Tatizo la Slaa siku zote anaongea kama mwanaharakati kazi kukosoa tu, Slaa unatakiwa useme mie tafanya A.B.C.D.
Slaa, sijui anaishi dunia ya wapi unashangaa serikali kuanzisha kodi maalum kwenye plate namba za magari eti unasema ni kuhalalisha mafisadi kutamba, Slaa huu utaratibu upo dunia nzima hata huku Ulaya na Marekani kwa wafadhili wenu wanatumia huo utaratibu tena serikali wamechelewa sana.
Tatizo la Slaa mtu akiishi maisha mazuri kwake ni fisadi weka wazi tujue sera zako kuhusu migodi Chadema wakichukuwa nchi watataifisha migodi yote au mtafanyaje.
Mkuu hii bajeti ya mwaka huu ni mbovu kuwahi kushuhudiwa Tanzania na ndio maana mbunge wa Kisesa CCM ameapa kuipinga kwa nguvu zote na yuko tayari kufukuzwa CCM kuliko kuunga mkono alichokiita uchafu.
Kama hii ni kweli basi eitha una laana au umerukwa akili. Huwezikuwa unauona ukweli kisha unaukana waziwazi.Bsc (UD),MSC(pretoria univ.) na ya kwako mkuu?
Mkuu hii bajeti ya mwaka huu ni mbovu kuwahi kushuhudiwa Tanzania na ndio maana mbunge wa Kisesa CCM ameapa kuipinga kwa nguvu zote na yuko tayari kufukuzwa CCM kuliko kuunga mkono alichokiita uchafu.
Slaa anajua nini kuhusu bajeti? hivi si vituko waungwana?
Dr slaa waambie,kwa mara nyingine kura yangu inakusubiri 2015 na nakuahidi nitailinda kwa garama yeyote!ccm akili imewaishia hadi wanakopa.
Mkuu inawezekana bajeti ikawa mbovu lakini Slaa, mbona uwa asemi mie nikichukuwa nchi tawafanyia haya Watanzania A.B.C.D. ambayo CCM wameshindwa kuwafanyia Watanzania, sio kukosoa tu kama mwanaharakati, Slaa, ebu tuambie Chadema wakichukuwa nchi watavunja mikataba yote ya madini na kutaifisha migodi yote ya dhahabu na Almasi au utafanyaje Watanzania wanataka kujua sera zako mapema.
Kiongozi Mkuu wa upinzani nchini na Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CDM Dr Wilbroad Slaa amesema ameshangazwa na kushtushwa na bajeti ya serikali ya mwaka huu.
Dr Slaa amesema serikali ya CCM imefikia mwisho wa kufikiri kwa kuomba misaada na mikopo kwa wahisani kwa lengo la kukidhi fungu la matumizi ya serikali.Dr Slaa amesema hakungekuwa na tatizo kama mikopo na misaada ingeelekezwa kwenye maendeleo kama ujenzi wa viwanda nk.Dr Slaa alihoji unakopa ili mlipane mishahara na marupurupu?
Dr Slaa alishangazwa pia na serikali kutegemea vinywaji kila mwaka katika kuongeza kodi na kusema huko ni kukosa ubunifu.Mbona hawaangalii madini? Alihoji kiongozi huyo.
Dr Slaa aliponda pia uamuzi wa kuanzisha kodi maalum kwenye plate namba za magari zenye majina ya watu na kusema huko ni kuleta matabaka katika nchi na kuhalalisha mafisadi kutamba na fedha zao haramu.
Source:Tanzania Daima Jumamosi
Siyo kila kitu anachofanya mfadhili wako basi na wewe unafanya,ungejisikiaje kama Matonya na uomba omba wake,anunue benzi ili awe sawa na wafadhili wake?Tatizo la Slaa siku zote anaongea kama mwanaharakati kazi kukosoa tu, Slaa unatakiwa useme mie tafanya A.B.C.D.
Slaa, sijui anaishi dunia ya wapi unashangaa serikali kuanzisha kodi maalum kwenye plate namba za magari eti unasema ni kuhalalisha mafisadi kutamba, Slaa huu utaratibu upo dunia nzima hata huku Ulaya na Marekani kwa wafadhili wenu wanatumia huo utaratibu tena serikali wamechelewa sana.
Tatizo la Slaa mtu akiishi maisha mazuri kwake ni fisadi weka wazi tujue sera zako kuhusu migodi Chadema wakichukuwa nchi watataifisha migodi yote au mtafanyaje.
heshima mkuu Molemo!
Nimeipenda sana hii" KIONGOZI MKUU WA UPINZANI NCHINI-dr slaa"
inasikitisha sana pale ambapo unakopa ili ule,ina maana wewe ni tegemezi,kuisifia bajeti hii ya tz ni kusifia utegemezi
Ama kweli!! Mheshimiwa unatoka pori gani wewe? ha! ha! ha! Hapa kinachoongelewa ni hoja na sio mtu!! Great minds discuss ideas; average minds discuss events; small minds discuss people... (Eleanor Roosevelt).