Kucheleweshwa kutolewa ruling ya kesi yangu

Kimali

Member
Oct 25, 2011
26
8
Mimi ni mtumishi wa umma wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nina kesi ya jinai inayonikabili tangu mwaka 2007, ambapo ushahidi wake ulifungwa tangu tarehe 12.06.2011, na kinachosubiriwa ni kutolewa 'ruling' kuwa nina kesi ya kujibu au la, lakini hadi leo October 27, 2011 mahakama haijatoa uamuzi huo. Je katika hatua hii nitumie mbinu gani ili niweze kupata haki yangu mapema kwa sababu hata kesi yenyewe nilibambikiziwa na mbunge wangu. Naombeni msaada wa kisheria wa jinsi ya kuilazimisha mahakama itoe 'ruling' ya kesi hii. Nilisimamishwa kazi tangu waka 2007 hadi leo ninakula nusu mshahara na familia inateseka sana jameni kutokana na kesi jinai .
 
Pole sana natumaini wajuzi wa sheria watakusaidia labda ulipo waulizia wahusika kwanini wanachelewa walisemaje?
 
Mara ya mwisho uliambiwa nini mahakamani?ulipewa tarehe ya kurudi mahakamani?jaribu kwenda kwa karani wa huyo hakimu anayesikiliza kesi yako halafu muulizie kama ulipangiwa tarehe nyngne?
N.B
Kama umeshapangiwa tarehe ya kurudi mahakamani tulia mpaka hyo tarehe.
 
Kweli hapo rafiki huna jinsi mpaka siku ambayo walikupangia kwenda, ila nimeshituka kusikia kwamba unalipwa nusu mshara kama ulivyoseme kwenye ujumbe wako "........ Nilisimamishwa kazi tangu waka 2007 hadi leo ninakula nusu mshahara na familia inateseka sana jameni kutokana na kesi jinai."

Kama wewe ni mtumishi wa serikali ambeye haupo kwenye makundi haya; Jeshi la Wananchi, Polisi, Magereza na JKT kwa mujibu wa Sheria ya Kazi Section 2 (1) basi sheria inasema unapaswa kulipwa mshara kamili kama Mwajiri amekusimamisha kazi (suspension) kwa ajiri ya uchuguzi wa hiyo kesi yako ya jinai. Soma Rule 27 of G.N.No 42, pia mwajiri hapaswi kukufukuza au kukupa adhabu yoyote ya kinidhamu kwa sababu ya kesi hiyo mpaka itapoisha soma Section 37 (5)

 
Nawashukuruni wote mliyonipa wawazo nitayazingatia na endapo nitakwama nitaomba tena msaada wenu baadaye
 
Back
Top Bottom