Jana jioni nilibahatika kujichomeka katikati ya baadhi ya wajumbe wa kamati ya ushindi hapa Shinyanga mjini, kwa kweli wanatia huruma!
Hawakuficha kusema ukweli kwamba hali ya chama ni mbaya mno kwa ujumla, si kwa madiwani si kwa mbunge na pia kwa Rais!
Wajumbe hao wamefikia hatua ya kuulaumu uongozi wa juu kwa kumkata Lowassa!
Tegemeo lao kubwa lilikuwa vijiji vya pembezoni lakini hali ni tofauti na walivyofikria, raia wana hamasa ya kiwango cha juu sana cha mabadiliko!