Kuishi Afrika na Tanzania bila kumuamini Mungu au ukiwa atheist ni jambo gumu sana

Kuishi Afrika na Tanzania bila kumuamini Mungu au ukiwa atheist ni jambo gumu sana

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
57,241
Reaction score
90,299
Sijui kwa nini watu wasio na hofu ya mungu wanaoenkana watu wabaya sana ukizingatia watu waliofanya na wanaofanya maovu makubwa katika jamii ni wenye dini na inayoitwa hofu ya mungu. Nafikiri mojawapo ya scam kubwa kuwahi kutokea duniani ni imani ya kwamba watu wenye hofu ya mungu ni wema sana na wasio nayo na waovu wakuu.
Screenshot_20250706_100145_X.jpg
 
Wengi wanaotoa kauli kama hizo ukijaribu kufanya tathmini utagundua wamesoma Bible kwa kukariri.

Kusoma Biblia ndio kitu pekee kinakufanya uwe mkristo

Lakini kuielewa Biblia ndio sababu itayokufanya uwe Atheist.
 
Wengi wanaotoa kauli kama hizo ukijaribu kufanya tathmini utagundua wamesoma Bible kwa kukariri.

Kusoma Biblia ndio kitu pekee kinakufanya uwe mkristo

Lakini kuielewa Biblia ndio sababu itayokufanya uwe Atheist.
Kuwa atheist ni uchaguzi tu kama ambavyo wengine wanaoielewa biblia kisha wanachagua kufuata dini nyengine au kuacha kufuata dini na kuwa wanaamini Mungu bila dini.
 
Wengi wanaotoa kauli kama hizo ukijaribu kufanya tathmini utagundua wamesoma Bible kwa kukariri.

Kusoma Biblia ndio kitu pekee kinakufanya uwe mkristo

Lakini kuielewa Biblia ndio sababu itayokufanya uwe Atheist.
Nakazia.
 
Miongoni mwa wanao amini uwepo wa Mungu.
Watu wenye hofu ya Mungu ni wachache sana.

Ndio maana "Wanyonya Damu" ni wengi.
 
Kuwa atheist ni uchaguzi tu kama ambavyo wengine wanaoielewa biblia kisha wanachagua kufuata dini nyengine au kuacha kufuata dini na kuwa wanaamini Mungu bila dini.
Katika ulimwengu wenye multi-options ya beliefs ni wazi katika mazingira hayo mtu kuwa Atheist inaweza kuonekana kama ni uchaguzi binafsi wa mtu kuamua kuufuata au kuukacha, but somehow inaweza kuwa na double meaning.

Ukirejea historia Atheism inaweza kutazamwa kama default au ndio msingi wa mwanzo kabisa ku exist kabla ya ujio wa imani. Hivyo katika hizo nyakati ambazo hakukuwa na imani za dini, huo uchaguzi haukuwezekanika kwasababu choices ilikuwa fixed eneo moja.

Na kwa hiyo unaweza kuwa logically kusema Atheist ndio muanzilishi wa hizi dini.
 
Tanzania hakuna wachaMungu Ila kuna watu wa dini .

So atheists na mwamposa ni kitu kimoja wote hawajui wanachosimamia

Watu wa dini na atheists ni kitu kimoja , wote wabishi , hawajui nini wanasimamia


MTU anayemuamini Mungu bila kuhusisha dini hauwezi kumkuta anabishana
 
Ni swali ambalo najiulizaga mara kwa mara sipati jibu... Ni sawa na ile wanasema ni lazima kila mtu awe na mtoto wakati ukiutazama ulimwengu kwa akili timamu unagundua kuwa na mtoto ni sawa ujikute gerezani alafu umlete mpendwa wako hukohuko gerezani alafu ujisifu.
 
Sijui kwa nini watu wasio na hofu ya mungu wanaoenkana watu wabaya sana
Mimi huyu kiongozi alinifungua macho kupitia hii nukuu yake:

"Religion is excellent stuff for keeping common people quiet. Religion is what keeps the poor from murdering the rich."

— Napoleon Bonaparte

Ukitumia akili yako vizuri, dini ni moja wapo ya aina za propaganda.

propaganda

habari zilizotiwa chumvi sana au za uongo zitolewazo kwa lengo la kushawishi watu kuamini au kukubali jambo fulani

 
Wengi wanaotoa kauli kama hizo ukijaribu kufanya tathmini utagundua wamesoma Bible kwa kukariri.

Kusoma Biblia ndio kitu pekee kinakufanya uwe mkristo

Lakini kuielewa Biblia ndio sababu itayokufanya uwe Atheist.
Mama asemewe, yeye kasoma Quran pekee. Kitabu kisicho na shaka ndani yake sio Biblia.
 
Katika ulimwengu wenye multi-options ya beliefs ni wazi katika mazingira hayo mtu kuwa Atheist inaweza kuonekana kama ni uchaguzi binafsi wa mtu kuamua kuufuata au kuukacha, but somehow inaweza kuwa na double meaning.

Ukirejea historia Atheism inaweza kutazamwa kama default au ndio msingi wa mwanzo kabisa ku exist kabla ya ujio wa imani. Hivyo katika hizo nyakati ambazo hakukuwa na imani za dini, huo uchaguzi haukuwezekanika kwasababu choices ilikuwa fixed eneo moja.

Na kwa hiyo unaweza kuwa logically kusema Atheist ndio muanzilishi wa hizi dini.
Imani ni pana hivyo si suala la kuhususiana na dini au Mungu tu, kwahiyo hata atheist yapo mambo anaamini(sio lazima iwe dini au Mungu) sidhani kama kwenye haya maisha kuna mtu haamini chochote hilo haliwezekani. Sasa kutokuamini au kutokuwa na imani ya kitu/jambo fulani huwa kuna sababu zake maana hata watu wa dini kuna mambo hawaamini kwa kutovijua au kwa kupinga.
 
Tofauti ni ipi?
Kuamini Mungu ni kutambua au kukubali uwepo wa Mungu tu ila kuwa na hofu ya Mungu ni kutofanya matendo maovu kwa kuhofu ya kwamba ni mambo yenye kumchukiza Mungu.

Ndio maana wenye kuamini Mungu wapo ambao ni majambazi,wauwaji n.k na wanajua kuwa hayo ni matendo maovu na ambayo yamekatazwa na Mungu ila wamekosa ile hofu ya Mungu.
 
Tanzania hakuna wachaMungu Ila kuna watu wa dini .

So atheists na mwamposa ni kitu kimoja wote hawajui wanachosimamia

Watu wa dini na atheists ni kitu kimoja , wote wabishi , hawajui nini wanasimamia


MTU anayemuamini Mungu bila kuhusisha dini hauwezi kumkuta anabishana
Mkuu mbona hao watu wapo hata humu wenye kuamini Mungu bila dini, tunabishana nao na ni watu ambao hushambulia sana dini kuliko hata atheism. Na ilivyo ni kwamba atheists na hao wenye kuamini Mungu bila kuhusisha dini huwa wanaona usahihi katika misimamo yao ni kukosoa dini.
 
wazazi wanajua mimi ni mfia dini mzuri kabisa kumbe nilishaachana na huo mtumwa kitambo sana
1751170395142.jpg
 
Back
Top Bottom