Kuhusu hili janga la corona, humu mtaani yawezekana wengi wameupata bila kujijua na maambukizi yanaendelea!

Freyzem

JF-Expert Member
Jun 29, 2013
10,052
24,442
Jamani hili janga la corona siyo la kitoto!

Kama imefikia watu kulazimishwa kukaa ndani kwa viboko na wengine kufungulia simba mtaani, kwa kuhakikisha usalama wa wananchi basi ni dhahiri kuwa hili gonjwa ni tata sana!
Sasa kwa hapa kwetu tz hayo hayajafanyika ya kuwafungia watu ndani!

Licha ya jitihada za serikali zinazofanyika kwa kutoa elimu lakini bado wananchi wanaona ni kitu cha kawaida tu au pengine ni kitu ambacho hakipo!

hali ya mitaani kwa kweli sidhani kama wenye mamlaka wameona hili! Ipo hivi humo mtaani kuna watu wanaumwa aisee, wapo wanaoonekana wanakohoa, wakiwa na mafua pamoja na kusema wanajisikia vibaya lakini wanaendelea kutembea mitaani huko na kuendelea na shughuli zao za kawaida za kila siku kwa kujichanganya na umma!

Wengine wapo pia wenye dalili zinazofanana na zilizoainishwa za corona ila wanaficha, pengine kwa kuogopa kuwa wakisema watatengwa au watazua taharuki maeneo wanayoishi hivyo huamua kujitibu wenyewe kwa kununua panadol huko pharmacy na kuzitumia...

Licha ya wizara na wadau kutoa maelekezo namna ya kujikinga na kutoa taarifa pale unapopata dalili za ugonjwa huu, bado watu ni wachache wanaofuata hayo maelekezo!
Mathalani daladala bado zinakaza abiria, mwendokasi vile vile abiria wanalundikana!

Kwenye bajaji huko ndio wanakaa hakuna hewa, distance ni zero so tutegemee nini hapa!
ni wazi hili gonjwa lipo mtaani na watu wengi yawezekana kabisa wameukwaa ila kwa ubishi au kutokujua watu wanaendelea kuusambaza!

Naamini hata wanajf wapo ambao wameshaugua au wanaugua kwa sasa na wanadalili zinazofanana kabisa na za corona ila wapo mtaani na hata sasa wapo sehemu za umma wakiendelea na shughuli zao kama kawaida!

Jitihada zaidi zinahitajika, mambo yakiiva tutaanza kutupiana mpira! Tuambe kwamba kama wapo walioupata huu ugonjwa na wapo mtaani wanakula mitishamba basi madhara yasiwe makubwa au yasitokee kabisa!

Nawasilisha...


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kuna namba za Simu za kupiga bure endapo utajihisi dalili tajwa au kumuona mtu Ana tatizo hilo ili kunusuru wengine. Actions speak louder than words

Sent using Jamii Forums mobile app
Naogopa nisije nikapiga hizo namba nikaisumbua serikali kumbe naumwa mafua ya kawaida tu. Ingawa nimetoka kumeza dawa Sasa hivi Hali ya mafua kwa mbali naiona. Lakini siumwi corona.
 
Mtaani wapo wanaambukizana, virus wamezagaa mtaani!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Jamani hili janga la corona siyo la kitoto!

Kama imefikia watu kulazimishwa kukaa ndani kwa viboko na wengine kufungulia simba mtaani, kwa kuhakikisha usalama wa wananchi basi ni dhahiri kuwa hili gonjwa ni tata sana!
Sasa kwa hapa kwetu tz hayo hayajafanyika ya kuwafungia watu ndani!

Licha ya jitihada za serikali zinazofanyika kwa kutoa elimu lakini bado wananchi wanaona ni kitu cha kawaida tu au pengine ni kitu ambacho hakipo!

hali ya mitaani kwa kweli sidhani kama wenye mamlaka wameona hili! Ipo hivi humo mtaani kuna watu wanaumwa aisee, wapo wanaoonekana wanakohoa, wakiwa na mafua pamoja na kusema wanajisikia vibaya lakini wanaendelea kutembea mitaani huko na kuendelea na shughuli zao za kawaida za kila siku kwa kujichanganya na umma!

Wengine wapo pia wenye dalili zinazofanana na zilizoainishwa za corona ila wanaficha, pengine kwa kuogopa kuwa wakisema watatengwa au watazua taharuki maeneo wanayoishi hivyo huamua kujitibu wenyewe kwa kununua panadol huko pharmacy na kuzitumia...

Licha ya wizara na wadau kutoa maelekezo namna ya kujikinga na kutoa taarifa pale unapopata dalili za ugonjwa huu, bado watu ni wachache wanaofuata hayo maelekezo!
Mathalani daladala bado zinakaza abiria, mwendokasi vile vile abiria wanalundikana!

Kwenye bajaji huko ndio wanakaa hakuna hewa, distance ni zero so tutegemee nini hapa!
ni wazi hili gonjwa lipo mtaani na watu wengi yawezekana kabisa wameukwaa ila kwa ubishi au kutokujua watu wanaendelea kuusambaza!

Naamini hata wanajf wapo ambao wameshaugua au wanaugua kwa sasa na wanadalili zinazofanana kabisa na za corona ila wapo mtaani na hata sasa wapo sehemu za umma wakiendelea na shughuli zao kama kawaida!

Jitihada zaidi zinahitajika, mambo yakiiva tutaanza kutupiana mpira! Tuambe kwamba kama wapo walioupata huu ugonjwa na wapo mtaani wanakula mitishamba basi madhara yasiwe makubwa au yasitokee kabisa!

Nawasilisha...


Sent from my iPhone using JamiiForums


kwani waweza kua nao na kubaki nao home muda wote bila kujipeleka mwenyewa
 
Yawezekana corona ipo Siku nyingi na vile watu hatupimwi lakini madhara si mukubwa... Na huenda huwa inapona yenyewe ktk siku Chache tu
Wale wakenya waliokutwa nao huenda hata wasingepimwa wange survive tu na baadae ungeishia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Back
Top Bottom