Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,813
- 59,393
Habarini great thinkers??
Kama ilivyo ada ya watu kwenda na fasheni ya nguo na viatu n.k ili wasipitwe na wakati ndivyo ilivyo kwa ndoa nyingi za sasa.Watu wanaoa na kuolewa mradi nao wajisikie/waonekane wako ndani ya ndoa.Wengi hawahangaiki kufikiri na kutafuta kile wanachotaka au hata kuvumilia mpaka watakapompata yule ambaye atawezana naye badala yake wanachukuana tu kisa eti muda unakimbia...fulani kashaolewa....matatizo yamezidi...marafiki wanamsema and so so!
Ni watu wachache sana hua wanakaa chini na kufukiria nini wanachotaka kwenye mahusiano kabla hawajaamua kua na mtu fulani.Mbaya zaidi ni wale wanaoingia kwenye ndoa bila uhakika wa nini wanachotaka na kama ndicho watakachopata!!
Hii inachochea sana ukosefu wa furaha na amani na uaminifu ndani ya ndoa kwasababu mtu anaingia akiwa hajui anataka nini alafu anachokuja kupata sicho... matokeo yake ndo watu wanatoka nje ya ndoa kutafuta maliwazo...watu wakuwasikiliza...watu wanaoweza kukaa nao chini wakaongea bila mtafaruku!Kwa kifupi wako watu wengi sana wanaotoka nje ya ndoa zao ni kwa vitu ambavyo ni vidogo sana ila vina umuhimu wake.
Ni wakati watu waanze kufikiria kabla ya kuomba mtu uchumba au kukubali kabla ya kuelekea ndoani.
Fikiria je unataka partner??Mtu unaeweza kushirikiana nae kwa hali na mali?Kama unataka mtu mtakaepeana mawazo na kushauriana katika level moja inabidi utafute mtu ambaye uwezo wenu wa kufikiria unaendana kwa kiasi fulani...Swala hapa sio kisomo cha darasani bali uwezo binafsi alionao mtu!!
Unamuoa mtu kwaajili ya kukuzalia watoto tu???Alafu akishazaa au akiwa uwezo huo hana??
Unakubali kuolewa ili kujipa uhakika wa kuishi(pesa)??Jiulize je siku zikiisha itakuaje???Kwanini usitafute mtu utakaempenda na mwenye uwezo?Better yet...kwanini usijishughulishe ukatengeneza vijisenti vyako ili usiwe tegemezi??
Ni uzuri wake ndo unaokuvutia???Iwe kwa mwanaume au mwanamke...siku huo uzuri ukipotea au kupungua utafanyaje??
Je ni pressure unayopata kutoka kwa ndugu na marafiki kwahiyo unamchukua tu aliye available kwa muda huo??Siku ukikutana na utakayempenda kwa dhati itakuaje??Kumbuka wao wanaokukumibiza kwenye ndoa sio watakaiishi hiyo ndoa!!
Kuna mengi sana ambayo yanapelekea watu kuoa/kuolewa bila kua na mapenzi ya dhati....vitu ambavyo vinaweza kupotea wakati wowote ule!!!Surelly hata mapenzi hua yanafifia kama maua yanavyonyauka yasipomwagiwa maji lakini angalau unajua kwamba ukiyajali na kuyapalilia yatachanua!!
Ushauri binafsi kwa kaka zangu na dada zangu mlio mbioni kuoa/kuolewa kueni makini na maamuzi yenu!Fikiria nini unataka kwenye hiyo ndoa na nini mwenzi wako anaweza kukupa!!
Mwisho....NI BORA KUA NA MIAKA 5 NDANI YA NDOA YENYE FURAHA badala ya 10 YENYE MASIKITIKO NA MANYANYASO....hivyo usikimbilie kwenye ndoa kama hujampata anaeuridhisha na kuufurahisha moyo wako.Ingia kwenye ndoa ukiwa na mapenzi na ubavu wako wa pili.....hapo inakua hata rahisi kuvumilia matatizo/makosa yake kuliko mtu usiyempenda.
Kila la heri kwa watarajiwa!!
Nawakilisha!!!
Kama ilivyo ada ya watu kwenda na fasheni ya nguo na viatu n.k ili wasipitwe na wakati ndivyo ilivyo kwa ndoa nyingi za sasa.Watu wanaoa na kuolewa mradi nao wajisikie/waonekane wako ndani ya ndoa.Wengi hawahangaiki kufikiri na kutafuta kile wanachotaka au hata kuvumilia mpaka watakapompata yule ambaye atawezana naye badala yake wanachukuana tu kisa eti muda unakimbia...fulani kashaolewa....matatizo yamezidi...marafiki wanamsema and so so!
Ni watu wachache sana hua wanakaa chini na kufukiria nini wanachotaka kwenye mahusiano kabla hawajaamua kua na mtu fulani.Mbaya zaidi ni wale wanaoingia kwenye ndoa bila uhakika wa nini wanachotaka na kama ndicho watakachopata!!
Hii inachochea sana ukosefu wa furaha na amani na uaminifu ndani ya ndoa kwasababu mtu anaingia akiwa hajui anataka nini alafu anachokuja kupata sicho... matokeo yake ndo watu wanatoka nje ya ndoa kutafuta maliwazo...watu wakuwasikiliza...watu wanaoweza kukaa nao chini wakaongea bila mtafaruku!Kwa kifupi wako watu wengi sana wanaotoka nje ya ndoa zao ni kwa vitu ambavyo ni vidogo sana ila vina umuhimu wake.
Ni wakati watu waanze kufikiria kabla ya kuomba mtu uchumba au kukubali kabla ya kuelekea ndoani.
Fikiria je unataka partner??Mtu unaeweza kushirikiana nae kwa hali na mali?Kama unataka mtu mtakaepeana mawazo na kushauriana katika level moja inabidi utafute mtu ambaye uwezo wenu wa kufikiria unaendana kwa kiasi fulani...Swala hapa sio kisomo cha darasani bali uwezo binafsi alionao mtu!!
Unamuoa mtu kwaajili ya kukuzalia watoto tu???Alafu akishazaa au akiwa uwezo huo hana??
Unakubali kuolewa ili kujipa uhakika wa kuishi(pesa)??Jiulize je siku zikiisha itakuaje???Kwanini usitafute mtu utakaempenda na mwenye uwezo?Better yet...kwanini usijishughulishe ukatengeneza vijisenti vyako ili usiwe tegemezi??
Ni uzuri wake ndo unaokuvutia???Iwe kwa mwanaume au mwanamke...siku huo uzuri ukipotea au kupungua utafanyaje??
Je ni pressure unayopata kutoka kwa ndugu na marafiki kwahiyo unamchukua tu aliye available kwa muda huo??Siku ukikutana na utakayempenda kwa dhati itakuaje??Kumbuka wao wanaokukumibiza kwenye ndoa sio watakaiishi hiyo ndoa!!
Kuna mengi sana ambayo yanapelekea watu kuoa/kuolewa bila kua na mapenzi ya dhati....vitu ambavyo vinaweza kupotea wakati wowote ule!!!Surelly hata mapenzi hua yanafifia kama maua yanavyonyauka yasipomwagiwa maji lakini angalau unajua kwamba ukiyajali na kuyapalilia yatachanua!!
Ushauri binafsi kwa kaka zangu na dada zangu mlio mbioni kuoa/kuolewa kueni makini na maamuzi yenu!Fikiria nini unataka kwenye hiyo ndoa na nini mwenzi wako anaweza kukupa!!
Mwisho....NI BORA KUA NA MIAKA 5 NDANI YA NDOA YENYE FURAHA badala ya 10 YENYE MASIKITIKO NA MANYANYASO....hivyo usikimbilie kwenye ndoa kama hujampata anaeuridhisha na kuufurahisha moyo wako.Ingia kwenye ndoa ukiwa na mapenzi na ubavu wako wa pili.....hapo inakua hata rahisi kuvumilia matatizo/makosa yake kuliko mtu usiyempenda.
Kila la heri kwa watarajiwa!!
Nawakilisha!!!