Kumbe halikuwa zuio la mikutano ya kisiasa bali ni zuio la mashindano ya kisiasa

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Mh Rais Magufuli alitoa tamko kuzuia mashindano ya kisiasa kwa nia njema kabisa atekeleze ilani ya chama chake kwa kuchapa kazi kama kauli mbiu ya chama chake inavyosisitiza"hapa kazi tu"

Lakini hakuzuia mikutano ya kisiasa kwa nia njema pia akitaka pasiwe na vurugu wala mwingiliano wa mikutano hiyo. Hivyo wabunge walipewa nafasi ya kuweza kunadi sera za vyama vyao na kuwaeleza wananchi waliowachagua kuwa nini wamefanya.kwenye majimbo yao tena kwa kufuata utaratibu.

Kumbe hata kwa wenzetu ambao huwa wanajinadi kuwa eti wanademokrasia iliyokomaa mshindi wa urais akishapatikana huwezi kumuona, mpinzani ananza kuzunguka nchi nzima kuanza kuleta upinzani katika kutekeleza ilani ya chama tawala.Mfano hata Usa hivi sasa ni D.Trump tu ameachiwa ulingo huo mpaka amalize muda wake.

Hapa nchini Tokea zuio la upinzani wa kisiasa na sio zuio la mikutano ya kisiasa litolewe vyama vya upinzani vinalalamika kuwa ndio sababu ya kuporomoka kisiasa na kukosa mvuto kwa wananchi.

Wanasahau kabisa kwamba zuio hilo lilikuwa na nia nzuri ya kuwapa wananchi fursa ya kufanya kazi zao kama uvuvi au kilimo na biashara,kuliko kusubiri helkopta kuanzia asubuhi hadi jioni.

Pia aliyepo madarakani ametumia fursa nzuri aliyopewa na wananchi kudhibiti ubadhirifu,rushwa ,kutekeleza miradi kama ujenzi wa vituo vya afya na na hospital,kujenga barabara na madaraja n.k hivyo amejijengea imani kubwa kwa wananchi.

Hivyo kuleta kisingizio ati wamezuiwa kufanya mikutano ndio sababu ya kuporomoka sidhani kama ni kweli.

Ukweli hauna chama,na mimi si mwana CCM ila nasema kweli tu.
 
Mkuu kuna ID zikiandika we ignore tu,unakuwa umeokoa muda wako!Hawa jamaa hawana hoja kabisa,yaani sijui wanasajiliwa kwa vigezo gani!
Nilitegemea uje na hoja juu ya zuio la upinzani ili watu wafanye kazi.
 
Nilitegemea uje na hoja juu ya zuio la upinzani ili watu wafanye kazi.

Ni nani aliwahi kuzuiwa kufanya kazi kwakuwa kulikuwa na mikutano? Ama kuna yoyote aliwahi kulazimishwa kuacha kazi zake ili aende kwenye mikutano ya siasa ya upinzani?
 
Ni nani aliwahi kuzuiwa kufanya kazi kwakuwa kulikuwa na mikutano? Ama kuna yoyote aliwahi kulazimishwa kuacha kazi zake ili aende kwenye mikutano ya siasa ya upinzani?
Watu walikuwa wanaacha kulima vijijini kwenda kushangaa helkopta .Matokeo yake njaa tu. Mnaambiwa watafika saa sita kumbe linafika saa kumi jioni. Tusubiri muda wa kumwaga sera haina haja ya papara.
 
Watu walikuwa wanaacha kulima vijijini kwenda kushangaa helkopta .Matokeo yake njaa tu. Mnaambiwa watafika saa sita kumbe linafika saa kumi jioni. Tusubiri muda wa kumwaga sera haina haja ya papara.

Narudia tena swali, kuna aliyelazimishwa kwenda kuangalia helkopta? Sioni kama una lolote la maana zaidi ya kuongea siasa za kitoto.
 
Narudia tena swali, kuna aliyelazimishwa kwenda kuangalia helkopta? Sioni kama una lolote la maana zaidi ya kuongea siasa za kitoto.
Hoja hapo ni kisababishi kilichokuwa kinafanya watu waache kufanya kazi. Wether walilazimishwa au la.
 
Mkuu bila kuandika uzi hata kama wa kipumbavu hulipwi buku 7 ndio maana wanahaha kuandika hata mambo yasiyo na Tija kwa Taifa

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi ni mambo ambayo hayana tija? Mnalalamika zuio la mikutano limewazoofisha! Alafu hizo buku saba hivi ni kweli au propaganda tu. Maana kwa propaganda mpo vizuri hadi mnaweka x ray picture za kufoji.
 
Mikutano ya wapinzani inasababisha mdororo wa uchumi na watu hawafanyi kazi ila mikutano ya kina Pole Pole na Bashiru nchi nzima haisababishi. Unasema wabunge walipewa nafasi kwenye majimbo yao, unajisahaulisha jinsi walivyokuwa wanakatazwa kufanya mikutano kina Zito, Msigwa, Halima na Mbowe majimboni mwao kabisa? Acha kujitoa akili basi Mkuu.
 
Hivi ni mambo ambayo hayana tija? Mnalalamika zuio la mikutano limewazoofisha! Alafu hizo buku saba hivi ni kweli au propaganda tu. Maana kwa propaganda mpo vizuri hadi mnaweka x ray picture za kufoji.
Kwa mantiki hii inaonesha mlipanga kuzunguka nchi nzima kupinga Sgr isijengwe,JNHHP isijengwe,daraja la busisi lisijengwe,daraja la wami lisijengwe,ubungo interchange isijengwe,na vituo vya afya na hospital zisijengwe.
 
Mikutano ya wapinzani inasababisha mdororo wa uchumi na watu hawafanyi kazi ila mikutano ya kina Pole Pole na Bashiru nchi nzima haisababishi. Unasema wabunge walipewa nafasi kwenye majimbo yao, unajisahaulisha jinsi walivyokuwa wanakatazwa kufanya mikutano kina Zito, Msigwa, Halima na Mbowe majimboni mwao kabisa? Acha kujitoa akili basi Mkuu.
Polepole na Bashiru wanapita kuangalia utekelezaji wa ilani ya chama. Hawa wengine kama walinyimwa ni kwa sababu za kiusalama
 
Polepole na Bashiru wanapita kuangalia utekelezaji wa ilani ya chama. Hawa wengine kama walinyimwa ni kwa sababu za kiusalama
Kuendelea kuchangia uzi kama huu ni kujikosea mwenyewe na kupoteza muda.

Sawa mkuu, umeshinda na mmefanya jambo jema sana kuwazuia wapinzani kwa miaka 4 wasifanye mikutano. Hongereni sana hakika. Mtapata thawabu duniani na mbinguni.
 
Back
Top Bottom