Maisha pesa
JF-Expert Member
- Nov 6, 2015
- 681
- 632
Vijana wengi wanatamani kuoa na wasichana wengi wanatamani kuolewa. Mimi ni miongoni mwa vijana wanaojiandaa kuoa na hivyo niko katika kipindi cha kuyatafakari maisha ya ndoa.
Jambo moja ambalo limenishangaza ni wimbi la kuachana wanandoa. Asilimia kubwa ya marafiki na jamaa zangu walionitangulia kwenye ndoa hawako pamoja leo hii. Siyo wadada wala wakaka ukija kusikia eti walishaachana. Tena wapo waliokuwa wanapendana sana kiasi kwamba niliamini ni kifo tu kingewatenganisha lakini leo hii nasikitika kusikia wameachana.
Tatizo ni nini wakuu? Zamani watu walikuwa wanaachana lakini siyo sana kama siku hizi make ilikuwa ni aibu kuachika na baadhi ya makabila mtoto wa kike alikuwa anaambiwa akiachika asirudi tena kwao, kwa lengo la kumfanya aiheshimu ndoa yake na awe mvumilivu.
Baadhi ya watu wazima wameniambia kuna tatizo la feminism, wanawake wengi hasa wenye vipato wanapenda kushindana na wanaume hawajishushi kama wanawake wazamani ambao hata wakipigwa walikuwa wanavumilia tu.
Pia michepuko ya wanaume ni tangu zamani lakini siku hizi mwanaume akichepuka na mwanamke naye anataka kuchepuka ili alipize mwishoe ni kuachana tu.
Kingine watu wamepungukiwa na uvumilivu, juzi nimepigana sana kuokoa ndoa ya mdogo wangu ambaye alitaka kumuacha mkewe waliyezaa naye watoto wawili ili aoe kabinti ka Chuo Kikuu bila sababu zinazoeleweka lakini mwishoe nikabaini huyu amemchoka shemeji tu. Wanawake nao mwanaume akichoka mathalani hana hela tena au kaishiwa nguvu za kiume wanaanza visa mwishoe wanakimbia.
Nini sababu nyingine zinachangia? Karibu mtoe maoni tuwaandae vijana kabla hawajaingia kwenye ndoa takatifu.
Jambo moja ambalo limenishangaza ni wimbi la kuachana wanandoa. Asilimia kubwa ya marafiki na jamaa zangu walionitangulia kwenye ndoa hawako pamoja leo hii. Siyo wadada wala wakaka ukija kusikia eti walishaachana. Tena wapo waliokuwa wanapendana sana kiasi kwamba niliamini ni kifo tu kingewatenganisha lakini leo hii nasikitika kusikia wameachana.
Tatizo ni nini wakuu? Zamani watu walikuwa wanaachana lakini siyo sana kama siku hizi make ilikuwa ni aibu kuachika na baadhi ya makabila mtoto wa kike alikuwa anaambiwa akiachika asirudi tena kwao, kwa lengo la kumfanya aiheshimu ndoa yake na awe mvumilivu.
Baadhi ya watu wazima wameniambia kuna tatizo la feminism, wanawake wengi hasa wenye vipato wanapenda kushindana na wanaume hawajishushi kama wanawake wazamani ambao hata wakipigwa walikuwa wanavumilia tu.
Pia michepuko ya wanaume ni tangu zamani lakini siku hizi mwanaume akichepuka na mwanamke naye anataka kuchepuka ili alipize mwishoe ni kuachana tu.
Kingine watu wamepungukiwa na uvumilivu, juzi nimepigana sana kuokoa ndoa ya mdogo wangu ambaye alitaka kumuacha mkewe waliyezaa naye watoto wawili ili aoe kabinti ka Chuo Kikuu bila sababu zinazoeleweka lakini mwishoe nikabaini huyu amemchoka shemeji tu. Wanawake nao mwanaume akichoka mathalani hana hela tena au kaishiwa nguvu za kiume wanaanza visa mwishoe wanakimbia.
Nini sababu nyingine zinachangia? Karibu mtoe maoni tuwaandae vijana kabla hawajaingia kwenye ndoa takatifu.
