Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,773
- 2,383
Nimeliona hili ndani ya gaezti la Majira leo 8/10/2013.
Na habari yenyewe inasema
"JK AMUOMBE RADHI LISSU-MBOWE
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ) , kimemtaka Rais Jakaya Kikwete amuombe radhi Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, Bw. Tundu Lissu.
Mwenyekiti wa Chama hicho Bw Freeman Mbowe, aliyasema hayao Dar es salaamjana wakati akifungua mkutano wa siku nne uliohusisha wataalamu wa chama hicho kutoka kanda zote nchini.
Alisema CHADEMA kimesikitishwa na hatua ya Rais Kikwete kumshambulia Bw. Lissu kwa maneno akidai hotuba yake ambayo aliisoma bungeni Mjini Dodoma katika bunge lililopita ilijaa uzushi,uongo,unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu.
Bw Mbowe alisema , hotuba hiyo haikuwa ya Bw Lissu bali ilitolewa na Kambi rasmi ya Upinzani bungeni....."
My Take:
Mbowe atilie maanani kuwa inaelekea amesikitishwa na jinsi ujumbe ulivyofikishwa na Mh JK, lakini hajapinga kile kilichondani ya ujumbe wenyewe.
Pili, lugha zisizo na staha zimekuwa zikivumiliwa sana na viongozi wa CHADEMA, hapa majuzi tu ni Mh. Lissu huyu huyu alisikika akisema miCCM,maCCM, leo yamempata makubwa!
Inakuwaje tena kulalama wakati mmechagua kuwa hiyo ndo staili ya kufikisha ujumbe?
Na habari yenyewe inasema
"JK AMUOMBE RADHI LISSU-MBOWE
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ) , kimemtaka Rais Jakaya Kikwete amuombe radhi Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, Bw. Tundu Lissu.
Mwenyekiti wa Chama hicho Bw Freeman Mbowe, aliyasema hayao Dar es salaamjana wakati akifungua mkutano wa siku nne uliohusisha wataalamu wa chama hicho kutoka kanda zote nchini.
Alisema CHADEMA kimesikitishwa na hatua ya Rais Kikwete kumshambulia Bw. Lissu kwa maneno akidai hotuba yake ambayo aliisoma bungeni Mjini Dodoma katika bunge lililopita ilijaa uzushi,uongo,unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu.
Bw Mbowe alisema , hotuba hiyo haikuwa ya Bw Lissu bali ilitolewa na Kambi rasmi ya Upinzani bungeni....."
My Take:
Mbowe atilie maanani kuwa inaelekea amesikitishwa na jinsi ujumbe ulivyofikishwa na Mh JK, lakini hajapinga kile kilichondani ya ujumbe wenyewe.
Pili, lugha zisizo na staha zimekuwa zikivumiliwa sana na viongozi wa CHADEMA, hapa majuzi tu ni Mh. Lissu huyu huyu alisikika akisema miCCM,maCCM, leo yamempata makubwa!
Inakuwaje tena kulalama wakati mmechagua kuwa hiyo ndo staili ya kufikisha ujumbe?