Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 8,971
- 6,919
Tile haziingizi maji. Wewe ulitegemea zifanye kazi ya waterproofing ambayo sio kazi yake. Hayo maji ni dalili kuwa kwenye sakafu ya chini/ zege kuna ufa na unapitisha maji kutoka kwenye udongo. Ondoa tiles sehemu husika ( kumbuka kuwa ufa unaweza kuwa mbali kidogo lakini maji yanapita sehemu ambayo grout imechoka. Ukishaona ufa, ziba halafu rudishia tiles. Weka upya grout ( siku hizi ziko ambazo ni waterproof) kote. Kama hayo maji yako bafuni, weka waterproofing kabla ya kuweka tiles. Zingatia pia kuwa kila baada ya miaka isiyozidi mitano karabati group.Hii nyuma nimejenga mwaka 2000 Kwa kufuata vigenzo vyote vya ufundi.
Nimeshangaa hizi mvua za mwaka kuna chumba nikiingia nakuta wet kuna majimaji, naagiza papigwe deki pakaushwe nikija tena nakuta wet majimaji hapo ndio sasa naamini maji yanatokea chini yanapenya taratibu kwenye tiles na Mimi sijajenga mabondeni, tatizo ni nini hapo na nifanyaje?
Amandla...