Kuishi na walimwengu yataka moyo

Kuishi na walimwengu yataka moyo

Hii kesi ni yangu kabisa na jirani yangu mtu mzima bandidu balaa.
Nataka kujenga fensi nikamfuata, nikamwambia bwana fensi tuziunge sababu ya kiusalama, akakataa akasema tuache mita moja na nusu pawe na uchochoro.
Mie kiroho safi nikatia fensi nzito ya tofali za block nikaacha mita moja na nusu, si nae akapata hela akaanza ujenzi wa fensi kuvuta kutoka kwenye fensi yangu, yani achukue na ile moja moja na nusu ya kwangu, nikamfuata sikumkuta, nikaacha maagizo kwa mke wake kwamba kama anataka kujenga fensi aache mita moja na nusu kama ambavyo alishauri vinginevyo hatojenga hiyo fensi.

Basi ukawa mwisho wa salamu na mimi nikakauka mpaka leo na fensi ile nikaongeza kozi mbili nikatia na security wire. Anabakiaga kusema huyo dogo anakula sana kaya kwa watu. 😁
 
Pole sana,
Unapakana na mwenzio kiwanja wewe unatangulia kujenga,wakati yeye anajenga vifaa anaweka kwako Hadi mchanga wako anatumia na harudishi mwisho wa siku anamaliza kujenga na kuhamia,mwisho wa siku anasema eti hupendi maendeleo yake!

Unapotezea tu!
Naona sasa jirani umefungua I'd na kuja kujibu mashtaka
 
Jirani yangu alizidisha mpaka akaingia kwenye eneo langu, ni kweli eneo lake ni dogo inaweza kuwa nusu ya eneo langu,
baada ya kuvuka mpaka ikabidi nimfuate kwa nia nzuri tu nikijua labda ni bahati mbaya,

Huwezi amini moto uliwaka maneno kibao, kwamba nawafatilia sana, ikabidi niondoke zangu baada ya kuona tunapoelekea siyo kuzuri,

Baada ya wiki kadhaa nikazungusha uzio ili kuepuka shari, huwezi amini jirani hataki hata kunisalimia, yani ni kimya kimya, sasa hapo sijui kosa langu ni lipi,

Hapo kabla niliwachukulia kama watu wema sana, walinitia moyo wakaniambia nisijali ipo siku nami ntajenga kama wao, lakini cha ajabu baada ya kuhamia kwangu jirani amekuwa tofauti sana, kila siku visa tu,

kweli ubinadamu kazi.
Siamini katika kujenga urafiki na jirani.
 
Haujui kosa lako? Ni wewe kuwazidi wao, mambo lazima yaharibike tu. Nina jirani yangu anaendesha boda, amejikuta akiuza pikipiki yake kisa namzidi vitu vya ndani. Shinikizo kubwa limetoka kwa mkewe.
Hatari sana
 
Jirani yangu alizidisha mpaka akaingia kwenye eneo langu, ni kweli eneo lake ni dogo inaweza kuwa nusu ya eneo langu,
baada ya kuvuka mpaka ikabidi nimfuate kwa nia nzuri tu nikijua labda ni bahati mbaya,

Huwezi amini moto uliwaka maneno kibao, kwamba nawafatilia sana, ikabidi niondoke zangu baada ya kuona tunapoelekea siyo kuzuri,

Baada ya wiki kadhaa nikazungusha uzio ili kuepuka shari, huwezi amini jirani hataki hata kunisalimia, yani ni kimya kimya, sasa hapo sijui kosa langu ni lipi,

Hapo kabla niliwachukulia kama watu wema sana, walinitia moyo wakaniambia nisijali ipo siku nami ntajenga kama wao, lakini cha ajabu baada ya kuhamia kwangu jirani amekuwa tofauti sana, kila siku visa tu,

kweli ubinadamu kazi.
Sijuhi huwaga wanashida gan me naona kabla ya kujenga Bora uzungushe kwanza ukuta
 
Back
Top Bottom