kweli watu wengi wanapoteza maisha (wengi huapasuka vichwa)hususani abilia wa bodaboda kwa sababu hawana safety gears (helment), usalama sio kwa dereva tu hata abiria. Niliwahi pita morogoro mjini, kila bodaboda ilikuwa na helment mbili ukionekana abilia haujavaa helment utapata matatizo na faini juu. nilipenda utaratibu huo utumike nchi nzima. nadhani hii ilikuwa kwa sababu matukio yalizidi.
sasa nashangaa picha ya hawa waheshimiwa wetu wanasherekea bila hata wasiwasi wakati hawako salama. ikitokea kwa bahati mbaya ajali ndogo tu ukaangukia kichwa ndio kwa heri au Mungu saidia kichwa kikaburuzwa kwenye rami unabaki na jeraha la maisha.
Mungu atusaidie.