Character X
JF-Expert Member
- Nov 22, 2012
- 331
- 382
katika Post hii, natafuta kuwashirikisha wana JF maswala kadhaa yanayo jionyesha sasa katika siasa za Tanzania kimataifa., lakini kwanza nataka kuanza na ziara hii ya Raisi Xi wa China na Mikataba ya makubaliano kadhaa iliyo fanyika hapa nchini hivi majuzi.
Kwanza nadhani swala hili (la mikataba) linahitaji kuangaliwa kwa makini sana kabla ya ku comment kwanamna yoyote ile.
Ukiiangalia mikataba hii kwa jicho la kibiashara zaidi kuliko jicho la kimsaada, utagundua SIO mikataba mibaya hatakidogo kibiashara. Ila kama uki itazama kwa jicho la kimsaada zaidi basi unaweza kusema mikataba hiyo SIO msaada wowote kwa Tanzania., nasema haya kwa sababu zifuatazo:
Msaada mtuhutoa pasipokufaidika yeye hasa, ila akitaraji kusaidia zaidi yule anayepokea msaada ule.,lakini katika biashara hutegemei kupewa kitu in your favor bila chochote in return kwa partner in business. kwahiyo hapa tuta angalia kwa undani (angalau ninaoweza kuwanao kwa sasa) nini tunachopata kwenye mikataba ile na kipi tunacho kitoa ili kupata tutakacho pata., yaani nini tutafaidi na kipi wata faidi waChina.
kufikia hapa tutakubaliana Wote kwamba mikataba ile ni ya kibiashara zaidi (exchange of goods and/or Services) kuliko ya kimsaada.
kwa madhumuni ya mjadala huu tuta tumia sehemu ya makubaliano baadhi ambayo tunayafahamu tayari juu ya mkataba wa ujenzi wa bandari ya bagamoyo kama case study.
Itazame mikataba ile (hasa sehemu zilizo wahi kuwa posted hapa JF) utagundua china ina weka picha ya kimataifa kwamba makubaliano haya ni ya kimsaada kwamfano sasa msaada wa ujenzi wa bandari hiyo ya bagamoyo lakini sasa maswali ya kujiuliza hapo ni wame toa msaada huu ILI IWEJE?
Ndugu zangu nime tazama swala hili kwa umakini (angalau kwa kiasi nilicho weza kwa sasa) yapo mambo ambayo ninataka kuya onyesha hapa, na haya yatakua katika makundi mawili.
Moja, (kibiashara)
Makubaliano hapa si kwamba tu yanataka bandari hiyo ijengwe na kandarasi za ki china ila pia ikikamilika iendeshwe na wachina kwa miaka 50 ili kurudisha mkopo wao., maana yake nini?
Hapa swala la interest kwa Uchina ni lipi? ni vyema kujua kwamba china contractors ni wengi na wana uwezo mkubwa lakini wana soko limited lenye competition kubwa sana sasa interest ya China hapa ni kuwatafutia soko contractors wao nje ya nchi, hili litakua na impact sio tu kibiashara lakini pia hata kiutamaduni, ushirika wa kimataifa na ukienda mbali zaidi hata ki intelijensia.
lakini pia, China ni kati ya nchi zenye population kubwa sana kuliko resources walizo nazo, in essence wanatatizo kubwa la unemployment huenda kubwa kuliko tulilo nalo hapa kwetu., Hapa wame tafuta ajira kwa ma engineers wakichina wanao ongezeka kila kukicha huku nafasi za kazi zimeendelea kujaa huko nyumbani sasa wamefungua mlango wa ajira kadhaa nchi ya mbali. Hii ni nchi inayojua kuwekeza si tu ndani ya nchi lakini hata nje nakufungua milago zaidi ya ajira ya watu wake., hiyo ni moja.
lakini pili, makubaliano ni kwamba waendeshe bandari hizi kwa miaka 50 baada ya kukamilika., hii inakuambia nini?
kwamba moja, wanaendelea kuongeza ajira za wachina hata nje ya china kwa miaka 50 zaidi lakini pia, wanajua kuhusu ubabaishaji wa nchi za ki africa katika uendeshaji wa mashirika ya umma na ulipaji madeni., sasa wanataka waendeshe wenyewe ili pamoja na kwamba wachina wengi zaidi wataendelea kupata ajira lakini pia pesa yao waliyo invest pale irudi.
utagundua haiishii tu kenye kutaka kuiendesha wenyewe, lakini pia wame weka clause inayo bind Tanzania katika kuhakikisha bandari watakayo ijenga itakua kubwa zaidi ya nyingine yoyote., maanake isije ikaundwa bandari kubwa zaidi ya hiyo ndani ya kipindi hicho kiasi chatengeneza competition ambayo huenda ika sababisha hii watakayo jenga kwenda out of business nakusababisha watu wao wasi pate ajira, au mkopo wao usilipike.
lakini hapa hasa swala sio kuangalia tu wao watapata nini katika biashara hii, lakini tujiulize je? tusipo kubali mikataba hii tunauwezo wa kujenga bandari hiyo kwa resources tulizo nazo wenyewe? nadhani hapa jibu ni HAPANA! nakama hatuna je tuendelee tu kukaa bila kua na maendeleo eti kwasababu hatutaki wachina waiendeshe kwa miaka 50 na kutumia mda huo kulipa mkopo huo? na kwamba hatutaki watumie contractors wao? je tukipewa sisi wapo ma contractors wazawa watakao weza kusimamisha project ya ukubwa huo??
Nadhani mikataba hii uki itazama kwa jicho la kibiashara ni mikataba nafuu sana., inayo lenga tukuwapa wachina wachache ajira nje ya nchi na kulipa mkopo wao lakini upande mwingine kuiachia tanzania bandari kubwa itakayo zalisha kwaajili ya watanzania miaka mingi baada ya miaka hiyo hamsini ya kurejesha mkopo huo.,
na kwa hakika tunge taka tuiendeshe wenyewe bandari ile na kulipa mkopo ule wenyewe huenda tungelipa mkopo huo kwa miaka mia mbili.,
kama pesa za kujenga daraja tu zinalipwa kwa miaka 40, sembuse bandari na installation ya vifaa vyote?
ndugu zangu kibiashara kilicho fanyika ni win-win situation KABISA!!
Kimahusiano
China ni rafiki wa Tanzania kwa miaka yote toka baada ya uhuru. Urafiki wa China na Tanzania haukuanza leo wala jana. yako mambo mengi ambayo yame kwisha fanyika na marafiki hawa wawili,. viwanda kama URAFIKI ni mfano mmoja tu. Huu ni wakati ambapo Tanzania inatunukiwa na rafiki zao hao kwakuendeleza urafiki huo.
lakini kubwa zaidi ni hili, kwa kawaida mataifa haya makubwa huwa na allies katika kila bara dunia nzima., hii inatengeneza nguvu situ ya sauti ya taifa katika forums mbali mbali lakini pia hutengeneza nguvu katika Representative Forums mbalimbali za kimataifa. allies hawa huonyeshwa ceremonially kwa matukio ya wazi kama haya., hotuba ya kwanza ya raisi, au/na safari ya kwanza baada tu ya kuchukua kiti., huonyesha symbolically huyu mtu au hili taifa lina fungamana na watu gani., hutafuta kuwaweka wazi marafiki zake na kwanamna flani hutafuta kuonyesha kuwatambua adui zake.
safari ya kwanza ya Raisi wa China anaamua kuifanya yakuja Tanzania.,
kwakifupi, raisi bush aliwahi kuja hapa pia na katika safari yake, mengi yalijiri lakini yote yalionyesha ushawishi flani., ziko fedha nyingi zilizo tolewa kwa tanzania kipindi kile.,na watu wengi wali hoji kulikoni? tena ukitafiti utagundua Tanzania kipindi flani hapo nyuma ndiyo ilikua nchi inayo pokea fedha nyingi kama msaada kutoka Uingereza kuliko nchi nyingine yoyote Duniani.
kama hiyo haitoshi raisi wa kwanza kualikwa na Obama mara tu baada ya kuapishwa kwake awamu ile ya kwanza alikua Raisi Kikwete (unaweza kusema labda kwakua alikua mwenyekiti wa AU kwa kipindi kile lakini je, alipo maliza mda wake aliye pokea kijiti naye alienda?), ukiyatazama haya kwaundani naukakumbuka juu ya siasa ya Tanzania ya kipindi cha mwalimu yakuto fungamana na upande wowote, utagundua kulikuwapo mvutano au ushawishi hapa., upande mmoja wa marekani inayo fahamu China kama uchumi unaokuwa kwa kasi sana sana kiasi cha kua tishio kwake hata ki tecnology na ki jeshi, na upande mwingine China ambayo imekua rafiki wa Tanzania kwa muda mrefu toka kipindi cha Uhuru, na siasa zinazo karibia kufanana.
lakini katika kutilia mkazo hili, itafute hotuba ya raisi kikwete bungeni Dodoma juzi katika Ziara hii ya Raisi Xi wa China ilikua hotuba kwanza ya kiingereza., kwanini? angeweza kuongea kiswahili, mbona hata Raisi Xi alikua akiongea kichina na kutafsiriwa., yaani maanake Raisi Xi hata kiingereza hajui., sasa unaongea kiingereza ili iwaje wakati unaeongea nae hajui hata icho kiingereza., utasema labda watafsiri wakichina hawajui kiswahili lakini sikweli ukitembelea ualozi wa china utashangaa sana kuna wachina wanaongea kiswahili kama wa pemba., maanake nini? aliongea kiingereza kwasababu kabisa., kwamakusudi kabisa., ile haikua hutoba tu kama nyingine ile ilikua NI HOTUBA YA KUSIKILIZWA NA DUNIA NZIMA, nihotuba yakutangaza msimamo.
itafute hotuba ile utagundua pia ni hotuba yenye utafauti mkubwa na hotuba nyingine nyingi za Raisi kikwete., hotuba ile ilikua kakamavu yenye kutafuta kuonyesha msimamo wa nchi., ikiwa na phrases "kama mtu asi tuhukumu juu ya urafiki au uadui wetu na mtu mwingine yoyote" (not an exact quote)., ikiwa namaana tumeamua kuwa marafiki wa China nahuo ndiyo msimamo wetu.
Kwamtu mwenyekutafiti siasa za dunia utagundua Si tu hotuba ya raisi kikwete lakini pia safari ya Raisi Xi zilikua staged Strategically Kabisa!
hapakua na wakati bora zaidi wa kutangaza wazi wazi ally wako wa sera zako za kimataifa kama Safari ya Kwanza ya Raisi Mpya wa Nchi kubwa kama China kufanyika kwenye nchi hiyo tena mapema kabisa baada tu yakua raisi. Hili limefanywa tukio la kihistoria., siotu ziara yakuaja kusign mikataba., No! hiyo mikataba ni ziada yake., lakini hasa nikutangazia dunia tumeamua nini, chakungoja sasa ni response ya wale wengine.
Baada ya kusema hayo mengi nije kwenye swala la China na maendeleo ya Tanzania., nina weza kusema China hapa haitoi msaada Sana kivile kama wengi wanavyo weza kufikiri., ila inafanya biashara, biashara ambayo inamanufaa kwao lakini pasipo kukosa shukrani lazima niseme itakua na manufaa kwetu pia.
Comrades,
ni hayo
Kwanza nadhani swala hili (la mikataba) linahitaji kuangaliwa kwa makini sana kabla ya ku comment kwanamna yoyote ile.
Ukiiangalia mikataba hii kwa jicho la kibiashara zaidi kuliko jicho la kimsaada, utagundua SIO mikataba mibaya hatakidogo kibiashara. Ila kama uki itazama kwa jicho la kimsaada zaidi basi unaweza kusema mikataba hiyo SIO msaada wowote kwa Tanzania., nasema haya kwa sababu zifuatazo:
Msaada mtuhutoa pasipokufaidika yeye hasa, ila akitaraji kusaidia zaidi yule anayepokea msaada ule.,lakini katika biashara hutegemei kupewa kitu in your favor bila chochote in return kwa partner in business. kwahiyo hapa tuta angalia kwa undani (angalau ninaoweza kuwanao kwa sasa) nini tunachopata kwenye mikataba ile na kipi tunacho kitoa ili kupata tutakacho pata., yaani nini tutafaidi na kipi wata faidi waChina.
kufikia hapa tutakubaliana Wote kwamba mikataba ile ni ya kibiashara zaidi (exchange of goods and/or Services) kuliko ya kimsaada.
kwa madhumuni ya mjadala huu tuta tumia sehemu ya makubaliano baadhi ambayo tunayafahamu tayari juu ya mkataba wa ujenzi wa bandari ya bagamoyo kama case study.
Itazame mikataba ile (hasa sehemu zilizo wahi kuwa posted hapa JF) utagundua china ina weka picha ya kimataifa kwamba makubaliano haya ni ya kimsaada kwamfano sasa msaada wa ujenzi wa bandari hiyo ya bagamoyo lakini sasa maswali ya kujiuliza hapo ni wame toa msaada huu ILI IWEJE?
Ndugu zangu nime tazama swala hili kwa umakini (angalau kwa kiasi nilicho weza kwa sasa) yapo mambo ambayo ninataka kuya onyesha hapa, na haya yatakua katika makundi mawili.
Moja, (kibiashara)
Makubaliano hapa si kwamba tu yanataka bandari hiyo ijengwe na kandarasi za ki china ila pia ikikamilika iendeshwe na wachina kwa miaka 50 ili kurudisha mkopo wao., maana yake nini?
Hapa swala la interest kwa Uchina ni lipi? ni vyema kujua kwamba china contractors ni wengi na wana uwezo mkubwa lakini wana soko limited lenye competition kubwa sana sasa interest ya China hapa ni kuwatafutia soko contractors wao nje ya nchi, hili litakua na impact sio tu kibiashara lakini pia hata kiutamaduni, ushirika wa kimataifa na ukienda mbali zaidi hata ki intelijensia.
lakini pia, China ni kati ya nchi zenye population kubwa sana kuliko resources walizo nazo, in essence wanatatizo kubwa la unemployment huenda kubwa kuliko tulilo nalo hapa kwetu., Hapa wame tafuta ajira kwa ma engineers wakichina wanao ongezeka kila kukicha huku nafasi za kazi zimeendelea kujaa huko nyumbani sasa wamefungua mlango wa ajira kadhaa nchi ya mbali. Hii ni nchi inayojua kuwekeza si tu ndani ya nchi lakini hata nje nakufungua milago zaidi ya ajira ya watu wake., hiyo ni moja.
lakini pili, makubaliano ni kwamba waendeshe bandari hizi kwa miaka 50 baada ya kukamilika., hii inakuambia nini?
kwamba moja, wanaendelea kuongeza ajira za wachina hata nje ya china kwa miaka 50 zaidi lakini pia, wanajua kuhusu ubabaishaji wa nchi za ki africa katika uendeshaji wa mashirika ya umma na ulipaji madeni., sasa wanataka waendeshe wenyewe ili pamoja na kwamba wachina wengi zaidi wataendelea kupata ajira lakini pia pesa yao waliyo invest pale irudi.
utagundua haiishii tu kenye kutaka kuiendesha wenyewe, lakini pia wame weka clause inayo bind Tanzania katika kuhakikisha bandari watakayo ijenga itakua kubwa zaidi ya nyingine yoyote., maanake isije ikaundwa bandari kubwa zaidi ya hiyo ndani ya kipindi hicho kiasi chatengeneza competition ambayo huenda ika sababisha hii watakayo jenga kwenda out of business nakusababisha watu wao wasi pate ajira, au mkopo wao usilipike.
lakini hapa hasa swala sio kuangalia tu wao watapata nini katika biashara hii, lakini tujiulize je? tusipo kubali mikataba hii tunauwezo wa kujenga bandari hiyo kwa resources tulizo nazo wenyewe? nadhani hapa jibu ni HAPANA! nakama hatuna je tuendelee tu kukaa bila kua na maendeleo eti kwasababu hatutaki wachina waiendeshe kwa miaka 50 na kutumia mda huo kulipa mkopo huo? na kwamba hatutaki watumie contractors wao? je tukipewa sisi wapo ma contractors wazawa watakao weza kusimamisha project ya ukubwa huo??
Nadhani mikataba hii uki itazama kwa jicho la kibiashara ni mikataba nafuu sana., inayo lenga tukuwapa wachina wachache ajira nje ya nchi na kulipa mkopo wao lakini upande mwingine kuiachia tanzania bandari kubwa itakayo zalisha kwaajili ya watanzania miaka mingi baada ya miaka hiyo hamsini ya kurejesha mkopo huo.,
na kwa hakika tunge taka tuiendeshe wenyewe bandari ile na kulipa mkopo ule wenyewe huenda tungelipa mkopo huo kwa miaka mia mbili.,
kama pesa za kujenga daraja tu zinalipwa kwa miaka 40, sembuse bandari na installation ya vifaa vyote?
ndugu zangu kibiashara kilicho fanyika ni win-win situation KABISA!!
Kimahusiano
China ni rafiki wa Tanzania kwa miaka yote toka baada ya uhuru. Urafiki wa China na Tanzania haukuanza leo wala jana. yako mambo mengi ambayo yame kwisha fanyika na marafiki hawa wawili,. viwanda kama URAFIKI ni mfano mmoja tu. Huu ni wakati ambapo Tanzania inatunukiwa na rafiki zao hao kwakuendeleza urafiki huo.
lakini kubwa zaidi ni hili, kwa kawaida mataifa haya makubwa huwa na allies katika kila bara dunia nzima., hii inatengeneza nguvu situ ya sauti ya taifa katika forums mbali mbali lakini pia hutengeneza nguvu katika Representative Forums mbalimbali za kimataifa. allies hawa huonyeshwa ceremonially kwa matukio ya wazi kama haya., hotuba ya kwanza ya raisi, au/na safari ya kwanza baada tu ya kuchukua kiti., huonyesha symbolically huyu mtu au hili taifa lina fungamana na watu gani., hutafuta kuwaweka wazi marafiki zake na kwanamna flani hutafuta kuonyesha kuwatambua adui zake.
safari ya kwanza ya Raisi wa China anaamua kuifanya yakuja Tanzania.,
kwakifupi, raisi bush aliwahi kuja hapa pia na katika safari yake, mengi yalijiri lakini yote yalionyesha ushawishi flani., ziko fedha nyingi zilizo tolewa kwa tanzania kipindi kile.,na watu wengi wali hoji kulikoni? tena ukitafiti utagundua Tanzania kipindi flani hapo nyuma ndiyo ilikua nchi inayo pokea fedha nyingi kama msaada kutoka Uingereza kuliko nchi nyingine yoyote Duniani.
kama hiyo haitoshi raisi wa kwanza kualikwa na Obama mara tu baada ya kuapishwa kwake awamu ile ya kwanza alikua Raisi Kikwete (unaweza kusema labda kwakua alikua mwenyekiti wa AU kwa kipindi kile lakini je, alipo maliza mda wake aliye pokea kijiti naye alienda?), ukiyatazama haya kwaundani naukakumbuka juu ya siasa ya Tanzania ya kipindi cha mwalimu yakuto fungamana na upande wowote, utagundua kulikuwapo mvutano au ushawishi hapa., upande mmoja wa marekani inayo fahamu China kama uchumi unaokuwa kwa kasi sana sana kiasi cha kua tishio kwake hata ki tecnology na ki jeshi, na upande mwingine China ambayo imekua rafiki wa Tanzania kwa muda mrefu toka kipindi cha Uhuru, na siasa zinazo karibia kufanana.
lakini katika kutilia mkazo hili, itafute hotuba ya raisi kikwete bungeni Dodoma juzi katika Ziara hii ya Raisi Xi wa China ilikua hotuba kwanza ya kiingereza., kwanini? angeweza kuongea kiswahili, mbona hata Raisi Xi alikua akiongea kichina na kutafsiriwa., yaani maanake Raisi Xi hata kiingereza hajui., sasa unaongea kiingereza ili iwaje wakati unaeongea nae hajui hata icho kiingereza., utasema labda watafsiri wakichina hawajui kiswahili lakini sikweli ukitembelea ualozi wa china utashangaa sana kuna wachina wanaongea kiswahili kama wa pemba., maanake nini? aliongea kiingereza kwasababu kabisa., kwamakusudi kabisa., ile haikua hutoba tu kama nyingine ile ilikua NI HOTUBA YA KUSIKILIZWA NA DUNIA NZIMA, nihotuba yakutangaza msimamo.
itafute hotuba ile utagundua pia ni hotuba yenye utafauti mkubwa na hotuba nyingine nyingi za Raisi kikwete., hotuba ile ilikua kakamavu yenye kutafuta kuonyesha msimamo wa nchi., ikiwa na phrases "kama mtu asi tuhukumu juu ya urafiki au uadui wetu na mtu mwingine yoyote" (not an exact quote)., ikiwa namaana tumeamua kuwa marafiki wa China nahuo ndiyo msimamo wetu.
Kwamtu mwenyekutafiti siasa za dunia utagundua Si tu hotuba ya raisi kikwete lakini pia safari ya Raisi Xi zilikua staged Strategically Kabisa!
hapakua na wakati bora zaidi wa kutangaza wazi wazi ally wako wa sera zako za kimataifa kama Safari ya Kwanza ya Raisi Mpya wa Nchi kubwa kama China kufanyika kwenye nchi hiyo tena mapema kabisa baada tu yakua raisi. Hili limefanywa tukio la kihistoria., siotu ziara yakuaja kusign mikataba., No! hiyo mikataba ni ziada yake., lakini hasa nikutangazia dunia tumeamua nini, chakungoja sasa ni response ya wale wengine.
Baada ya kusema hayo mengi nije kwenye swala la China na maendeleo ya Tanzania., nina weza kusema China hapa haitoi msaada Sana kivile kama wengi wanavyo weza kufikiri., ila inafanya biashara, biashara ambayo inamanufaa kwao lakini pasipo kukosa shukrani lazima niseme itakua na manufaa kwetu pia.
Comrades,
ni hayo