Mhabarishaji
JF-Expert Member
- Oct 5, 2010
- 1,006
- 598
Katika mila na desturi za Watanzania; ni ajabu kwa wanasiasa maarufu kuugua; na hata wakiugua, basi siyo magonjwa sugu kama UKIMWI. Ndiyo maana wakiugua, basi tunawaza haraka kwamba, huenda "wamepewa sumu".
Ingawa Watanzania wengi hatutaki kukubali hadharani, lakini ni dhahiri kwamba, wanasiasa wengi maarufu, wanaumwa magonjwa sugu; hususan UKIMWI. Jambo hili lilidhihirika, kutokana na jinsi wanasiasa hawa, kwa wingi wao; walivyomiminika kwenda Loliondo kwa Babu. Asikudanganye mtu! Watu wengi waliokwenda kwa Babu, kilichowavutia kwenda huko, ilikuwa tiba ya UKIMWI; na magonjwa yale mengine yaliyokuwa yanatajwa, yalikuwa ni danganya toto tu. Sasa tujiulize, kwa nini tunashindwa kuwa wazi kuhusu magonjwa ya wanasiasa maarufu?
Kama tunalipenda taifa letu, hatuna budi kuuacha utamaduni wetu huu. Tabia hii ya wanasiasa maarufu, kushindwa kuwa wazi kuhusu magonjwa yao, siyo tabia njema; itakuja kuliangamiza Taifa letu lote. Wanasiasa hawa, ni kioo cha jamii. Wakishindwa kuonesha mfano, ni vigumu kutarajia kwamba watu wengine, watamudu kuwa wazi kuhusu magonjwa yao.
Tujifunze kwa wenzetu, katika nchi ya Zimbabwe. Mwezi wa Juni, mwaka huu wa 2011; Makamu wa Waziri Mkuu wa Zimbabwe, Thokozani Khupe, alitangaza hadharani kwamba, ingawa bado ana nguvu ya kufanya kazi; hata hivyo anaumwa Saratani (Kansa) ya Matiti. Baada ya kauli hii, Spika wa Bunge la Zimbabwe, Lovemore Moyo; alimpongeza hadharani mwanamke huyu, na kumtaja kuwa ni mwanasiasa wa kuigwa; kwa jinsi alivyokuwa wazi, kuhusiana na ugonjwa unaomsibu.
Gazeti la Zimbabwe Standard la Oktoba 2 mwaka huu wa 2011; pia lilimnukuu Spika wa Bunge Moyo, akisema jana yake hadharani kwamba, wabunge wengi wa Bunge la Zimbabwe, wana UKIMWI, na baadhi yao wamefiwa na wenzi wao (waume/wake zao); kutokana na UKIMWI.
Kabla ya hapo, mwezi wa Septemba, mwaka huu wa 2011; Rais Robert Mugabe, yeye naye; alisema kwamba anawajua Viongozi wengi wa juu wa Serikali, wenye virusi vya HIV, ambao wanatumia ARV's (dawa za kurefusha maisha). Akasema kwamba, pamoja na kwamba viongozi hawa wameathirika, bado wanawaambukiza UKIMWI, watu wengine; bila kujali. Akawaonya wasifanye hivyo, ili kulinusuru taifa hilo lenye waathirika wengi wa UKIMWI.
Katika hatua nyingine, mwezi wa Juni, mwaka huu wa 2011; Mwandishi wa kike wa Gazeti la B-Metro, Simiso Mlevu; alimpeleka mahakamani, Mbunge wa Bulawayo-Insiza, Siyabonga Ncube (MDC-N); kwa kumwambukiza UKIMWI, huku akijua kwamba anao. Simiso alidai kwamba, amekuwa ni rafiki yake Ncube, kwa miaka miwili; baada ya mkewe kufariki. Aliendelea kusema kwamba ingawa Ncube alimficha, hata hivyo, alikuja kuthibitisha baadaye kwamba; mkewe Ncube alifariki kutokana na UKIMWI.
Huo ndiyo uwazi uliopo kwa watu wa nchi ya Zimbabwe, wanajua kwamba hata wanasiasa maarufu wanaweza kuugua magonjwa sugu, na hata UKIMWI. Hivyo sivyo ilivyo kwetu Watanzania. Kwetu sisi, wanasiasa maarufu wakiugua, wanakuwa "wamepewa sumu". Tumefikia mahali pa kudanganyana kwamba, mwanasiasa fulani amepelekwa India, kwa sababu ya vijidudu 150 vya Malaria. Je, uongo huu ni kwa faida ya Taifa letu? Na je, wanasiasa wanaposhindwa kuwa wazi juu ya magonjwa yanayowasibu; TANZANIA ISIYO NA UKIMWI, KWELI INAWEZEKANA? Katika nchi yetu, eti UKIMWI ni maradhi ya walalahoi tu, lakini wanasiasa maarufu, wao, hawawezi kuwa nao. Tunamdanganya nani? TUTAFAKARI!
Ingawa Watanzania wengi hatutaki kukubali hadharani, lakini ni dhahiri kwamba, wanasiasa wengi maarufu, wanaumwa magonjwa sugu; hususan UKIMWI. Jambo hili lilidhihirika, kutokana na jinsi wanasiasa hawa, kwa wingi wao; walivyomiminika kwenda Loliondo kwa Babu. Asikudanganye mtu! Watu wengi waliokwenda kwa Babu, kilichowavutia kwenda huko, ilikuwa tiba ya UKIMWI; na magonjwa yale mengine yaliyokuwa yanatajwa, yalikuwa ni danganya toto tu. Sasa tujiulize, kwa nini tunashindwa kuwa wazi kuhusu magonjwa ya wanasiasa maarufu?
Kama tunalipenda taifa letu, hatuna budi kuuacha utamaduni wetu huu. Tabia hii ya wanasiasa maarufu, kushindwa kuwa wazi kuhusu magonjwa yao, siyo tabia njema; itakuja kuliangamiza Taifa letu lote. Wanasiasa hawa, ni kioo cha jamii. Wakishindwa kuonesha mfano, ni vigumu kutarajia kwamba watu wengine, watamudu kuwa wazi kuhusu magonjwa yao.
Tujifunze kwa wenzetu, katika nchi ya Zimbabwe. Mwezi wa Juni, mwaka huu wa 2011; Makamu wa Waziri Mkuu wa Zimbabwe, Thokozani Khupe, alitangaza hadharani kwamba, ingawa bado ana nguvu ya kufanya kazi; hata hivyo anaumwa Saratani (Kansa) ya Matiti. Baada ya kauli hii, Spika wa Bunge la Zimbabwe, Lovemore Moyo; alimpongeza hadharani mwanamke huyu, na kumtaja kuwa ni mwanasiasa wa kuigwa; kwa jinsi alivyokuwa wazi, kuhusiana na ugonjwa unaomsibu.
Gazeti la Zimbabwe Standard la Oktoba 2 mwaka huu wa 2011; pia lilimnukuu Spika wa Bunge Moyo, akisema jana yake hadharani kwamba, wabunge wengi wa Bunge la Zimbabwe, wana UKIMWI, na baadhi yao wamefiwa na wenzi wao (waume/wake zao); kutokana na UKIMWI.
Kabla ya hapo, mwezi wa Septemba, mwaka huu wa 2011; Rais Robert Mugabe, yeye naye; alisema kwamba anawajua Viongozi wengi wa juu wa Serikali, wenye virusi vya HIV, ambao wanatumia ARV's (dawa za kurefusha maisha). Akasema kwamba, pamoja na kwamba viongozi hawa wameathirika, bado wanawaambukiza UKIMWI, watu wengine; bila kujali. Akawaonya wasifanye hivyo, ili kulinusuru taifa hilo lenye waathirika wengi wa UKIMWI.
Katika hatua nyingine, mwezi wa Juni, mwaka huu wa 2011; Mwandishi wa kike wa Gazeti la B-Metro, Simiso Mlevu; alimpeleka mahakamani, Mbunge wa Bulawayo-Insiza, Siyabonga Ncube (MDC-N); kwa kumwambukiza UKIMWI, huku akijua kwamba anao. Simiso alidai kwamba, amekuwa ni rafiki yake Ncube, kwa miaka miwili; baada ya mkewe kufariki. Aliendelea kusema kwamba ingawa Ncube alimficha, hata hivyo, alikuja kuthibitisha baadaye kwamba; mkewe Ncube alifariki kutokana na UKIMWI.
Huo ndiyo uwazi uliopo kwa watu wa nchi ya Zimbabwe, wanajua kwamba hata wanasiasa maarufu wanaweza kuugua magonjwa sugu, na hata UKIMWI. Hivyo sivyo ilivyo kwetu Watanzania. Kwetu sisi, wanasiasa maarufu wakiugua, wanakuwa "wamepewa sumu". Tumefikia mahali pa kudanganyana kwamba, mwanasiasa fulani amepelekwa India, kwa sababu ya vijidudu 150 vya Malaria. Je, uongo huu ni kwa faida ya Taifa letu? Na je, wanasiasa wanaposhindwa kuwa wazi juu ya magonjwa yanayowasibu; TANZANIA ISIYO NA UKIMWI, KWELI INAWEZEKANA? Katika nchi yetu, eti UKIMWI ni maradhi ya walalahoi tu, lakini wanasiasa maarufu, wao, hawawezi kuwa nao. Tunamdanganya nani? TUTAFAKARI!