Kuletewa Balozi mtaalamu wa Ulinzi wa Masuala ya Mitandao ni 'Diplomatic Gesture' ?

Balozi nyingi zimejaa attaché wenye sifa mbalimbali, ukienda balozi za nchi kama Marekani na Uchina kuna mijasusi mingi tu. Kuna jamaa wa Marekani aliwahi kufanya kazi hapa Tanzania miaka ya nyuma, kipindi cha Obama akapelekwa Afghanistan kusimamia ile Drone-Program inayoshughulikia magaidi. Pia inasemekana hilo jamaa ndiyo lilihusika na kumshughulikia yule kamanda wa Iran, Qassem Solemani.

Hivyo nadhani ni kawaida sana balozi za nchi kubwa kuwa na wataalamu wa aina mbalimbali, tena ambao hata huwezi kufahamu Resume zao kirahisi....................
 
Mkuu you're my favorite JF member.... Mara zote huwa unakuja na facts na sources bila speculations tupu.

Unanikosha sana kwa kweli
 
Naamini Maxence atatulinda na kutusaliti kwa weledi wake na timu yake kwenye mambo ya mitandao hasa kufanya siri majina ya halisi ya wanachama wa JF ambao wanatumia majina bandia.
Sidhani kama JF ina shida, wa kule twitani ndio...
 
Hizo ni speculations tu...
Tatizo letu wabongo tumebobea kwa ramli chonganishi.
Mimi nimetoa mawazo yangu, ungetoa yako hayo mambo ya ramli yanatoka wapi mbona wenzako wamechangia vizuri tu au hujaelewa
 
Kwamba balozi atakuwa na muda wa kushughulikia wakosoaji wa watawala wa Tz mitandaoni?

I doubt it.. Kwao wakosoaji ni wengi zaidi.

Labda kama angekuwa balozi wa nchi ya kidikteta kama China, North Korea..
Balozi zinaunganisha nchi na nchi. Marehemu alivyotaka kununua Ndege alipata ushauri kwa Kagame na hili aliliweka wazi. Kabla ya kumfikia Kagame alikutana na Balozi.
 
Mkuu mngony wenzetu wapo mbali sana!
Sisi tumekariri mwafulani tumtupe wapi na kujuana kwingi pasipo kuangalia matunda ya mteuliwa ktk masrahi ya taifa.
 
Ambassador Mary O'Neill from Ireland.

Ireland ni nchi inayotoa misaada mingi ya kijamii na kiutu pia kufuatilia kwa karibu nchi zinazokumbwa na mikasa ya asili na yale yaletwayo na binadamu. Nadhani taifa hili la Jamhuri ya Ireland kutokana na kuwa linaamini sana utengamano na amani, balozi huyu mpya atafanya kazi kwa karibu na serikali hii ya awamu ya sita.

 
Na kweli mama anafungua nchi ! Yaani sasa hivi mpaka balozi anachambuliwa na raia !?.hakika kazi iendelee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…