Jana nikiwa napita maeneo ya Ubungo na family yangu, mwanangu mwenye umri wa miaka 6 aliliona jengo la TANESCO na maandishi makubwa "TANESCO" akaniuliza: "Baba, kumbe pale ndio TANESCO?" Nikamwambia: Ndio, pale ni makao makuu ya TANESCO" Akaendelea: "Kwa hiyo pale ndio wanapokata umeme?". Nikacheka sana. Kwa hiyo yeye kwa mtazamo wake kazi ya TANESCO ni kukata umeme na sio kuzalisha umeme. Bila shaka fikra hizi zimejengeka kutokana na kusikia watu wakiwalalamikia TANESCO kwa kukata umeme mara kwa mara.