Anselm
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 1,710
- 291
Mojawapo wa utofauti ambao nimekuwa nikiamini umeletwa na team ya Azam ni undeshwaji wa kisasa wa team hiyo inayomilikwa na mmoja wa matajiri wakubwa sana hapa nchini. Katika team hii sikutarajia kuona/kusikia mambo ambayo nimekuwa nikiyaona na kuyasikia kwenye team za Simba na Yanga,ni lazima niseme nimesikitishwa sana na shutuma zilizotolewa na uongozi wa team hii kuwa kuna wachezaji walicheza chini ya viwango vyao ili kuruhusu Yanga kuchukua ubingwa....jamani nyie ni Azam haya mambo ya kushikana uchawi ooh fulani kafungisha fulani kacheza chini ya kiwango embu ziachieni hizi team 2 (za Simba na Yanga),ni wajibu wenu kujitambua kwani nyie hata akina Mzee Akilimali hamna kila kitu mnaendesha kisasa sasa inakuwaje mnajisahaulisha kuwa mchezo wa mpira una matokeo ya aina 3 kushinda,kushindwa na kutoka sare.
Eti Salum Aboubakar,Mrisho Ngassa na Dida wamewahujumu kwenye mechi na Yanga,mbona hamkuwashutumu kwenye mechi na Simba fainali ya Urafiki ambako mlifungwa,au hujuma ni pale mnapofungwa na Yanga tu? acheni kuweweseka bwana mnawavunja mioyo hawa Vijana wadogo wanaochipukia,mtaharibu.
Eti Salum Aboubakar,Mrisho Ngassa na Dida wamewahujumu kwenye mechi na Yanga,mbona hamkuwashutumu kwenye mechi na Simba fainali ya Urafiki ambako mlifungwa,au hujuma ni pale mnapofungwa na Yanga tu? acheni kuweweseka bwana mnawavunja mioyo hawa Vijana wadogo wanaochipukia,mtaharibu.