Ndibalema
hakuna mahala popote imeongelewa Mkataba wa ujenzi wa bandari na EPZ Bgamoyo utakuwa ni wa miaka 50. Hizo ni speculations za watu wanaotaka kujenga hoja za kuupinga mradi. Kilichosainiwa ni framework agreement, wala haina details zozote za gharama au muda wa kurudisha uwekezaji uliofanyika. Ile framework agreement ndio imetengeneza njia ya kuanza mazungumzo ya kina kuhusu namna ya kutekeleza mradi wenyewe.
Lakini for the sake of argument hata ingekuwa kweli kuna mkataba wa miaka 50, sio lazima iwe ni jambo baya,kitakacho determine miaka ni uwekezaji uliofanyika ni wa kiasi gani (thamani gani) na return of investment itachukua muda gani. Hizo ndio factors zinazo determine muda wa mtu kuendesha mradi chni ya utaratibu wa Build Operate Transfer (BOT).
Ipo mifano ya mradi kama wa Eurostar- reli ya kutoka Uingereza kwenda Ufaransa ambayo ujenzi wake uligharimu Pauni za Kiingereza Bilioni 5 (takriba dola za kimarekani Bilioni 10). Makisio ya awali ya mwekezaji kuendesha reli ile na kurejesha faida ilikuwa ni miaka 50. Lakini baada ya kuanza kazi, reli ile ilikumbwa na misukosuko kadhaa ikiwemo na abiria kutoitumia sababu ya uwepo wa other cheaper options kama low cost airlines (Easyjet, Ryan Air), ongezeko la gharama za uendeshaji kutokana na bei ya mafua kupata, mtikisiko wa uchumi barani ulaya n.k mwisho wake wale wawekezaji walirudi mezani na Serikali za Uingereza na Ufaransa wakakubaliana kwamba miaka 50 haitoshi kurejesha kiasi cha fedha kilichowekezwa...ikaamuliwa waongezewe miaka 40 mingine which means jumla miaka 90. (Ukitaka kusoma kwa undani kuhusu mradi huu nenda kwenye link hii:
Illustrative Examples of PPP in the EU
Nimelazimika kukusimulia ya Uingereza ili tupate picha kwamba suala la muda wa mwekezaji kuendesha mradi unakuwa determned na factors nyingi........ni vrma kuzielewa badala ya kukurupuka kushambulia hoja bila kuwa na facts za kutosha kuhusu mradi wenyewe.
Jambo la muhimu la kuzingatia ni kwamba mradi wa Bandari ya Bagamoyo na Eneo la viwanda utakuwa na manufaa mengi from day one utakapoanza. Wananchi wapatao 3000 watapata ajira za muda za moja kwa moja katika ujenzi wa bandari na EPZ, wananchi wengine wapatao 2000 na zaidi watapata ajira zisizo za moja kwa moja kama vile Mama Ntilie watakaouza chakula, wenye nyumba zao watakaowapangisha wajenzi, wauza vinywaji, watoa huduma za usafiri-daladala, taxi, maroli ya kusafirisha mizigo n.k
Faida nyinginezo za mradi huo ni kwamba mara utakapokamilika, thamani ya properties zilizopo eneo la mradi na maeneo ya jirani kama vile Bunju,Boko, Mbezi, Tegeta n.k yatapanda thamani na kuwafaidisha wamiliki endapo watahitaji kukodisha property zao au kuzitumia kuwekea rehani kupata mikopo benki n.k
Faida nyingine ni za moja kwa moja kwa Serikali......ukubwa wa bandari maana yake volume ya mizigo itakayopitia hapo itaongezeka ambapo Serikali itaongeza mapato kupitia IMPORT DUTY, customs Duty......bandari itakapokamilika itaajiri wafanyakazi wasiopungua 1000, eneo la viwanda litakapomilika-litawezesha viwanda vingi kujengwa (by the way Mwekezaji ndio atavutia viwanda kutoka sehemu mbalimbali duniani kuja kuweka viwanda vyao kwenye eneo hilo na tayari ameshapata wawekezaji walio tayari kuwekeza provided kuna efficient port) na viwanda hivyo vitatoa ajira kwa wananchi wasiopungua 50,000 na zaidi.
Kwa faida ya wasiojua kwanini viwanda vingi vitakuja kuwekeza katika eneo hilo:
1) bidhaa zitakazozalishwa hapa Tanzania katika eneo hilo la viwanda zitaweza kufaidi misamaha ya kodi inayotolewa kwa Nchi masikini huko Marekani (Chini ya AGOA); Ulaya (Everything but Arms EBA), Japan (TICAD consession), na China yenyewe iliyotoa msamaha wa kodi kwa asilimia 95 ya bidhaa zinazozalishwa Tanzania
2) Cheap labour- ukweli ni kwamba toka China uchumi wake umekua, factors of production zilizokuwa zinawa favour zimetoweka....Afrika ndio ina fursa ya kuziba pengo hilo la China
3) Kwakuwa viwanda vingi lengo lao ni kuzalisha bidhaa za kupeleka nje ya nchi- uwepo wa bandari kubwa yenye mtandao mkubwa duniani inakuwa ni kivutio kikubwa kwao.....mwekezaji wa Bandari ya Bagamoyo anao mtandao wa bandari kadhaaa ulimwenguni....wao ndio wanamiliki bandari tano kati ya bandari kubwa kumi duniani....ikiwemo bandari ya Hongkong, Schenzen n.k
Ukiachilia ajira etc.....serikali inaweza kufaidika pia kwa kupata mrahaba (royalty) katika kipindi chote ambacho mwekezaji ataendesha bandari ili kurejesha uwekezaji aliofanya.
La muhimu hapa ni wataalam wetu watakao negotiate mkataba huo kuwa makini na kuhakikisha serikali inapata WIN-WIN deal na hao wawekezaji. Kwenye nchi nyingine kama Singapore, India, Ulaya, Marekani...zipo specialised firms zinazotoa huduma ya kuguide serikali zinazo negotiate na wawekezaji complex transactions za aina hii. Ipo haja ya Serikali kuangalia uwezekano wa ku procure services za firm za aina hiyo.