kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,255
- 16,185
Wanaotumia vituo vya mafuta ni wananchi, unapovifunga kwa wingi namna hii unalenga kuwaumiza watumiaji wa vituo hivyo zaidi kuliko wamiliki wake. Inakuwaje mtu asifikirie mateso yatakayowapata wananchi waliowengi badala ya kumuangalia mmiliki wa kituo tu? Bila shaka aliyetoa amri ya kufunga vituo hivyo anafahamu uwezo mdogo wa wananchi katika kuhoji,na kudai haki zao zinapovunjwa. Hivi hakuna njia nyingine za kuwafanya wenye vituo vya mafuta wafunge mashine za kutoa risiti bila kusababisha usumbufu kwa wananchi?