Kumbe hata bila ya Mawaziri Nchi inaenda

Kumbe hata bila ya Mawaziri Nchi inaenda

Magnesium

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2014
Posts
317
Reaction score
185
Wakuu habari ya jioni? Nimekaa nikatafakari juu ya utendaji wa Mh. Rais Dr. JPM ndani ya mwezi mmoja na kuona mabadiliko makubwa bila hata ya usaidizi wa baraza la mawaziri na bado mambo yanaenda yakinyooka.. Kuanzia suala la Muhimbili, TRA, TANESCO na Bandari inaonekana wazi kabisa kazi iliyofanywa na Dr. JPM na Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa ni kubwa.

Mpaka sasa sijaona pengo la kutokuwepo kwa baraza la mawaziri. Natamani Mh Rais asitangaze hilo baraza la mawaziri hadi mwakani. Peke yake atosha. Hao mawaziri wakiingia huenda wakaanza kuleta mlolongo mrefu wa utatuaji wa matatizo ya wananchi.

Kingine kinachonifurahisha ni Mh Rais kutosafiri nje ya nchi tangu ameapishwa. Inaonesha jinsi gani yuko makini na matatizo yetu zaidi kuliko ziara za nje. Kwa hili nampa Dr. JPM heko. Cha msingi Watanzania tumuungo mkono na kumtia moyo ikiwa na pamoja na kumuombea aendelee KUTUMBUA MAJIPU...
 
nisahihi hilo Na tunaamini hata baraza lake litafuata jasi ya kiongozi Wa juu
 
Tanzania ni ya watanzania hata kama watanzania wenyewe ni mbumbumbu na wakora. Ndo maana tunasema katiba ambayo inampa nguvu kubwa Rais ya kuweza hata kuendesha nchi bila kuwa na mawaziri haitufai kabisa. Nguvu hizi ni kubwa sana hasa mkimpata kiongozi asiyekuwa na maadili.

Tunaomba baraza la mawaziri litangazwe haraka na mchakato wa katiba uanze mara moja. Tuna bahati kuwa Rais Magufuli ni mzalendo mwenye uchungu na nchi yake na wananchi wake, lakini ipo siku tutakujakupata hasara kubwa wote kwa kutumia katiba hii ya sasa.

Tutengeneze katiba ambayo rais anaelekezwa nini cha kufanya na nini asifanye.

Mawaziri ni muhimu kwa mujibu wa utawala bora.
 
Na huu ndiyo Ujinga mkubwa tulio nao Waafrika wengi, kwani unafikiri Katiba ni nini? Si karatasi tu, sasa unafikiri Karatasi inawezaje kumzuia mtu mbaya kufanya mabaya?

Wakenya wana Katiba mpya, ambayo imezuia yote hayo na kupunguza madaraka ya Raisi, sasa imewasaidia nini? Angalia wanavyolia sasa hivi na wizi na rushwa iliyopitiliza, upendeleo watu wanapewa vyeo na kulindwa kwa kuwa tu wanaukaribu na Raisi sasa hiyo Katiba imesaidia nini?

Acheni Ujinga Waafrika, cha muhimu ni kupigania kuondoa umaskini kwanza kwa kuwekeza kwenye Elimu tukifanikiwa hapo mengine yote yatafuatia yenyewe tu, watu walioeleimika na wasio masikini hawawezi kuchagua kiongozi mbaya kuwaongoza lkn kama watu wanabakia kuwa masikini na hawana Elimu hata ukichukuwa Katiba ya Japani au sijui Kanada bado Raisi kama ni mbaya ataharibu tu nchi kwa kuikandamiza katiba hiyo hiyo!
 
Ni kweri katiba inamtaka Rais kuwa na baraza la mawaziri lakini haimpi muda gani aliweke baraza la mawaziri wala idadi. Lakini pia tutazame uteuzi alioufanya Obama kwa mfano alitumia miezi mingapi kutengeneza serikali yake? au Rais wa Nigeria ametumia muda miezi 6 kuwa na baraza la mawaziri.
Rais wetu acha ajipange na afanye screening ya kutosha kupata aina ya watu anaowahitaji kufanya nae kazi.
 
Hatuwataki hata kama.....

Watakuja kupunguza tu kasi ya Magufuli hakuna lolote

Si mmeishapata ubunge, why bado tu mwatolea mate uwaziri

Ni kuongeza tu gharama bure wakati hakuna chochote mnafanyaga........ yako wapi kina Sitta na Mwakyembe, sijui Mwigulu na Saada, madudu tupu!!!

Safari hii tunakwenda na makatibu wa wizara tu baasi
 
yaani huu ndo ujinga na ulofa aliousema yule mzee jangwani
mlipokuwa na mawaziri 60 walifanya nini zaidi ya kukanyagana tu,
mlipopunguza wakabaki 45 kulikuwa na impact gani? pumba kabisa
Juzi mwanasheri mkuu wa serikali katole ufafanuzi kuwa katiba haisemi mawaziri wateuliwe lini, isipokuwa inaelekeza kuwa bunge haliwezi kukaa bila baraza la mawaziri, so vuta subira, kuna bunge januari 2016, baraza litakuwa tayari
kama uliahidiwa au baba yako au ndugu yako mwambie awe mpole
ni hayo tu
 
vipi mmejiandaa kwa sherehe ya kujipongeza kwa uteuzi ?
 
Buhari wa Nigeria alikaa miezi 6 bila mawaziri, na watu wanakiona cha mtema kuni pale panapofichuka siri za wizi.
 
Angewahi kulitangaza pengine leo Mwaki-dodo angekuea waziri, lakini siku zinavyoenda ndio anazidi kuwajua
 
Magufuli akisema anataka Katiba nawee utamuunga mkono kwa Furaha nchi hii bado tunasafari ndefu

Katiba hii bado mim naiona nzuri ,maana inampa mkuu wa nchi supa power ,sasa hii ya kenya inayosifiwa imeleta kitu gani kipya mbona rushwa kwa kama kawa
 
Unamtaka Mr President achague baraza la mawaziri mara moja.....hahahaaaa muache Magufuli apate muda wakuchunguza watu anaowataka muda ukifika utawaona.
 
Tanzania ni ya watanzania hata kama watanzania wenyewe ni mbumbumbu na wakora. Ndo maana tunasema katiba ambayo inampa nguvu kubwa Rais ya kuweza hata kuendesha nchi bila kuwa na mawaziri haitufai kabisa. Nguvu hizi ni kubwa sana hasa mkimpata kiongozi asiyekuwa na maadili. Tunaomba baraza la mawaziri litangazwe haraka na mchakato wa katiba uanze mara moja. Tuna bahati kuwa Rais Magufuli ni mzalendo mwenye uchungu na nchi yake na wananchi wake, lakini ipo siku tutakujakupata hasara kubwa wote kwa kutumia katiba hii ya sasa. Tutengeneze katiba ambayo rais anaelekezwa nini cha kufanya na nini asifanye.

Mawaziri ni muhimu kwa mujibu wa utawala bora.

Una matatizo wewe. Yaani umeisoma katiba yote sura kumi zote haukuona inakotamka kuwepo kwa baraza la mawaziri? Unahisi ni rais tu kuamua au kutoamua? ama chango linakusumbua?
 
Hatuna haja nao hata walipokuwepo awakusaidia chochote
 
Back
Top Bottom