Oscar Lyrics
JF-Expert Member
- Oct 8, 2022
- 2,744
- 4,672
Jirani yangu alizidisha mpaka akaingia kwenye eneo langu, ni kweli eneo lake ni dogo inaweza kuwa nusu ya eneo langu,
baada ya kuvuka mpaka ikabidi nimfuate kwa nia nzuri tu nikijua labda ni bahati mbaya,
Huwezi amini moto uliwaka maneno kibao, kwamba nawafatilia sana, ikabidi niondoke zangu baada ya kuona tunapoelekea siyo kuzuri,
Baada ya wiki kadhaa nikazungusha uzio ili kuepuka shari, huwezi amini jirani hataki hata kunisalimia, yani ni kimya kimya, sasa hapo sijui kosa langu ni lipi,
Hapo kabla niliwachukulia kama watu wema sana, walinitia moyo wakaniambia nisijali ipo siku nami ntajenga kama wao, lakini cha ajabu baada ya kuhamia kwangu jirani amekuwa tofauti sana, kila siku visa tu,
kweli ubinadamu kazi.
baada ya kuvuka mpaka ikabidi nimfuate kwa nia nzuri tu nikijua labda ni bahati mbaya,
Huwezi amini moto uliwaka maneno kibao, kwamba nawafatilia sana, ikabidi niondoke zangu baada ya kuona tunapoelekea siyo kuzuri,
Baada ya wiki kadhaa nikazungusha uzio ili kuepuka shari, huwezi amini jirani hataki hata kunisalimia, yani ni kimya kimya, sasa hapo sijui kosa langu ni lipi,
Hapo kabla niliwachukulia kama watu wema sana, walinitia moyo wakaniambia nisijali ipo siku nami ntajenga kama wao, lakini cha ajabu baada ya kuhamia kwangu jirani amekuwa tofauti sana, kila siku visa tu,
kweli ubinadamu kazi.