Kugoma kurejesha fedha uliyokopeshwa na jamaa, ndugu, rafiki au mtu yeyote unakuwa unafikiria nini?

Good Father

JF-Expert Member
Feb 28, 2014
10,275
18,352
Habari za majukumu wakuu.

Pole na pilika za kutafuta maisha sambamba na kupambana na janga la Covid-19. Mungu ni mwema atatuvusha, tuendelee kuchukuwa tahadhari kujikinga na kuwakinga wenzetu.

Niende kwenye kiini cha mada yangu.

Kuna tabia flani imezuka au nisema labda ilikuwepo hata kwa watangulizi wetu (babu na bibi enzi hizo), unakuwa na rafiki ama ndugu yako mnashibana sana, mnasikilizana sana. Inatokea anapata shida au dharura, anakujia umkopeshe fedha kiasi flani aweze kutatua shida yake.

Kutokana na mnavyoheshimiana roho inakwambia sio vema uache kumsaidia rafiki yako au ndugu yako, unaingia ndani unakomba akiba yako kiduchu uliyokuwa nayo unampa kwa ahadi ya kurejesha baada ya siku mbili tatu let say anakwambia baada ya siku 2 atarudisha.

Unampa anashukuru sana anaondoka, sasa unakaa wiki mbili au mwezi au miezi kadhaa baadae hujapata mrejesho hata wa kuambiwa labda amekwama au mambo yalikwenda tofauti na alivyotarajia, yaani anakaa kimya tu, unamuona mitandaoni akipost mavitu kwa furaha tele, anasahau wewe ulijibana ukamuazima fedha ashughulikie shida iliyomkabili wakati ule.

Hebu wakuu tuelezane kiutu uzima hii tabia ya kitoto namna hii huwa inalenga nini? Kwamba marafiki tusisaidiane mwenzetu anapopata shida? Tabia kama hii inajenga picha gani na wewe unayekopeshwa na hurejeshi wala kutoa taarifa kwamba umekwama somewhere hii ni nini? Mambo ya kijinga kabisa.

Mtu anakukopa unamheshimu sana kiasi kwamba hata kumdai unaona aibu, lakini yeye kwa ujasiri mkubwa anakupotezea as if wewe huna shida na fedha.

Vijana wenzangu, wazee, mabibi na mabwana hebu tuache mambo ya ajabu, mtu utakuja kupata shida watu wanakukwepa maana una tabia ya kudhurumu kirahisi rahisi.

Najua mnanielewa, wewe mwenye tabia kama hii iache maana haina siha njema, watu tunaishi kwa kutegemeana, usilazimishe tuishi kwa kubaguana tukashindwa kusaidiana.

Tuendelee kunawa mikono kwa maji tiririka na tutumie vitakasi mikono vyenye alcohol isiyopungua 60%

Asanteni kwa kunielewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dash ,mkuu kusema kweli hili jambo huwa linakera sana

Unakuta pesa yenyewe unasubirie akulipe ili ufanye mambo yako ya maana ,
Kumbe mwenzako wala hawazi kuwa anadaiwa

Sasa mtu unaazimwa pesa kwa makubaliano ya kurudisha baada ya wiki kadhaa au mwezi tens bila riba alafu unaleta usumbufu kwenye kulipa

Hili jambo linafikirisha sana
 
Kuna jamaa yangu yeye mda mwingi kulalamika, akikopa kurudisha hataki kabisa
Mkikutana anaweza ongea yeye mda ote huku blah blah nyingi

Ukimkumbusha tu kidogo atajitetea kwa shida , akijisahau tu kidogo utamsikia mara oh hiki kipindi cha Corona nakula matunda sana siunajua malimao machungwa nini n.k huku mbwembwe nyingi zakutumia pesa,
Kiukweli inauma sana ipo siku! Tamchangamkia
😑Ukiwa mpole sana kwa mbongo lazima uteseke
 

Attachments

  • Screenshot_2020-05-02-23-03-04.png
    Screenshot_2020-05-02-23-03-04.png
    9.8 KB · Views: 5
Kama hela unayo msaidie tu, akishindwa kulipa msamehe(hata kama hela anayo, maana wengine wana roho ya ubinafsi). watanzania wengi ni maskini na njaa kali.

HUWEZI KUWA MASKINI KWA KUMSAIDIA NDUGU, JIRANI AU RAFIKI YAKO.
 
Linapokuja swala kama hili kila mwana JF anajidai yeye ni mwema sana na hadaiwi au yeye ndio mtoaji wa mikopo tu.
Mimi ni miongoni mwa watu wagumu sana kulipa madeni, kama hivi yaani
"KUTOKA BR@NCH: MAWAKALA NA WANASHERIA Wanaendelea kuondoa WALAGHAI wa pesa za BR@NCH kwa kutuma na kusambaza TAARIFA za wadaiwa kwenye TAASISI ZA KIFEDHA ikiwemo BANK, SACCOS NA VIKOBA vilivyopo nchini. Wameamua kuwatangaza pamoja na kuwafuata mitaani LIPA LEO HII UEPUKANE NA FEDHEHA KAMPUN NO:256699."
" MUHIMU:Kulingana na KIFUNGU CHA 44(1)SHERIA YA MWENENDO WA SHAURI LA MADENI, deni linafunga endapo mdaiwa ATAKAIDI kulipa deni lake kulingana na hukumu,pia AMRI ya XXI kanuni ya 35(I) inaruhusu mdaiwa kukamatwa endapo atakiuka wito, MDAIWA WA BR@NCH Kamilisha Mkopo Wako Sasa Bila Shuruti KAMP NO:256699. "
" UMEKIUKA AGIZO lililokutaka ukamilishe marejesho yako BR@NCH Taasisi Ya mikopo imesikitishwa na Kitendo Hicho Tuhisi unadhulumu, Jukumu letu tumelitimiza Vizuri kukuhimiza ukamilishe malipo hatuta husika na madhara yatakayo jitokeza pindi mamlaka itakapo chukua hatua Kali Na stahiki dhidi yako Lipa Leo."
Kila siku wananitumia na kunipigia simu
 
Linapokuja swala kama hili kila mwana JF anajidai yeye ni mwema sana na hadaiwi au yeye ndio mtoaji wa mikopo tu.
Mimi ni miongoni mwa watu wagumu sana kulipa madeni, kama hivi yaani
"KUTOKA BR@NCH: MAWAKALA NA WANASHERIA Wanaendelea kuondoa WALAGHAI wa pesa za BR@NCH kwa kutuma na kusambaza TAARIFA za wadaiwa kwenye TAASISI ZA KIFEDHA ikiwemo BANK, SACCOS NA VIKOBA vilivyopo nchini. Wameamua kuwatangaza pamoja na kuwafuata mitaani LIPA LEO HII UEPUKANE NA FEDHEHA KAMPUN NO:256699."
" MUHIMU:Kulingana na KIFUNGU CHA 44(1)SHERIA YA MWENENDO WA SHAURI LA MADENI, deni linafunga endapo mdaiwa ATAKAIDI kulipa deni lake kulingana na hukumu,pia AMRI ya XXI kanuni ya 35(I) inaruhusu mdaiwa kukamatwa endapo atakiuka wito, MDAIWA WA BR@NCH Kamilisha Mkopo Wako Sasa Bila Shuruti KAMP NO:256699. "
" UMEKIUKA AGIZO lililokutaka ukamilishe marejesho yako BR@NCH Taasisi Ya mikopo imesikitishwa na Kitendo Hicho Tuhisi unadhulumu, Jukumu letu tumelitimiza Vizuri kukuhimiza ukamilishe malipo hatuta husika na madhara yatakayo jitokeza pindi mamlaka itakapo chukua hatua Kali Na stahiki dhidi yako Lipa Leo."
Kila siku wananitumia na kunipigia simu
Mkuu asante kwa mchango wako lakin lengo la uzi sio kutafuta kuonekana mwema, hapa tunajadili kwanini mtu akikopeshwa na mtu anayemuheshimu lakini harejeshi?
Unakuta ni rafiki wa karibu sana mnashibana lakini urafiki unaweza kufa kwa sababu ya fedha kwanini? Je tuache kusaidiana tunapokuwa na shida?

Mimi binafsi naogopa sana madeni na simkopi mtu kama sina ulazima na sikopi alaf nishindwe kurejesha, niko tayari hata kukopa salary advance nimlipe mdeni wangu asisononeke ili siku nyingine nikiwa na shida anikopeshe tena.

Nini maoni yako sasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za majukumu wakuu.

Pole na pilika za kutafuta maisha sambamba na kupambana na janga la Covid-19. Mungu ni mwema atatuvusha, tuendelee kuchukuwa tahadhari kujikinga na kuwakinga wenzetu.

Niende kwenye kiini cha mada yangu.

Kuna tabia flani imezuka au nisema labda ilikuwepo hata kwa watangulizi wetu (babu na bibi enzi hizo), unakuwa na rafiki ama ndugu yako mnashibana sana, mnasikilizana sana. Inatokea anapata shida au dharura, anakujia umkopeshe fedha kiasi flani aweze kutatua shida yake.

Kutokana na mnavyoheshimiana roho inakwambia sio vema uache kumsaidia rafiki yako au ndugu yako, unaingia ndani unakomba akiba yako kiduchu uliyokuwa nayo unampa kwa ahadi ya kurejesha baada ya siku mbili tatu let say anakwambia baada ya siku 2 atarudisha.

Unampa anashukuru sana anaondoka, sasa unakaa wiki mbili au mwezi au miezi kadhaa baadae hujapata mrejesho hata wa kuambiwa labda amekwama au mambo yalikwenda tofauti na alivyotarajia, yaani anakaa kimya tu, unamuona mitandaoni akipost mavitu kwa furaha tele, anasahau wewe ulijibana ukamuazima fedha ashughulikie shida iliyomkabili wakati ule.

Hebu wakuu tuelezane kiutu uzima hii tabia ya kitoto namna hii huwa inalenga nini? Kwamba marafiki tusisaidiane mwenzetu anapopata shida? Tabia kama hii inajenga picha gani na wewe unayekopeshwa na hurejeshi wala kutoa taarifa kwamba umekwama somewhere hii ni nini? Mambo ya kijinga kabisa.

Mtu anakukopa unamheshimu sana kiasi kwamba hata kumdai unaona aibu, lakini yeye kwa ujasiri mkubwa anakupotezea as if wewe huna shida na fedha.

Vijana wenzangu, wazee, mabibi na mabwana hebu tuache mambo ya ajabu, mtu utakuja kupata shida watu wanakukwepa maana una tabia ya kudhurumu kirahisi rahisi.

Najua mnanielewa, wewe mwenye tabia kama hii iache maana haina siha njema, watu tunaishi kwa kutegemeana, usilazimishe tuishi kwa kubaguana tukashindwa kusaidiana.

Tuendelee kunawa mikono kwa maji tiririka na tutumie vitakasi mikono vyenye alcohol isiyopungua 60%

Asanteni kwa kunielewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani inakera sana!
Mahusiano na ndugu yangu wa damu yamekufa baada ya kumkopesha fedha ili amalize chuo.
Calls zangu hapokei, SMS hajibu, fedha yangu hatumi na inaelekea mwaka wa pili sasa.
Pesa anayo na ana kazi yake inayomlipa vizuri tu.
Nimemua kuachana naye.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za majukumu wakuu.

Pole na pilika za kutafuta maisha sambamba na kupambana na janga la Covid-19. Mungu ni mwema atatuvusha, tuendelee kuchukuwa tahadhari kujikinga na kuwakinga wenzetu.

Niende kwenye kiini cha mada yangu.

Kuna tabia flani imezuka au nisema labda ilikuwepo hata kwa watangulizi wetu (babu na bibi enzi hizo), unakuwa na rafiki ama ndugu yako mnashibana sana, mnasikilizana sana. Inatokea anapata shida au dharura, anakujia umkopeshe fedha kiasi flani aweze kutatua shida yake.

Kutokana na mnavyoheshimiana roho inakwambia sio vema uache kumsaidia rafiki yako au ndugu yako, unaingia ndani unakomba akiba yako kiduchu uliyokuwa nayo unampa kwa ahadi ya kurejesha baada ya siku mbili tatu let say anakwambia baada ya siku 2 atarudisha.

Unampa anashukuru sana anaondoka, sasa unakaa wiki mbili au mwezi au miezi kadhaa baadae hujapata mrejesho hata wa kuambiwa labda amekwama au mambo yalikwenda tofauti na alivyotarajia, yaani anakaa kimya tu, unamuona mitandaoni akipost mavitu kwa furaha tele, anasahau wewe ulijibana ukamuazima fedha ashughulikie shida iliyomkabili wakati ule.

Hebu wakuu tuelezane kiutu uzima hii tabia ya kitoto namna hii huwa inalenga nini? Kwamba marafiki tusisaidiane mwenzetu anapopata shida? Tabia kama hii inajenga picha gani na wewe unayekopeshwa na hurejeshi wala kutoa taarifa kwamba umekwama somewhere hii ni nini? Mambo ya kijinga kabisa.

Mtu anakukopa unamheshimu sana kiasi kwamba hata kumdai unaona aibu, lakini yeye kwa ujasiri mkubwa anakupotezea as if wewe huna shida na fedha.

Vijana wenzangu, wazee, mabibi na mabwana hebu tuache mambo ya ajabu, mtu utakuja kupata shida watu wanakukwepa maana una tabia ya kudhurumu kirahisi rahisi.

Najua mnanielewa, wewe mwenye tabia kama hii iache maana haina siha njema, watu tunaishi kwa kutegemeana, usilazimishe tuishi kwa kubaguana tukashindwa kusaidiana.

Tuendelee kunawa mikono kwa maji tiririka na tutumie vitakasi mikono vyenye alcohol isiyopungua 60%

Asanteni kwa kunielewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi mdogo wangu wa damu alinikopa 1 milioni mwaka jana mwezi wa wa Julai akiahidi kunilipa kwenye mwezi wa Tisa, kwani atakuwa ameshachenjua mchanga wa madini.
Dogo alikata mawasiliano na mimi, kabla ya kumkopesha kila wiki ilikuwa lazima tujuliane hali, dogo akawa nikimpigia simu hapokei msg hajibu na biashara napata taarifa inaendelea vizuri.
Kabla ya Corona kuanza nikaambiwa na mdogo wetu mwingine wa pili kwamba mdeni wako amechenjua mchanga nakapata fedha milioni 22, kulipa hana nia kwani hapokei simu kabisa na mimi hatimaye nimemwachia Mungu na nimejifunza mtu yeyote yule sitamkopesha kiwango kikubwa ambacho hata kusamehe moyo unakuwa unaumia, huyu dogo nilimhurumia namna ambavyo biashara yake inayumba nikaenda kutoa hela yangu Karibia yote Airtel money nakutumia ili kuokoa jahazi.
Fedha fedha kwa wasio na hekima na kiasi kwao ni tanzi.
 
Yaani Mimi sasa hivi sikopeshi binadamu yeyote shenzi kabisa hata awe anakufa imenitokea sana yaani mtu unamkopesha anashukuru mnakubaliana siku ya kurudisha hela anapiga kimya dah inakera sana yaani wewe sasa unapoteza mda kumdai na kufatafata pengine na gharama zingine, sijawahi kutana na mkopaji mwaminifu 100% jibu ni moja SIKOPESHI, SINA ase mtu akakope kwenye taasisi za mikopo au benki, mimi walichonifanyia wadeni sina hamu nao Corona nae imepigilia msumari.
 
Habari za majukumu wakuu.

Pole na pilika za kutafuta maisha sambamba na kupambana na janga la Covid-19. Mungu ni mwema atatuvusha, tuendelee kuchukuwa tahadhari kujikinga na kuwakinga wenzetu.

Niende kwenye kiini cha mada yangu.

Kuna tabia flani imezuka au nisema labda ilikuwepo hata kwa watangulizi wetu (babu na bibi enzi hizo), unakuwa na rafiki ama ndugu yako mnashibana sana, mnasikilizana sana. Inatokea anapata shida au dharura, anakujia umkopeshe fedha kiasi flani aweze kutatua shida yake.

Kutokana na mnavyoheshimiana roho inakwambia sio vema uache kumsaidia rafiki yako au ndugu yako, unaingia ndani unakomba akiba yako kiduchu uliyokuwa nayo unampa kwa ahadi ya kurejesha baada ya siku mbili tatu let say anakwambia baada ya siku 2 atarudisha.

Unampa anashukuru sana anaondoka, sasa unakaa wiki mbili au mwezi au miezi kadhaa baadae hujapata mrejesho hata wa kuambiwa labda amekwama au mambo yalikwenda tofauti na alivyotarajia, yaani anakaa kimya tu, unamuona mitandaoni akipost mavitu kwa furaha tele, anasahau wewe ulijibana ukamuazima fedha ashughulikie shida iliyomkabili wakati ule.

Hebu wakuu tuelezane kiutu uzima hii tabia ya kitoto namna hii huwa inalenga nini? Kwamba marafiki tusisaidiane mwenzetu anapopata shida? Tabia kama hii inajenga picha gani na wewe unayekopeshwa na hurejeshi wala kutoa taarifa kwamba umekwama somewhere hii ni nini? Mambo ya kijinga kabisa.

Mtu anakukopa unamheshimu sana kiasi kwamba hata kumdai unaona aibu, lakini yeye kwa ujasiri mkubwa anakupotezea as if wewe huna shida na fedha.

Vijana wenzangu, wazee, mabibi na mabwana hebu tuache mambo ya ajabu, mtu utakuja kupata shida watu wanakukwepa maana una tabia ya kudhurumu kirahisi rahisi.

Najua mnanielewa, wewe mwenye tabia kama hii iache maana haina siha njema, watu tunaishi kwa kutegemeana, usilazimishe tuishi kwa kubaguana tukashindwa kusaidiana.

Tuendelee kunawa mikono kwa maji tiririka na tutumie vitakasi mikono vyenye alcohol isiyopungua 60%

Asanteni kwa kunielewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu watu wenye tabia hiyo ni wengi na ukija kufatilia unakuta wana madeni kila kona na wanakuwa wepesi sana kuanzisha urafiki na watu wapya ili waendeleze hiyo tabia kwa watu wengine

Mimi baada ya kuzungushwa sana hela yangu kwa muda mrefu ilibidi niende kumdai akiwa nyumbani kwake ili afedheheke vizuri

Pesa yangu niliipata na tokea siku hiyo
hatujatafutana tena,urafiki mwingine haunaga faida hata ukitoweka hujutii
 
Back
Top Bottom