Kukojoa mara kwa mara kukiwa na baridi

E52

Member
Oct 31, 2010
81
14
wadau nina tatizo,,,siku kukiwa na baridi ninaenda haja ndogo mara kwa mara, nauliza hivi ni ugonjwa au kawaida ?
 
kawaida. mbona umetumia tu E52 O.K karibu huku mi msaidizi wa mzizi mkavu nakusanya ma file jina lako please umetoka mtaa gani i mean jukwaa gani na balozi wako nani?
 
wadau nina tatizo,,,siku kukiwa na baridi ninaenda haja ndogo mara kwa mara, nauliza hivi ni ugonjwa au kawaida ?
Pole sana inategemea upo nchi gani za baridi? mimi pia huwa inanitokea wakati wa baridi nakunywa sana chai na kwenda haja ndogo na nipo nchi za baridi hali ya hewa yake na joto pia lipo kwa wakati wake maalum. Kwani unapokwenda hiyo haja ndogo kuna maumivu yoyote yale? kama hakuna maumivu ni hali ya hewa huko uliko kwenda haja ndogo wkati wa baridi ni kawaida tu. lakini ikiwa unapata hiyo haja ndogo na unasikia maumivu itabidi umuone Daktari haraka.
 
MziziMkavu, ungesubiri the secretary amalize kuchukua maelezo na mie mhasibu kumkatia risiti. Si ataenda toilet apitilize bila kulipa?
 
MziziMkavu, ungesubiri the secretary amalize kuchukua maelezo na mie mhasibu kumkatia risiti. Si ataenda toilet apitilize bila kulipa?
Mkuu King'asti Ni kweli ningeli mngojea, The secretary amaliza kazi yake kisha ningeliingia mimi . Kukojoa kwa nchi za baridi kunatokana na hali ya hewa ya baridi kibofu chako cha mkojo kinafanya kazi

vizuri ndio maan aunakwenda sana haja ndogo ,jambo lingine pia kukojoa kila wakati kunasababishwa na mawazo ya mtu,

ukiwa mtu mwenye mawazo mengi basi kila wakati utakuwa ani mtu wa kwenda haja ndogo kila wakati . Jambo lingine pia

kwenda haja ndogo kila wakati kwa nchi za baridi kunasababishwa na wewe kunywa chai ya moto hususa chai ya rangi. Mkuu ukiwa na wasi wasi nenda kapime Hospitali kuhakikisha afya yako. Mkuu E52
 
Vile vile ujue kuwa wakati wa baridi njia moja ya kupunguza hiyo unwanted liquid waste in mkojo sababu matundu yote ya kutolea jasho huwa hayafanyi kazi. Ina maana kama hau sweat njia moja ya mkojo inatumika
 
wadau nina tatizo,,,siku kukiwa na baridi ninaenda haja ndogo mara kwa mara, nauliza hivi ni ugonjwa au kawaida ?

that's very normal hi ni kw sababu wakati wa baridi matundu ya jasho huziba na hiyo kuzuia maji ya ziada ya mwilini kutoka kwa wingi na hivyo njia pekee hubaki kuwa mkojo wa mara kwa mara.usijali hilo sio tatizo labda kama unaona vtu vinginine kwa wakati huo.cheer up buddy!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kama unajisikia kuchokachoka, njaa sana mara kwa mara, inaweza kuwa dalili ya kisukari! Jaribu kuu lamba mkojo wako kama ni mtamu! kama si mtamu basi nakubakiana na mawazo yaliyotangulia!
 
Zipo njia kuu mbili za kutoa maji maji yasiyotakiwa mwilini

1. Majimaji yasiyotakiwa hutoka kwa njia ya kawaida ya kukojoa.

2. Majimaji yasiyotakiwa mwilini hutolewa mwilini kama jasho, kipindi cha baridi matundu matundu ya ngozi hufunga hivyo kulazimisha majimaji yote yatoke kwa njia ya kukojoa.

Huna tatizo lolote la kiafya, huo ni taratibu za kawaida kukojoa sana ukiwa maeneo yenye baridi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom