Kufuru: Kikwete alitumia takribani Milioni 4 kwa siku moja hotelini Serengeti

MENGELENI KWETU

JF-Expert Member
May 8, 2013
9,549
24,159
Katika Gazeti la MwanaHalisi la leo kuna taarifa yenye kichwa cha habari KIKWETE KUFURU, kwamba wakati wa utawala wa JK kulikuwa na tabia ya kufuja pesa za walipa kodi kwa njia za FEDHEHA.

Katika moja ya safari chache za ndani ya Nchi mapema mwaka huu, ofisa mmoja wa Ikulu aliyekuwa kwenye msafara wa Rais alitumia pesa Tshs 821,997.24 kwa MASAJI peke yake (kukandwa na kutomaswa mwili) akiwa katika hotel ya kifahari iliyopo ndani ya mbuga ya Serengeti ya FOUR SEASONS SAFARI LODGE. Kiasi hicho cha pesa kililipwa na Ikulu.

Ofisa huyo wa Ikulu alifika Arusha akiwa katika msafara wa JK na kwenda moja kwa moja kwenye Hoteli hiyo kwa usiku mmoja na alikuwa katika chumba no 9017 na kwa ujumla kwa usiku huo mmoja gharama zote zilikuwa Tshs 3,862,997.24 zikiwa ni gharama za Masaji, Kufua Nguo, Kula, Kunywa na Kulala kwa usiku mmoja huo wa April 17.

Gharama za ufuaji wa nguo za ofisa huyo wa Ikulu pamoja na mwanamke aliyekuwa nae kwa siku hiyo jumla ni Tshs 676,000/=.
Gharama zote tajwa hapo juu zimelipwa na Ikulu.

Chanzi: MwanaHalisi la leo, Toleo 318.

My Take:
Awamu ya nne haikuwa na chembe ya huruma kwa wananchi wake.
 
Ngoja nilinunue nione hizo gharama za kukandwa na kutomaswa. Si angekandwa na kutomaswa na huyo mwanamke aliyekuwa naye?
 
Dingi yake ritz haki ya nani ni zimu. He is an ignorant person. He must answer all atrocities he committed. Huyu jamaa ni muuaji hana hata chembe ya huruma. Yani utafujaje hela ya wananch halaf unabaki kuchekacheka name mizahamizaha. He must pay back
 
Mlitaka liandike nini hilo gazeti?

NYUMBU nao wamo tu bila hata kuhoji! Kalala na mwanamke mwingine lakini alichohongwa anakijua KAHABA wa humu jf!!
 
Huyo Afsa wa ikulu ni yule Ngurumo aliyekuwa mnikulu au make ndo mwenye kufanana na upuuzi wote huu??!!
JK badala ya kumkalipia hapo usikute ndo kwaanza alianza kucheka cheka tuu!!
 
kwa matumizi ya rais na ujumbe wake hiyo mbona hela ndogo sana...kwa aina hiyo ya hotel..Mimi na familia yangu msimu huu wa sikuku tunalala hotel moja pale Bagamoyo kwa gharama za mara mbili ya hiyo
 
Hivi kwa nn mnaletaga topic za hilo jitu mmeshaharibu siku yangu km kuna mtu namchukia Mungu anisamehe ni huyo mliyemtaja sina hata haja kuandika jina lake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom