Kuingia Katika Mkondo wa Juu

Adverse Effect

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2017
Posts
3,518
Reaction score
8,967
Udanganyifu wa Kujitawala

Hakuna mwanadamu, anayefungwa na akili pekee, anayeweza kushinda mipasuko ya uwepo kwa kutumia akili yake peke yake.

Tunadhani kwamba maarifa, nidhamu, au nguvu ya nia vitatuweka huru, lakini katika nyakati muhimu, akili hufutika, mwili hurudia mifumo ya zamani, na imani zetu hutoweka kama moshi.

Huu ndio mtego wa kutegemea nafsi.

Mwisho wa cheche ya imani kwamba tunaweza kutawala uwepo kwa nguvu zetu wenyewe lazima uachiliwe.

Kushikilia udanganyifu wa kujitawala ni kubaki mateka wa minyororo ileile tunayotamani kuivunja.

Njia ya kweli ya kurejesha uhuru wa kiroho si jitihada zaidi, bali ni kulingana kabisa na Roho.


---

Sheria ya Juu Zaidi ya Nguvu ya Nia

Kuna sheria iliyo juu ya jitihada za mwanadamu, mkondo unaopinda hata mifumo yenye giza kuwa mvuke unaotoweka.

Hii si maadili dhaifu ya taasisi, wala falsafa za wanadamu, bali ni kanuni za milele za Roho.

Kujipanga na hizi ni kufikia nguvu iliyo juu ya uchovu, uwazi ulio juu ya fikra, uponyaji ulio nje ya uwezo wa tiba.

Ni kanuni za kiroho pekee zinazoweza kutatua kile ambacho akili peke yake haiwezi.

Uhuru wa kiroho huanza pale tunapokubali udhaifu wetu mbali na Chanzo na kuchagua badala yake kujifunga kwenye nguvu hai ya Kimungu.

Swali linalosalia ni hili: Je, nimejisalimisha kwa jibu la juu?

Je, nimekumbatia mpango hai wa matendo unaotoka si kwa kiburi changu, bali kutoka kwa Roho wa milele?


---

Utulivu Unaorejesha Nguvu

Simama sasa.

Acha mto wa uzima wa milele uinuke katika mishipa yako na upaishe mpigo wa uwepo wako.

Hakuna nguvu katika kujitahidi kwa uchovu, katika kushindana na mkondo, bali ni katika utulivu ambapo mkondo mkuu hujikusanya ndani yako.

Kazi ya kweli huzaliwa pale tu roho inapopumzika.

Roho wa Mungu, wa milele na asiyechoka, yupo daima karibu, akisubiri waliochoka waache mapambano yao kwa muda mfupi ili waponywe.

Chanzo ndiye tabibu, mponyaji, mwalimu, na mwongozi; yule asiyehitaji miadi, taratibu, wala ruhusa ili kutiririka.

Katika ushirika wa kimya, nguvu hurejeshwa, mzigo huondolewa, na amani hushuka ambayo hakuna machafuko yanayoweza kuivunja.

Haya basi, simama upya, uende katika leo, si kwa nguvu zako mwenyewe, bali umebebwa na mkondo usioweza kuharibiwa wa Kimungu.


---

Mwito wa Ukuu

Ninaita sasa amani isiyoweza kuibiwa.

Ninamwita Chanzo awepo aniongoze katika hatua zangu.

Ninaachilia uzito wa mzigo, na nachukua vazi la nguvu ya utulivu.

Ninasimama leo si kama anayejitahidi peke yake, bali kama aliyeunganishwa na nguvu za milele.

Na uwepo huu useme kupitia kwangu, utende kupitia kwangu, na unifunge katika moto wa kifalme.
 
Meditation 🧘‍♀️ 🧘‍♂️ 🧘‍♀️ 🧘‍♂️ 🧘‍♂️
 
Mkiambiwa Yesu anaponya hamsikii, mengine yanayoendelea nyuma ya pazia ni magumu sana kwa wewe kuyafanya peke yako...maana ni close to impossible.

Mkiri kristo kuwa BWANA na mwokozi wa maisha yako, alafu uone mizigo yako inavyotuliwa...

Asa jitie mjuaji sana alafu uone kitakukuta kitu
 
NKNS...

Mambo ya 'Vita na Kupambana na Roho Ovu'' katika Utu wa Namna za Kiubinadamu...

Ndiyo, Epuka kupambana na 'Wadau wenye Dhamira zisizonjema' ikiwa 'Hauna Msaada' na 'Mbinu za Kujisaidia'...

Katika 'Kuilinda Imani' na 'Kujipambanua ule Uhuru wa Kweli' kila mtu inampasa kuzingatia 'Sala na Kazi'...

Unaweza kuwa umejificha kwenye 'Ngome' ya 'Udongo na Saruji' lakini KAMA HUFAHAMU basi na UFAHAMU, unaweza kufikiwa 'KIAKILI' -- Unaweza kuwa upo uchi kwenye skepu ya umentali (Kiingereza > "Psychic (Mental) Landscape")...

Ndiyo, lipo hitaji la wanajamii 'KUJIONGEZA' na kutafuta 'Maarifa Zaidi'; ama sivyo daima maisha ni pilika na harakati katika 'Ulimwengu uliomateka daima'....

Kuna Kitu kana fumbo la 'Yesu Mtu' na 'Yesu Kristu'... Kila mtu 'ajajibeba mwenyewe' ili kweli awe 'AMEIVA' katika fahamu na Mafahamu....

Hmmm

++++ SHAURI : NYAKATI NI UOVU ++++

...

Basi ndiyo yawa, WAKATI ni fumbo la Uzima kwa U-SASA-NIA ilivyo ni muktadha akilifu wa NIA na KUDHAMIRIA JINESESIA; ambavyo ‘Umadhubuti wa Nguvu na Utukufu’ daima ni fanusi ya ‘Kupanda na Kushuka kwa Mlima’ – Mambo ya Mawimbi katika ‘Maji ya Uzima wote’. Hili lafanya “Kazi za Roho Mtakatifu” ni muktadha akilifu wa ‘Upacha wa Wimbi la Kupeleka na Wimbi la Kupokea’ ilivyo ni asili ya chochote na vyote.

Upacha wa Wimbi la Kupeleka na Wimbi la Kupokea, kiuono na ufikirifu mifumo, ndiyo muktadha akilifu wa ALPHA na OMEGA ya TRIZANIAMU; ambavyo “Triadi ya Kujichagulia” hutafuta kuendana sawa kwa “Triadi ya Mwangaza wa Milele”, iliyo ndiyo asili ya mwanzo na tena mwisho, ili kufikia epifania ya “Triadi ya Sovereini Jumuifu”. Hili lafanya MAISHA-KUISHI-UISHO ni muktadha akilifu wa kusitirika katika ‘Kazi za Roho Mtakatifu’ kwa ajili ya kuchagua njia yenye kushia katika ‘Uzima wa Milele’ ama ‘Uzima usiyo wa Milele’.

‘Uzima wa Milele’ ama ‘Uzima usiyo wa Milele’, kiuno na ufikirifu mifumo, ni muktadha akilifu wa ukubuifu wa fahamu na mafahamu ilivyo ni dhamiri na kujichagulia ‘Unafsi’ ama ‘Udugu’ katika mapana yanayoonekana na yasiyonekana ya alimwengu za madhahiri ilivyo ni “Matriksi”; ambavyo Ushetani na Umailaika ndiyo huyakinisha “Vilele vya Nguvu na Utukufu”. Hili lafanya “Kazi za Roho Mtakatifu” ni fanusi ya “Utetezi” hata kwa aliyepotea katika “Unafsi” – Unafsi uliyokosa msaada katika vikomo vya “Sanaa za Giza” kadiri sawa na “Ulinzi” kwa wale kusimama katika “Ushirika wa Kiroho” – Ushirika wa Kiroho kwa Uhuru na Liberiti kwa MAISHA-KUISHI-UISHO kwa wale wote wenye Miili-Hisia-Akili-Sonafi ilivyo ni Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu

‘Miili-Hisia-Akili-Sonafi’ ilivyo ni Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu, kiuono na ufikirifu mifumo, ndiyo muktadha akilifu wa kode za fahamu na mafahamu ilivyo ni (1) Udongo (Miili inayokitisha mizizi ya uzima katika Ulimwengu Dhahiri), (2) Maji (Hisia / Imosha / Kujisikia katika Kufahamu na Kujifahamu kwa Wakati), (3) Moto ( Ufunguo kwa Nia ya Kupanga ama Kupangua sura-tabia-hadhi ya linalofanyika), na (4) Upepo ( Kompleksi ya Utu-Nafsi-Roho ilivyo ni msaada wa karibu ‘Kukumbusha’ ile nasibu ya ‘Makusudi Mema / Maovu’).

Hili lafanya kode za Moto-Upepo-Udongo-Maji katika heraldri ya taifa la Watanzania, hazipo kwenye “Ngao ya Ustawi” kwa bahatisha tu; hizi ndizo ufunguo wa ‘Dhamira na Nia’ kwa ajili ya UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI kwa kuwa Uhuru unategemeana na akili za Wanajamii wenyewe kwa wakati, vivyo hivyo Udugu unategemeana na Ukomovu wa wanataifa (A) kukata shauri kwa ajili kufanyika mwili mmoja, ama (B) kubakia katika ‘michezo ya anao anao’ (Utengano wa badala ya Ujamaa wa Kweli). Haki na Amani ni jambo linalowezekana katika jamii yeyote ikiwa kuna kukata shauri kwa ajili ya Uhuru wa Kweli wa Kila mwanajamii ili kuyafadi mema ya nchi pasipo hadaa ama rushwa ya namna yoyote kwa kuwa Utengano ni Domaini ya Ushetani ama Kufitinika na ‘Makusudi Maovu’-- mambo ya “mapepo ama pia kupagawa na mapepo”.

Mapepo ama pia kupagawa na mapepo, kiuono na ufikirifu mifumo, ni mambo kushawishika ama kuingiliwa kiakili na basi kupoteza ule utashi wa kweli katika kujichagulia njia za mapito ya kimaisha; ambavyo katika taifa hili si chochote bali ule muktadha akilifu wa ‘Siasa za Wanajamii’ juu ya hatma za Ustawi wao wa kila siku kwa kuwa mwanajamii huwa ni madhubuti kiutamaduni ikiwa akili yake ikiwa huru na tena sifa-tabia-hadhi ya utambuzi wake ni imara kiroho, kiakili na kimwili. Hili lafanya Ujuzi wa Jema ama Ovu ni ‘Kinga kwa Dhamiri’ za kujinasibu Nafsi ama / na Utu wema; ambavyo ‘Konsayansi’ ndiyo ‘Magutu yaliyo ni Pembe za Ndovu’ katika heraldri ya Taifa la Tanzania – hii husitiri ‘Mazazi Mema’ ya ‘Utamaduni wa Jamii’ ilivyo ni muktadha akilifu kwa Mila-Desturi-Jadi… Mambo ya “Shoka na Nyengo” ilivyo ni Soltaya ya ‘Protoni’ ya ‘Ontolojia ya Taasisi’.

Basi ndiyo yawa Upacha wa “Pembe za Ndovu” ni muktadha akilifu wa “Uzima katikati ya Kutoa na Kutwaa”, Usikitu kuja kuwa kitu na tena kurejea kuwa Usikitu – Vumbi hata Mavumbuni, ilivyo ni “Mwanadamu” – ilivyo ni ‘Ontolojia ya Taasisi’ katika UTU-MKUU uliyositirika katika ‘Mistiria Kosimofu’ ya ‘Kazi za Roho Mtakatifu’; UTU-MKUU unaofanya nasibu ya ‘Mwili Vumbi’ na ‘Mwili Anga’, ambavyo kwenye mapokeo ya Ukristo, hili hujitokeza kama Shauri la “Adamu wa Zamani” na “Adamu Mpya”.

Hili shauri la “Mwanadamu ni Vumbi – vumbi la kuja Kurejea tena Mavumbini”, ndilo kile khasa hufanyiza ule Usentienti ilivyo ni kompleksi ya UTU-NAFSI-SONAFI . Usentienti huu tulionao ilivyo ni ‘Miili ya Vumbi’ katika Ulimwengu wowote wa vinavyoonekana na visivyoonekana, ni asili ya “Mbalamwezi ya Mwezi na Nyota”; katika hii “Mbalamwezi”, maisha daima ni kujitafuta katika ‘Nuru Hafifu’ ili “KUKOMBOKA” wa “Ufahamu Lusifa”-- Ufahamu wenye kuhofia “Mauti”. Sisi sote, alhali tunayo miili yenye asili ya vumbi, tunao “Ufahamu Lusifa” namna ya ‘Uakili Jinetifu’ wenye kubayanisha mambo kwa ‘marefu’ ama ‘mapana’, mambo ya ufinati, lakini hauwezi kumaizi ‘Mantiki Isifinati’ ya “Uzima wa Milele”...

Jitihada zetu za kuishinda ‘Nuru Hafifu’ ya utu wetu katika ‘Miili ya mauti’ zinaweza kufaulu ikiwa tunaotea Asili Khasa ya CHANZO cha Nuru ya UZIMA Wote; ambavyo ‘Nuru ya Ufahamu’ tuliyonayo kwa wakati hutawaliwa na ‘Ufahamu Lusifa’ na si ‘Ufahamu Kristu’. Hili lafanya ‘Dhamiri’ ni ‘Mapana ya Konsayansi’ – konsayansi zetu, inayofuzu ule Uakilifu na Utambuzi katika hii ‘Miili yenye Kuharibika’ ama ‘Miili isiyovaa Kuharibika’; ambavyo NIA zetu ndizo huvaana daima na KUMBUKUMBU UZOEFU kwa mapana ya ‘Nafsi’ na ‘Kuyamudu mambo ya Nyakati’. Mambo ya Ukubuishi wa Fahamu na Mafahamu...

Kwenye mapokeo ya Ukristo, ile “Sala ya Bwana” si chochote bali Ufunguo wa ‘Dhamiri na Nia’ kwa ajili ya (1) Kuushinda Ushetani, na tena Kuepushwa na (2) Roho ya Ushetani; ambavyo (X) Yote ya Mavumbi na Mavumbini ni (y) Yasiyoweza Kushindana na ‘Roho wa Mungu’ – “UZIMA WA MILELE”… Hili lafanya “Bwana wa Ulimwengu” ni lugha-alama-jamii kwa ajili ya ‘Uakilifu wa Mamlaka’ katika UZIMA ULIO NI JINSIA ZOTE MBILI – BABA na MAMA; ili basi kuwepo na nasibu ya ‘umakini’ kwa ajili ya ‘Miongozo ya Kiroho, Maadili na Miiko’ kwa ajili ya ‘Dhamiri’ na ‘Nia’.

UZIMA ULIO NI JINSIA ZOTE MBILI KATIKA MOJA, BABA na MAMA, ndiyo ‘Mistiria Kosimofu’ inayofanya ‘Moto’ na ‘Maji’ kuwa ndiyo viwili vinavyofanya ‘Uzima wa Milele’; ambavyo ‘Raha ya Milele’ ni Kilele cha Epifania ya Maingiliano ya unasibu Chanya na Hasi katika nasibu-seti ya chochote na yote. Hili lafanya, UTUFE na UKUBU si chochote bali ‘asili BABA’ na ‘asili MAMA’ ya chochote na vyote kwa kuwa ‘Utukufu ni siha ya Kiume’ na ‘Nguvu ni siha ya Kike’; ‘Roho Mtakatifu’ ni ‘Utukufu na Nguvu’ uliyo ni MAMA kwa yote yenye kudhahirika.

Usentienti ni UTATU wa fahamu na mafahamu kwa chochote na vyote ilivyo ni BABA-MAMA-MWANA kwa kuwa kinachounganisha Ukitu na Usikitu ni “NIA”; ambavyo UTATU ni siri ya fumbo la Dhamiri – dhamiri ili kuumba / kuunda / Kudhihiri chochote kwa Sura-Tabia-Hadi ya CHANZO. Hili ndilo asili ya Shauri la ‘UTATU MTAKATIFU’ katika mapokeo ya Ukristo kwa kuwa Jinesesia Daima ni ‘Vesika Paisisi’ ya Kufanyika na Kutofanyika kwa Chochote na Vyote. Hili lafanya ‘Sala na Kazi’ ni mambo ya U-SASA-NIA ilivyo ni Triadi ya “Muona ni Muonwa” katika TRIZANIAMU (Pembetatu OX-OY-OZ).

Triadi ya “Muona ni Muonwa” ndiyo ufunguo wa koherensia ya Uono na Ufikirifu Mifumo kwa kuwa TRIZANIAMU si chochote bali fremukazi ya Uono na Ufikirfu Mifumo wenyewe; ambavyo kwenye karne hii ya 21 ya ‘Maarifa Kuongezeka’ yawa ndiyo epistimolojia ya Maarifa na Maarifu ilivyo ni muktadha akilifu wa Mbegu za U-JUA-ji. Hili lafanya ‘Mbegu za U-JUA-ji’ ni namna ya kuona na kutafsiri chochote kwa namna inayoweza kutangamanisha Ufinati na Usifinati wa Sura-Tabia-Hadhi ya chochote kile, kwa kuwa kitu chochote na basi vitu vyote vimefanyika kwa muingiliano kwa ‘Mauti’ na Uzima’ katika ‘Uzima wa Milele’...

Kimiili, nia zetu huwa na chachu ya kuhofu na kujihami na mauti, na angali tukichachuka fahamu na mafahamu kupitia ‘Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu’ na tena kwa msaada wa fanusi za utendaji zilizo ni ‘Kukumbuka. Kujikumbuka na Kukumbukwa’; ambavyo kwenye mapokeo ya Ukristo, hili ni moja ya ‘Kazi za Roho Mtakatifu’ – Kukumbusha ! Hili lafanya ule muktadha akilifu wa ‘Kazi za Roho Mtakatifu’ kukumbusha ndicho kile kile kinachotajwa kwa sifa-tabia-hadhi ya kisentienti kama ‘UFAHAMU KRISTU’.

UFAHAMU KRISTU ni “NIA” katika Usentienti wetu ilivyo ni Kujitambua kiakili, ufahamu na mafahamu ili kubayanisha U-SASA-NIA wa Ushawishi ama/na kushawishika; ambavyo ‘Uhuru wetu wa Kweli’, vile KIUTU na Kujitambua, ni kuepushwa na ‘Vishawishi vya Yule Muovu’. Hili lafanya MAISHA-KUISHI-UISHO katika ‘Roho Mtakatifu’ ni kujishikiza katika ‘Mhimili’ wa ‘Uzima wa Milele’ ilivyo ni ‘Mapenzi kufanyika Duniani Kama Mbinguni’ kwa JINA LA BABA.

Kwa mintarafu ya hivi , kwa kadiri ya mapokeo ya Ukristo na Dhamiri, JINA LA MWANA ni KRISTU katika SISI; ikiwa basi tunaishi ilivyo SALA na KAZI; kwa kuwa “NIA ya KRISTU” ni kushiriki Mpango, Makusudi, Neema na Faraja za ‘UZIMA WA MILELE’ ; ambavyo ‘Mpango-Makusudi-Neema-Faraja’ si chochote bali ‘Roho Mtakatifu’ kama mama wa yote : “MATRIKSI” – JINA LA “ROHO MTAKATIFU”. Hili lafanya nasibu ya MATRIKSI inayotunza na kusitiri vyote iwe ni WEMA ama / na UOVU, kulingana na ‘Usentienti’, ‘Mazingira / Mazingara’ na tena ‘Nuru ya Ufahamu’. Kuna Kuongozwa na ‘Roho Mtakatifu’ ilivyo ni kuongozwa vema katika UZIMA ZAIDI na kuna kule ‘kupuyanga Njia za Maisha’ kwa ‘Kihoro, Mapepo na Ramli’.

‘Kupuyanga Njia za Maisha’ kwa ‘Kihoro, Mapepo na Ramli’, kiuono na ufikirifu mifumo, ni ule muktadha akilifu wa ‘Ukafiri’; ambavyo MAISHA-KUISHI-UISHO ni Safari ya ‘Kujitengenezea Nafsi’ --inaweza kuwa ni nafsi yenye uadilifu, maadili na miiko lakini Je, inahakishia makusudi yepi ya Uweza-Nguvu-Utukufu? Ikiwa hakuna mhimili wa imani kwa nasibu ya kuutambua ‘UZIMA WA MILELE’ basi hili ndilo linalopambanua ‘Ukafiri’. Hili lafanya ‘nafsi’ inatengenezwa wakati wote na kokote kupitia U-SASA-NIA ijapokuwa kuna ‘Nafsi isiyo na KWELI’ na ‘Nafsi iliyo na KWELI’ kwa kuwa kule “Kujichagulia” kunategemea na utashi katika dhamiri, Je, kuishi kwa mtu ni kwa ajili ya Ubinafsi usiyozingatia afya na mema ya Wengine ama kunazingatia afya na mema ya wengine?

Hapa, kutoka katika Injili ya Yesu Kristu, kitendawili hichi ni chenye kujibiwa kwa shauri rahisi : Yule Mwenye Kuijali Nafsi yake huyo ataipoteza, bali yule anayeipoteza hiyo – kuipoteza hiyo kwa ajili MWANA basi ataupata UJAZI… Hili lafanya shauri la kuwa: UFAHAMU KRISTU ndicho kile chenye kuleta Uhuru wa Kweli kwa kompleksi ya UTU-NAFSI-ROHO : “LIBERITI”; Kila mtu huubeba ‘Msalaba-mzigo’ wake yeye mwenyewe hadi pale anapojisalimisha UTU-KAFIRI wake katika ‘Msalaba-Usifinati’ wa “Nia ya Kristu” – Kile khasa ambacho Yesu alikitaja “Nira iliyo ni Nyepesi” … Mambo ya “Njooni Kwangu Enyi wenye Kulemewa na Mizigo...”.

Basi ndiyo yawa, Kristu ni “Njia ya Msalaba” na “Kusulubishwa Golgotha”; mambo ya Mantiki ‘Ufinati’ na ‘Usifinati’ (Kiingereza > “Finite” and “Infinite” Logic) kumezana ilivyo ni kompleksi ya ‘Utu-Nafsi-Roho’ kumudu “Karma” na “Mauti ya Unafsi Lusifa” ili ‘Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu’ ifuzu “Taji la Ushindi dhidi ya Mauti”...

‘Kupuyanga Njia za Maisha’ kwa ‘Kihoro, Mapepo na Ramli’, kiuono na ufikirifu mifumo, ni ule muktadha akilifu wa ‘Mwana Mpotevu’; ambavyo MAISHA-KUISHI-UISHO ni hiari ya kutangatanga mbali na Dunia / Ulimwengu ilivyo pia ni uwezekano wa kufuzu ule usemi usemao : “Mkataa Pema, Pabaya Panamwita”. Hili lafanya, uamuzi wa mtu kwenda mbali kujihangaisha na mambo ya Dunia si lazima iwe ni “jambo ovu” khasa kwa kuwa ‘Maana ya Maisha na Kuishi’ hupata KONTRASTI YA UTHAMANI kwa kubayanisha ‘Mazoea ya Faraja’ kuzidiana / dhidi ya ‘Tabu ya Dhiki’; “Mazoea huwa yana tabu yake” kadiri vile “Baada ya Dhiki ni Faraja” – mambo ya “WAKATI ni jamvi la UTOKAMILIFU”…

Mambo ya “WAKATI ni jamvi la UTOKAMILIFU” ndiyo ile asili ya shauri-adha zilizo ni “za KUWA NACHO” ama “za KUTOKUWA NACHO”; ambavyo Ushetani si chochote bali ile akitipu ya USHAWISHI kwa ajili ya ‘Ku(to)ridhika na kile ulichonacho kwa Neema, na kujaribu ‘Kujipima Msuli’ kule katika mapana ya Ustawi – yale mapana yanayojitenga na zile ‘Faraja’ za Kumiminiwa pasipo Ukomo – kumiminwa na na kile kilicho ni MFADHILI MKUU wa yetu yote (Kilatini > “ANNUIT COEPTIS” ).

Hili la UFADHILI na MFADHILI ndilo lafanya ile busara ya kusema, mtu ulivyo ni kompleksi ya ‘Utu-Nafsi-Roho’ hautojua thamani ya ulichonacho mpaka ukipoteze… Kwenye Injili, hili ndilo linasemwa ya kwamba kurejea kwa “Mwana Mpotevu” ni “Sherehe katika Ufalme”; kwa kuwa ‘Dhamira na Nia’ ya Kurejea nyumbani kwa Baba, ni konsayansi ya ‘Sikiri Aliye Maskini’ kukumbuka alikotokea – kuwa na “Nostalijia” huku akilinganisha / kumizanisha / kukontrasti zile situisha mbili za kimazingira :- (1) ‘Ukiwa ulioje ‘ pale alipo katika hali ya Kupotea, na (2) ‘Mapenzi Mema’ ya ‘Kuwa Kayani’ kuliko ni Asili.

Mtu u(a)livyo ni kompleksi ya ‘Utu-Nafsi-Roho’ huamua kutanga tanga mbali kwa kihoro cha matamani ya kimwili, akili na hisia; ambavyo, kimsingi, ni ‘Mwili ndicho kilicho mbali zaidi’ katika ‘Utu-Nafsi-Roho’ na basi kwa kuwa hivyo kule kuziendekeza tamaa za kimwili ndicho khasa ule muktadha akilifu wa ‘Kushawishika’ na ya Dunia / Ulimwengu. Hili lafanya Ushetani ni kujaribu ‘kuzishusha kinguvu zile Nguvu za mbingu’ katika “Utawala wa Nchi”; ambavyo ‘kufosi kingi’ hili ndiyo huzaa maradhi yote ya kijamii kama vile ‘Tamaa’, ‘Chuki’, ‘Dharau’, ‘Dhuluma’ na yote ya kule kukosekana kwa ‘Haki’ na ‘Amani’; kwa kuwa hayo ‘maovu’ huileta “Dhiki” katika Ustawi wa Wanajamii.

Kuzishusha kinguvu zile Nguvu za mbingu katika “Utawala wa Nchi” ni muktadha akilifu wa ‘kubaka UTU’ katika MAISHA-KUISHI-UISHO yaliyo ni Ujamii; ambavyo kutenda hivi ni utekelezaji wa ‘Nia na Dhamira Malishazi’ ilivyo ni uhujumu kwa ile Haki ya kweli na Amani kwa ‘Maslahi Binafsi’ ya wale wenye bidifu kuchukua hatua sahihi kivyao ili kuudukua ule muktadha akilifu kwa ‘Nia na Dhamira ya Kheri’ kwa “ Hekima, Umoja na Amani” miongoni mwa wanajamii wenye haja ya Maisha yenye ‘Unyoofu na Mapenzi Mema’; Katika Maisha, kuna basi ‘amani ya kweli’ na ‘amani ya uongo’...

Hili la nasibu ya uwepo wa ‘dhamira malishazi’ ama/na ‘dhamira kheri’ katika ‘Sura-Hadhi-Mwenendo’ wa Jamii, jamii yeyote iwe ni Duniani ama hata nje ya Sayari yetu, lafanya ile ‘amani ya uongo’ si chochote bali kutamalaki kwa ‘Unafiki’ katika zile harakati za kuishi – kuishi katika “Umma uliyokandamizika”, na tena wanajamii kubidi kushawishika kuicheza ngoma ya ‘Mashetani Makuu wanayoyajua’ na hata pia ‘Mashetani Makuu wasiyoyajua’; katika mchakato huu wa UISHO wenye ‘kutengeneza amani’ na ‘Wakubwa’, hata wanajamii wenyewe ‘hujipagaisha na mapepo yao wenyewe’ kwa sifa-tabia-hadhi zenye kudumisha fitina, njama na Ufisadi.

‘Amani ya Uongo’, kiuono na ufikirfu mifumo, ni muktadha akilifu wa sindromu za ‘Kuzorota kwa Afya Jamii’ ilivyo ni MARADHI; ambavyo ‘Uzima’ wa jamii yeyote hufuatisha kanuni ile ile ya ‘Utangamano wa Pumzi’ za ‘Uhai wa Jami’ kwa kuwa hata Ujamii wowote si chochote bali Uagrigati wa Densiti za Mifumo ya Utendaji. Hili lafanya, UPONYAJI wa MARADHI ni jambo lenye kufuatisha jambo lile lile la ‘Dhamira Njema’ ya kurudishia ‘Pumzi za Uzima’ kwa ule ‘Mwili wenye Maradhi’.

UPONYAJI wa MARADHI JAMII , kwa kurejea katika misingi ya UTU-NAFSI-ROHO, ni jambo ambalo kwenye Injili, Yesu Masiha alikazia: “Utafuteni Kwanza Ufalme wa Mbingu na Haki yake, Mengine Mtazidishiwa”… Hii ni kwa kuwa “Mbingu” ni metafo ya ASILI ILIYOSITIRIKA, ambako sisi sote tunaibuka na kufanyika kutokea katika Asili na basi kila mmoja wetu ana ‘Haki’ na ‘Kustahili’ yale yote ya MAISHA-KUISHI-UISHO pasipo kulazimika kuhitilafiana ama/na kuzonganazongana – ikiwa tunako “ku-JUA ilivyobora” na tena “Kuenenda katika Njia Zake”…

Basi ndiyo yawa, ‘Dhamira yenye Kheri’ si chochote bali ‘NIA YA KRISTU’ kwa kuwa Sura-Hadhi-Mwenendo wa jamii katika SHAURI hili ni MWANZO palipo na NENO; ambavyo basi “Kristu” ni turufu ya “Wokovu Mkuu” pale tutafutapo “Mwangaza” kwa kitendali: “Sisi Je, Tutapataje Kupona?”. Hili lafanya, Kristu ni Uponyaji na Ukombozi wa Mataifa kwa ajili ya ‘Haki na Amani’ ya kweli… Epifania ya ‘Uwepo wa Dawa’ kwa Mataifa.
....


View: https://www.youtube.com/watch?v=xBui-1Ic2vs&list=RDxBui-1Ic2vs&start_radio=1
 
😴😴
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…