Kumbe kiswahili ni Kiarabu kitupu!

How comes mie sielewi kiarabu kabisa kama kiswahili ni kiarabu?
 

Ukitaka kujifurahisha zaidi, unaweza ukajiaminisha pia kuwa dunia nzima wenyeji walikuwa waarab, na watu wengine walikuwa wakuja tu.

Haiyamkiniki, kwa jinsi waarab wanavyopenda kuzaliana kwa wingi, wawe wachache hivi kwenye bara la africa kama kweli wao ndio wenyeji.

Na tatizo linakuja pale kila mwenye "genes" mbili tatu na anafuata uislam basi anajiita mwarabu, hata kama ni mmanyema mwenye pua kubwa kama ngumi.
 

Nani alikudanganya kuwa Waarabu ni kidogo Afrika?

Waarabu wako wengi Afrika kuliko pengine popote duniani.
Nnajuwa sana kuwa watu kama wewe walioenda shule za kusomea ujinga wanadhani kuwa Waarabu ni weupe tu.

Uarabu si rangi si taifa si nywele. Uarabu ni lugha.

Hata wewe una asilimia kubwa ya Uarabu ikiwa lugha mama kwako ni Kiswahili.

Maswali yangu hujayajibu, kama hukuyaona utakuwa ni wale waliosomea ujinga na kiherehere juu.
 

Waliosomea ujinga ni watu kama wewe, unayefikiri kuongea kiarabu au kiswahili ndio uarabu.
Mbona wazenji wanaojiita ni waarabu, hukanwa wakienda middle East? Wewe mwenyewe na uarabu-koko wako ukienda kule wanakukataa kuwa wewe ni mwarabu.
 
Kiswahili ni kikongo
 
Punguza jazba atakuelewa tu huyo muungwana wa bara.
 
Kiswahili kina maneno mengi ya kiarabu hiyo ni fact. Ila si kweli Kiswahili ni kiarabu. Kiswahili ni Kiswahili. Kiswahili kimezaliwa kwa muunganiko wa lugha mbali mbali ikiwemo kibantu, kiarabu, kiingereza, kireno nk

Ukisema Kiswahili ni kiarabu tutakosea maana ukiangalia baadhi ya herufi zipo kwenye Kiswahili ila hazipo kwenye kiarabu.

Mfano: p, e, o, v, nk. Hizo herufi hazipo kwenye kiarabu. Japo kwasasa wanajitahid kuziingiza hizo herufi lakin bado hazijaanza kutumika rasmi. ( Waarabu mtihan mkubwa kutamka PEPSI kwa ufasaha wanatamka BEBSI).

sasa kukiita kiswahili ni kiarabu ni makosa. Kiarabu ni Kiarabu na Kiswahili ni Kiswahili
 


Kama Kiswahili ni Kiarabu basi pia lugha karibia zote Tanzania kama Kipare, kisukuma, kipogoro, kinyakyusa, kimachame n.k. pia ni Kiarabu kwa maana lugha zote hizo zaidi ya 80% Misamiati yake ni ya Kiswahili au inafanana na Kiswahili hivyo Kibantu pia ni Kiarabu kama unaamini Kiswahili ni Kiarabu na kama ni hivyo ina maana sisi pia ni Waarabu!
 
Si kweli mkuu endelee kuchimba utaona tofauti kubwa iliyopo kati hizi lugha. Tena kiarabu ni kigumu kujifunza kuliko kiswahili au kiingereza.

Mfano:
Kwenye kiarabu unapaswa kuongea kitu kwa jinsia yake. Mfano utakavyoongea kwa mwanamke ni tofauti kwa mwanaume.

Umoja na wingi sio rahisi kama lugha nyingine. Kwenye kiarabu kuna wingi mkiwa wawili na wingi mkiwa zaidi ya wawili. Kuna wingi kwa wanawake/wanaume wakiwa wawili na wanawake/wanaume wakiwa zaidi ya wawili.

Bado kuna kujifunza herufi ambazo hazipo kwenye kiswahili utamkaji wake nao ni changamoto.

Ila the good thing kwenye kiarabu ni katika uandishi kama ukiweza kulitamka neno kwa ufasaha ndivyo utakavyoliandika hivyo hivyo baada ya kuzijua herufi zake kwa ufasahA. Sio kama kiingereza unatamka vingine unaandika vingine.

Na the worst case in kiarabu ni katika kusoma hasa kama ni beginner. Hawa jamaa maandishi yao hawaweki hizi ilabu (harakhat) a ,e, i, o, u ambapo kwa kiarabu zipo 3 tu a, i, u. Hebu jenga picha hapo uone. Ni mwendo wa kuotea neno ila ukishayajua maneno mengi zaid utaweza kusoma vizuri.

Usijidanganye mkuu kufanana kwa misamiati iliyopo katia lugha hizi mbili ukamalizia kwa kusema kiswahili ni kiarabu.
 
 
Waliosomea ujinga ni watu kama wewe, unayefikiri kuongea kiarabu au kiswahili ndio uarabu.
Mbona wazenji wanaojiita ni waarabu, hukanwa wakienda middle East? Wewe mwenyewe na uarabu-koko wako ukienda kule wanakukataa kuwa wewe ni mwarabu.


Naam, wanakanwa kwa sababu si Waarabu wa "Middle East" ni Waarabu wa Zanzibar.

Napenda uelewe kuwa "wazenji" kujiita Waarabu siyo kosa kwani wana hisoria ndefu ya kale kuwa ni nchi ya Kiarabu, tena siyo kuwa iliishia huko visiwani tu.

Hata hapo Tanganyika na zaidi ya Tanganyika iliwahi kuwa "Zenji". Jee unajuwa maana ya "Zenji"? Hilo ni neno la Kiarabu kabisa 100%.

Pata historia ya Dola ya "Zenj Empire" kwa ufupi:


Faidika na darsa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa
 

= usirudie
 


Haya yote niliyoewekea rangi nyekundu yanatokana na Kiarabu.

Piga asilimia ngapi kwa ujumla, asilimia hizo hizo ndiyo Uarabu wako.
 
Pata historia ya Dola ya "Zenj Empire" kwa ufupi:
youtube N3EAirHqDbU
Faidika na darsa la FaizaFoxy; Uliza chochote utajibiwa

Foxy, huyu msemaji uliyemleta hana habari za undani za historia (sijui kama ni jukwaa hapa?).
Maskini wasio na elimu wakiaanza kuamini haya.

Hapakuwa "Empire of Zanj". Sultani wa Omani alipata kipaumbele kwenye pwani la Waswahili baada ya kutoka kwa Wareno manmo mwaka 1700. Alipokuwa na ghasia kwake Omani karne ya 19 alihamisha makao makuu kwenda Zanzibar na kwa miaka kadhaa mji mkuu wa "Omani Empire" ilikuwepo Unguja. Baadaye Waomani waligawana tena kuwa sehemu mbili. Na hao Waomani walitia sahihi mara kadhaa kupinga biashara ya watumwa kwa shabaha ya kupata usaidizi wa Waingereza lakini waliendesha biashara hii hadi miaka ya kwanza ya ukoloni.

Menginevyo walikuwepo watu (si wengi nyakati zile) katika Afrika ya Mashariki kabla ya kufika kwa Waarabu. Ni kweli Waarabu, Waswahili na Uislamu vilikuwepo kwenye pwani ya Afrika ya Mashariki kabla ya kufika kwa makabila mengi wa Kibantu. Hata hivyo hawakuwa wa kwanza . Kiswahili kilianza kwa sababu wasemaji wa Kibantu walikuwepo wakati wafanyabiashara Waarabu walifika na katika mkutano huu Kiswahili kilianza.

Unachosema kuhusu "Uarabu" na Afrika ni kweli tu kwa Afrika kaskazini ya Sahara. Huko Waarabu walivamia wakatawala na kubadilisha utamaduni wa wazalendo. Nje ya hapo kulikuwa tu na hao wahamiaji Waarabu katika Afrika ya Mashariki waliochanganyika na watu wa pwani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…