Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Naamini umeishakutana na watu wasemao: “Mimi sipendi ndizi, sipendi dagaa, mimi sipendi parachichi, sitaki mboga fulani, sitaki kula chakula hiki wala kile, chakula changu ni chips mayai na soda.” Tabia hii ya kubagua bagua vyakula inapingana na hekima ya Mungu aliyeumba vyakula. Mungu sio mjinga; kila alichokiumba kina maana na faida katika mwili wa mwanadamu.
Maandiko yanasema:
“Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani, kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba..” (1 Timotheo 4:4-5)
Hii inatufundisha kwamba chakula chochote kilichoumbwa na Mungu kina faida. Waulize nutritionists, watakuthibitishia ukweli huo, kwamba kila aina ya chakula hubeba virutubisho maalum. Hakuna chakula kimoja peke yake kinachoweza kukupa virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini. Ndiyo maana Mungu aliumba aina nyingi za vyakula. Hivyo ukikataa baadhi ya vyakula, unakataa baraka na hekima ya Mungu aliyeumba vyakula vinavyotufaa.
Mara nyingi wanaosema: "Mimi sili mihogo, sili mchicha, sili chakula hiki au kile, utakuta wana upungufu wa virutubisho (nutrient deficiency) na hatimaye huathirika kiafya kwa kupatwa na magonjwa yatokanayo na kutokula vyakula fulani.
Ukibagua bagua vyakula, siku ukiugua na kukimbilia hospitali, usishangae daktari akikuambia utafute vyakula vile vile ulivyovikataa awali. Hata hivyo, watu wengi huambiwa hivyo wakati afya zao tayari zimeishaharibika!
Maandiko yanasema:
“Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani, kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba..” (1 Timotheo 4:4-5)
Hii inatufundisha kwamba chakula chochote kilichoumbwa na Mungu kina faida. Waulize nutritionists, watakuthibitishia ukweli huo, kwamba kila aina ya chakula hubeba virutubisho maalum. Hakuna chakula kimoja peke yake kinachoweza kukupa virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini. Ndiyo maana Mungu aliumba aina nyingi za vyakula. Hivyo ukikataa baadhi ya vyakula, unakataa baraka na hekima ya Mungu aliyeumba vyakula vinavyotufaa.
Mara nyingi wanaosema: "Mimi sili mihogo, sili mchicha, sili chakula hiki au kile, utakuta wana upungufu wa virutubisho (nutrient deficiency) na hatimaye huathirika kiafya kwa kupatwa na magonjwa yatokanayo na kutokula vyakula fulani.
Ukibagua bagua vyakula, siku ukiugua na kukimbilia hospitali, usishangae daktari akikuambia utafute vyakula vile vile ulivyovikataa awali. Hata hivyo, watu wengi huambiwa hivyo wakati afya zao tayari zimeishaharibika!