Kumbe Chadema imepoteza mtu muhimu- Professor

Kumbe Chadema imepoteza mtu muhimu- Professor

MIDFIELD

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2013
Posts
1,944
Reaction score
703
Nilikuwa naangalia BBC taarifa ya habari, mara naona Kikeke akimhoji niliyekuwa namjua km Dr Kitila Mkumbo, kumbe kesha ukwaa U-Professor. Sijui ni lini kaupata lakini ni prof tayari. ndo nikaona kumbe chadema imepoteza kichwa muhimu sana. Hongera sana Prof Mkumbo Kitila kwa hatua hiyo
 
Unaweza ukawa Professor uprofessor wako usiendane matendo yako na kufanya ukawa professor jina
 
Nilikuwa naangalia BBC taarifa ya habari, mara naona Kikeke akimhoji niliyekuwa namjua km Dr Kitila Mkumbo, kumbe kesha ukwaa U-Professor. Sijui ni lini kaupata lakini ni prof tayari. ndo nikaona kumbe chadema imepoteza kichwa muhimu sana. Hongera sana Prof Mkumbo Kitila kwa hatua hiyo
Kama ni profesa na aitendee haki fani yake na elimu yake. Kama siasa si fani aliyosomea basi kwenye uwanda huo atembee pole pole. Anaweza kuwa profesa mzuri wa kile alichosomea na kubobea lakini akawa mbaya kwenye siasa na misimamo ya kawaida katika masuala muhimu ya kijamii. Yeye si profesa wa kwanza kuingia kwenye siasa. Wapo wengi tu na walio wengi walishindwa kuonyesha tofauti kati yao na waloe ambao hawana ubavu wa kielimu kama wao. Kwa hiyo, ni suala la kutizama vema. Hatuwezi kusema CDM imepoteza mtu muhimu kwa kuwa tu amekuwa profesa, maana CDM si chuo kikuu ambapo profesa anakuwa raslimali muhimu moja kwa moja!
 
UDSM nayo inaenda kuwa chuo cha kata. SAD.
 
Kama ni profesa na aitendee haki fani yake na elimu yake. Kama siasa si fani aliyosomea basi kwenye uwanda huo atembee pole pole. Anaweza kuwa profesa mzuri wa kile alichosomea na kubobea lakini akawa mbaya kwenye siasa na misimamo ya kawaida katika masuala muhimu ya kijamii. Yeye si profesa wa kwanza kuingia kwenye siasa. Wapo wengi tu na walio wengi walishindwa kuonyesha tofauti kati yao na waloe ambao hawana ubavu wa kielimu kama wao. Kwa hiyo, ni suala la kutizama vema. Hatuwezi kusema CDM imepoteza mtu muhimu kwa kuwa tu amekuwa profesa, maana CDM si chuo kikuu ambapo profesa anakuwa raslimali muhimu moja kwa moja!

Bovidae umeiweka vizuri mno hongera
 
Last edited by a moderator:
Nilikuwa naangalia BBC taarifa ya habari, mara naona Kikeke akimhoji niliyekuwa namjua km Dr Kitila Mkumbo, kumbe kesha ukwaa U-Professor. Sijui ni lini kaupata lakini ni prof tayari. ndo nikaona kumbe chadema imepoteza kichwa muhimu sana. Hongera sana Prof Mkumbo Kitila kwa hatua hiyo

ni profesa wa vitabu lakini ubongo kashikiwa na zitto kabwe sasa kuna mtu hapo.
 
Siasa za Tanzania hazihitaji utaalamu au wasomi. Ni siasa ambazo ni za ubabaishaji, uraghai na ubabe tu. Hivyo hata kama hujaenda shule lakini uwe na kigezo mojawapo wa hivyo nilivyovitaja basi umewini kwenye siasa za Tanzania. CDM hawawezi kujutia kwa kumkosa msomi huyo maana hana sifa hizo
 
Ccm ina maprofesa zaidi ya 18 nin wanafanya?Elimu ni utendaji,Ufuatiliaji na utekelezaji,kinyume na hapo mbumbumbu kama wa chama.
 
hata JUMA KAPUYA naye ni profesa.
Nilikuwa naangalia BBC taarifa ya habari, mara naona Kikeke akimhoji niliyekuwa namjua km Dr Kitila Mkumbo, kumbe kesha ukwaa U-Professor. Sijui ni lini kaupata lakini ni prof tayari. ndo nikaona kumbe chadema imepoteza kichwa muhimu sana. Hongera sana Prof Mkumbo Kitila kwa hatua hiyo
 
asanteni wadau kwa michango yenu. jf hapaharibiki kitu
 
hata JUMA KAPUYA naye ni profesa.
Nilikuwa naangalia BBC taarifa ya habari, mara naona Kikeke akimhoji niliyekuwa namjua km Dr Kitila Mkumbo, kumbe kesha ukwaa U-Professor. Sijui ni lini kaupata lakini ni prof tayari. ndo nikaona kumbe chadema imepoteza kichwa muhimu sana. Hongera sana Prof Mkumbo Kitila kwa hatua hiyo
 
hata JUMA KAPUYA naye ni profesa.

Jumanne Maghembe nae ni professa lakini ameshindwa kuongoza wizara zote alizopewa kuziongoza na mpaka hivi sasa maji ni shida si Dar tu bali sehemu nyingi za nchi!! Taaluma na utendaji ni vitu tofauti sana.
 
Siasa za Tanzania hazihitaji utaalamu au wasomi. Ni siasa ambazo ni za ubabaishaji, uraghai na ubabe tu. Hivyo hata kama hujaenda shule lakini uwe na kigezo mojawapo wa hivyo nilivyovitaja basi umewini kwenye siasa za Tanzania. CDM hawawezi kujutia kwa kumkosa msomi huyo maana hana sifa hizo

Umenena vema mkuu, ukiwaongoza watu ambao wengi wao uwezo wao wa kuchambua mambo na kufikiri ni mdogo, hauhitaji kuwa na elimu kubwa. Kila unachowaambia wanakubali bila kuhoji. Wanaweza kuaminishwa kuirahisi kuwa video ya ugaidi imetengenezwa lakini waraka wa kumchaua fulani haujatengenezwa!

Wanaambiwa kuwa chama fulani kinajipambanua kwa kupinga ufisadi wakati Mwenyekiti wa chama hicho hicho anachukua rushwa kwa mgombea fulani ili asipige kampeni jimboni mwake apite bila kupingwa!
 
Siasa za Tanzania hazihitaji utaalamu au wasomi. Ni siasa ambazo ni za ubabaishaji, uraghai na ubabe tu. Hivyo hata kama hujaenda shule lakini uwe na kigezo mojawapo wa hivyo nilivyovitaja basi umewini kwenye siasa za Tanzania. CDM hawawezi kujutia kwa kumkosa msomi huyo maana hana sifa hizo

Ni kwli kaka, nimekubali
 
Back
Top Bottom