ulaya12
JF-Expert Member
- Nov 16, 2017
- 834
- 899
Nimekuelewa vizuri.Kufilisika kwa mabenki Tanzania ni kukua kwa uchumi au kuanguka kwa uchumi?, mjadala huu unaweza kutazamwa kwa namna yoyote kutokea upande wowote, lakini unaweza kuvurugika au kuimarika kama siasa na mihemko inaweza kutumika kujadili hili..
Mimi sio mtaalamu wa mambo ya uchumi, mimi tafsiri yangu ndogo ya kijinga hasa kwa mie mjinga mkuu mwerevu mkulima wa bamia Mbutu Kigamboni, huwa ni idadi ya milo yangu na waleti yangu inasomaje. Haijalishi utanipa siasa gani za uchumi, kama sijashiba milo yangu mitatu kwa siku na kuhakikisha kwa macho yangu ya nyama kwamba pochi yangu haina pesa ya ugoro, basi mie nitasimamia kwamba uchumi umeyumba.
Wiki ya mwisho, masaa ya mwisho na dakika za mwisho za Gavana Beno Ndulu zineshuhudiwa bank tano zinazotambuliwa na Bank kuu Tanzania zinatangazwa rasmi kufilisika na kwamba wateja wake watakwenda kulipwa amana za benki hizo pale Bot.
Baada ya miaka ya 90 Bank ya Meridian kufa baadae ikafa Bank ya Greenland, BOT walituhakikishia kwamba kuanzia wakati ule bank binafsi zitakuwa zinaweka Amana BOT na kila wakati watakuwa wanazikagua, Wateja wasiwe na wasiwasi na Amana zao, hii inamaana kama katika binki flani unapesa kiasi cha bilioni moja, benki hiyo ikifilisika, bilioni moja yako itarudishwa kwako kupitia Bot.
Leo hii Bot wasema kwamba Wateja wa Benki zilizofilisika watalipwa fedha zao na Bodi ya Bima ya Amana huku kiwango cha mwisho cha malipo kikitajwa kuwa ni shilingi Milioni 1.5 bila kujali mteja alikuwa na akiba ya shilingi ngapi? Huku wale wenye akiba ya chini ya shilingi Milioni 1.5 watalipwa zote.
Hii inamaana kwamba kama ulikuwa na milioni miatano katika akaunti yako basi jiandae kulipwa milioni 1.5. Na kama kuna mteja mwingine kwenye akaunti yake alikuwa na milioni moja tu, huyu atalipwa yote bila kuugulia maumivu
Ukweli mchungu ni kwamba Sera za nchi hubuniwa na huenezwa na chama, kisha chama hicho kikishinda uchaguzi kinaunda serikali ambayo inaanza maramoja kusimamia sera za chama hicho katika kutawala.
Kwa Tanzania sera za ccm ndizo zilishinda na ndi yenye sera zote, hivyo mambo yakiharibika au yakiwa mazuri sifa au lawama ni za ccm bila kukukwepesha sifa hizi,
Muhimu cha kujua benki hizi zimenguka kutokana sababu za mdodoro wa kiuchumi iwe Tanzania au dunia vyovyote watakavyotaka kujitetea watetezi wa sera, chama na serikali.
Mdororo huu unasababishwa na sera mbovu za uchumi. Ukosefu wa ajira na kupungua kwa uwekezaji.Hii imesababisha kuweka pesa benki (deposit) kupungu, mikopo kupungua na uwezo wa kulipa mikopo kutoweka. Haya ni ndani ya miaka miwili tu.
Nini kifanyike? Wanauchumi karibuni.....
NB: Wanasiasa uchwara mtupishe na omo zenu midomoni, tunajadili kitaaluma mambo haya.....
Na Yericko Nyerere
View attachment 668959