Kumbe hata Azam wanaweweseka!!

Kumbe hata Azam wanaweweseka!!

Anselm

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2010
Posts
1,710
Reaction score
291
Mojawapo wa utofauti ambao nimekuwa nikiamini umeletwa na team ya Azam ni undeshwaji wa kisasa wa team hiyo inayomilikwa na mmoja wa matajiri wakubwa sana hapa nchini. Katika team hii sikutarajia kuona/kusikia mambo ambayo nimekuwa nikiyaona na kuyasikia kwenye team za Simba na Yanga,ni lazima niseme nimesikitishwa sana na shutuma zilizotolewa na uongozi wa team hii kuwa kuna wachezaji walicheza chini ya viwango vyao ili kuruhusu Yanga kuchukua ubingwa....jamani nyie ni Azam haya mambo ya kushikana uchawi ooh fulani kafungisha fulani kacheza chini ya kiwango embu ziachieni hizi team 2 (za Simba na Yanga),ni wajibu wenu kujitambua kwani nyie hata akina Mzee Akilimali hamna kila kitu mnaendesha kisasa sasa inakuwaje mnajisahaulisha kuwa mchezo wa mpira una matokeo ya aina 3 kushinda,kushindwa na kutoka sare.
Eti Salum Aboubakar,Mrisho Ngassa na Dida wamewahujumu kwenye mechi na Yanga,mbona hamkuwashutumu kwenye mechi na Simba fainali ya Urafiki ambako mlifungwa,au hujuma ni pale mnapofungwa na Yanga tu? acheni kuweweseka bwana mnawavunja mioyo hawa Vijana wadogo wanaochipukia,mtaharibu.
 
Mojawapo wa utofauti ambao nimekuwa nikiamini umeletwa na team ya Azam ni undeshwaji wa kisasa wa team hiyo inayomilikwa na mmoja wa matajiri wakubwa sana hapa nchini. Katika team hii sikutarajia kuona/kusikia mambo ambayo nimekuwa nikiyaona na kuyasikia kwenye team za Simba na Yanga,ni lazima niseme nimesikitishwa sana na shutuma zilizotolewa na uongozi wa team hii kuwa kuna wachezaji walicheza chini ya viwango vyao ili kuruhusu Yanga kuchukua ubingwa....jamani nyie ni Azam haya mambo ya kushikana uchawi ooh fulani kafungisha fulani kacheza chini ya kiwango embu ziachieni hizi team 2 (za Simba na Yanga),ni wajibu wenu kujitambua kwani nyie hata akina Mzee Akilimali hamna kila kitu mnaendesha kisasa sasa inakuwaje mnajisahaulisha kuwa mchezo wa mpira una matokeo ya aina 3 kushinda,kushindwa na kutoka sare.
Eti Salum Aboubakar,Mrisho Ngassa na Dida wamewahujumu kwenye mechi na Yanga,mbona hamkuwashutumu kwenye mechi na Simba fainali ya Urafiki ambako mlifungwa,au hujuma ni pale mnapofungwa na Yanga tu? acheni kuweweseka bwana mnawavunja mioyo hawa Vijana wadogo wanaochipukia,mtaharibu.

Wamezidiwa na uzoefu, bado wachanga hao...Yanga bado itabaki Yanga milele..wana kipigo kingine Ligi kuu wasubiri!
 
Wataweweseka sana mwaka huu ngoja ligi ianze hasira zote za mwaka jana zitawaishia.
 
Back
Top Bottom