwafanya wafuate ufugaji wa kisasa? Jibu pia ni hapana. Isitoshe, Wamasai wanalalamika kila siku kuhusu matatizo ya ardhi yanayowakabili; Je, Lowassa amewasaidia vipi katika suala hilo? Hata hapa jibu ni hajawasaidia.
Lowassa anadai eti yeye ni mtu wa kuleta mabadiliko. Si angeanza kwanza kuibadili Monduli yake kabla hajaibadili Tanzania nzima? Lowassa amekuwa mbunge kwa miaka zaidi ya miaka 30 hakuna alichokifanya kuwainua wana Monduli kiuchumi na kijamii.
Dk. Slaa amekuwa Mbunge wa Jimbo la Karatu kwa miaka 15 lakini ameacha mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa Karatu ukilinganisha na Lowassa ambaye pamoja na kuwa mbunge kwa zaidi ya miaka 30, amewahi pia kuwa Waziri na Waziri Mkuu wa Tanzania. Huduma za elimu na maji ziko kwa kiwango cha juu katika Jimbo la Karatu ukilinganisha na Jimbo la Monduli.
Ukweli ni kwamba hata alipokuwa waziri wa ardhi aligawa viwanja kwa rafiki zake akina Ladwa wakajenga hoteli ya Golden Tulip. Ni kipindi hicho cha uwaziri wake pia kipande cha Gymkhana kilimegwa na kujengwa Serena Hotel. Je, alishughulikia migogoro ya ardhi ya wananchi wa kawaida? La hasha.
Wanaomzunguka wanazungumzia sera zake zipi? Kwamba wakiingia ikulu watafanya nini? Nijuavyo, maswahiba wake tayari wameshajigawia madaraka na miradi kana kwamba tayari wameshinda uchaguzi!
Inasikitisha kwamba baadhi ya Watanzania (kwa wiki hizi nne) wameshindwa kuyaona yote hayo, na wanamshabikia tu kwa kufuata mkumbo kama vile hawana akili nzuri. Lakini nina hakika watanzania wengi wameanza kuyaona mapungufu mengi ya Lowassa.
Baadhi ya Viongozi wakuu wa CHADEMA waliyaona matatizo ya Lowassa na wakasema katika thread hii,
Kwa ulafi wa madaraka, leo baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA ndiyo wamekuwa watetezi wa Lowassa.
Lowassa hafahamu kuwa, kwa mujibu wa data kutoka TCRA na NBS, Watanzania zaidi ya milioni 35 hawana internet access kutokana na umasikini na ukosefu wa umeme wa uhakika katika maeneno mengi hasa vijijini. Lowassa anayedai anafahamu matatizo ya Watanzania hafahamu ni watanzania wachache wanaweza kuisoma hiyo hotuba yake.
Lowassa hafahamu kuwa gharama ya kununua smart phone ni anasa isiyowezekana kwenye familia nyingi nchini.
Kumbe kupanda daladala na kuongea na Mama Lishe haukuwa usanii bali alikuwa kweli anataka kufahamu matatizo ya msingi ya Watanzania pamoja na kuwahi kuwa Waziri Mkuu.
Ukweli ni kwamba, Lowassa hana maono na hana hata msingi mmoja anaousimamia. Historia haimuonyeshi kuwa ni nabii ingawa baadhi ya watu wamempa unabii na amekuwa ni kama ideology kwa sasa.
Lakini hawa Watanzania wanaomshabikia Lowassa wamekuwa sawa na wale watu wazima wanaohubiriwa na mchungaji mmoja huko Afrika Kusini na bila kufikiri kukubali kula majani, nyoka, na hata kuvua nguo! Hawana tofauti na wafuasi wa Kibwetere waliochomwa moto na kufia kanisani.
Kwa maono haya haishangazi kuzisoma data zinazoonyesha Monduli ni moja ya Jimbo masikini sana kiuchumi na kijamii nchini.
Hivi karibuni niliwauliza watu wanaomshabikia swali hili: Lowassa amefanya nini kwao Monduli akiwa Mbunge wa miaka zaidi ya 30, Waziri na Waziri Mkuu? Je, Monduli kajenga shule za kutosha, kawaletea maji ya kutosha, kajenga kiwanda cha nyama? Kajenga kiwanda cha maziwa au jibini? Jibu ni hapana.
Wamasai wa Monduli ni wafugaji; je amewabadilisha kiasi cha kuwafanya wafuate ufugaji wa kisasa? Jibu pia ni hapana. Isitoshe, Wamasai wanalalamika kila siku kuhusu matatizo ya ardhi yanayowakabili; Je, Lowassa amewasaidia vipi katika suala hilo? Hata hapa jibu ni hajawasaidia.
Lowassa anadai eti yeye ni mtu wa kuleta mabadiliko. Si angeanza kwanza kuibadili Monduli yake kabla hajaibadili Tanzania nzima? Lowassa amekuwa mbunge kwa miaka zaidi ya miaka 30 hakuna alichokifanya kuwainua wana Monduli kiuchumi na kijamii.
Dk. Slaa amekuwa Mbunge wa Jimbo la Karatu kwa miaka 15 lakini ameacha mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa Karatu ukilinganisha na Lowassa ambaye pamoja na kuwa mbunge kwa zaidi ya miaka 30, amewahi pia kuwa Waziri na Waziri Mkuu wa Tanzania. Huduma za elimu na maji ziko kwa kiwango cha juu katika Jimbo la Karatu ukilinganisha na Jimbo la Monduli.
Ukweli ni kwamba hata alipokuwa waziri wa ardhi aligawa viwanja kwa rafiki zake akina Ladwa wakajenga hoteli ya Golden Tulip. Ni kipindi hicho cha uwaziri wake pia kipande cha Gymkhana kilimegwa na kujengwa Serena Hotel. Je, alishughulikia migogoro ya ardhi ya wananchi wa kawaida? La hasha.
Wanaomzunguka wanazungumzia sera zake zipi? Kwamba wakiingia ikulu watafanya nini? Nijuavyo, maswahiba wake tayari wameshajigawia madaraka na miradi kana kwamba tayari wameshinda uchaguzi!
Inasikitisha kwamba baadhi ya Watanzania (kwa wiki hizi nne) wameshindwa kuyaona yote hayo, na wanamshabikia tu kwa kufuata mkumbo kama vile hawana akili nzuri. Lakini nina hakika watanzania wengi wameanza kuyaona mapungufu mengi ya Lowassa.
Baadhi ya Viongozi wakuu wa CHADEMA waliyaona matatizo ya Lowassa na wakasema katika thread hii,
Kwa ulafi wa madaraka, leo baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA ndiyo wamekuwa watetezi wa Lowassa.