Elections 2015 Kulinda kura: Wakili Peter Kibatala afungua kesi Mahakama Kuu

amilyroley

JF-Expert Member
Jun 23, 2015
621
1,199
Tayari wakili jembe na nguli Peter Kibatala akiambatana na wanasheria nguli wa Ukawa Prof Safari, Mallya na Tundu Lissu asubuhi ya leo amefungua kesi mahakama kuu kuishitaki NEC kwa ukiukwaji wa sheria juu ya wananchi kukaa mita mia mbili na kulinda kura.

Kesi imefunguliwa under certificate of urgency nadhani kama sijakosea kwa kiswahili ni 'hati ya dharura' ili isikilizwe na tafsiri itoke kabla ya uchaguzi.Tayari jalada lishapelekwa kwa pilato na wanasheria nguli wa Ukawa wamejipanga kwa hoja za nguvu na ushahidi wa kutosha.

Pia jopo la wanasheria nguli wa UKAWA wameiomba mahakama kuu ya Tanzania kutoa tafsiri ya kisheria juu ya matamshi ya rais wa nchi kuwa alitumia mamlaka gani kuvaa kazi za tume.

 
kila la kheri my learned brother,I hope High Court watatoa tafsiri liberally kuhakikisha haki inapatikana
 


dah nahisi mtu anaweza kurogwa hapa manake kila mwanya wa goli la mkono ukitokeza mnaziba....dah msidhani wanafurahi?
 
Nice move,ila pia wafanye utaratibu wa kumlima Kikwete kwa wawakilishi wa nchi za Ulaya,International Observers na ICC kwa kitendo chake cha kuingilia NEC huku akipotosha idadi ya wapiga kura na kutoa vitisho vya kutumia mabavu/kuvunja amani!!!
 
kila la kheri my learned brother,I hope High Court watatoa tafsiri liberally kuhakikisha haki inapatikana

Mkuu wala liberal approach haihitajiki kwani kifungu kipo wazi kabisa kuwa kukaa mita mia mbili toka sehemu ya kupigia kura sio kosa. Ila haisemi mkiwa hapo muwe kwa ajili ya kulinda kura. Kwa hiyo watu wakae mita hizo mia mbili ila polisi wakija wasiseme tupo hapa tunalinda kura hata kama mioyoni mwao lengo ni kulinda kura.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…