Kuchelewa maisha

Kuchelewa maisha

Mung Chris

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2017
Posts
3,438
Reaction score
3,951
Hakuna MWANAUME Aliyechelewa Maisha Wala Hakuna Mwanaume Aliyewahi Maisha kila Mmoja Ana Nafasi Ya Kuwa Bora Cha Msingi Ni Kupeana Heshima Na kupeana Moyo.

woman.jpg
 
Maisha hayana SI unit wala hayana Script..
Ukisema umewahi/ umechelewa maisha unatumia kipimo gani? Mfano, Kama muda wa kufika ofisini ni saa 2 asubuhi, nikifika saa mbili nanusu asubuhi nitasema nimechelewa and vice versa is true. Sasa kwenye maisha hakuna kipimo kama hiko.

Hii nadharia ya kuwahi/ kuchelewa maisha ndo inawafanya vijana wengi watumie shortcuts, ambazo mwisho wa siku zinakuja kuwagharimu sana.

Wito wangu, kila mmoja apambane na hali yake...work hard lakini usijilinganishe na mtu. Stick in your lane!
 
Hakuna MWANAUME Aliyechelewa Maisha Wala Hakuna Mwanaume Aliyewahi Maisha kila Mmoja Ana Nafasi Ya Kuwa Bora Cha Msingi Ni Kupeana Heshima Na kupeana Moyo.

View attachment 1167906
Hapana kaka kupo.... Kuna hard workers ambao tayari at 40 wameshapata muelekeo wa maisha halafu kuna ambao jua linawachwea Lakini hawana hata kibanda
 
Hakuna MWANAUME Aliyechelewa Maisha Wala Hakuna Mwanaume Aliyewahi Maisha kila Mmoja Ana Nafasi Ya Kuwa Bora Cha Msingi Ni Kupeana Heshima Na kupeana Moyo.

View attachment 1167906
Kuchelewa kupo mkuu...kwa mfano, kuna ma-agemate wako uliokuwa nao utotoni, wana familia, wanamaisha mazuri, wana amani na ndoa zao,...Lakini wewe (mfano unaendelea) huna mbele wala nyuma, huna hata geto la kupanga (unaishi kwa ndugu au kwenu), kama kuna watu ulisoma nao wao wana masters na ma-phd wewe una diploma, mdogo wako wa nne kukufata ana watoto watatu wewe hata mmoja huna na hapo we sio mgumba wala tasa..hapo utasema bado hujachelewa...ni mifano tu mkuu sipingani na hoja yako
 
Tofautisha kati ya maisha na vitu
Kuchelewa kupo mkuu...kwa mfano, kuna ma-agemate wako uliokuwa nao utotoni, wana familia, wanamaisha mazuri, wana amani na ndoa zao,...Lakini wewe (mfano unaendelea) huna mbele wala nyuma, huna hata geto la kupanga (unaishi kwa ndugu au kwenu), kama kuna watu ulisoma nao wao wana masters na ma-phd wewe una diploma, mdogo wako wa nne kukufata ana watoto watatu wewe hata mmoja huna na hapo we sio mgumba wala tasa..hapo utasema bado hujachelewa...ni mifano tu mkuu sipingani na hoja yako
 
Kila mtu ana maana yake hukusu maisha, sasa unaposema unachelewa au unawahi maisha ni vigumu ku generalize... mwingine kuwahi maisha ni kuzaa na watoto 9 hadi 12 kabla ya kufika umri wa miaka 40.

Mwingine kuwahi maisha ni kuoa wanawake zaidi ya 2 akiwa na umri wa chini miaka 26, Mwingine kuwahi maisha ni kujenga kabla ya kufikisha umri wa kustaafu yaani 60.

Maisha hayana kanuni.....
 
Hapana kaka kupo.... Kuna hard workers ambao tayari at 40 wameshapata muelekeo wa maisha halafu kuna ambao jua linawachwea Lakini hawana hata kibanda
kwamba above 40 hawezi kujenga,,!? Au unamaanisha nini kaka mkuu Mshana Jr
 
Nikisimama kiimani zaidi hakuna kuchelewa wala kuwahi,kwasababu Biblia inasema "kila jambo kwa wakati wake na majira yake chini ya jua" hivyo aliye oa/olewa juzi/jana muda wake na majira yake yalitimilika hivyo wewe ambaye bado usilazimishe "majira"😄muda sahihi ukifika wala hutotumia nguvu utaona tuu kila kitu kinajipanga chenyewe mpaka unajiuliza huu ni muujiza ama....!!!

Japo subira ni ngumu lakini ina malipo,.tuwe na imani na tumaini huku tukijituma kwa dhati.
 
Kila mtu ana maana yake hukusu maisha, sasa unaposema unachelewa au unawahi maisha ni vigumu ku generalize... mwingine kuwahi maisha ni kuzaa na watoto 9 hadi 12 kabla ya kufika umri wa miaka 40.

Mwingine kuwahi maisha ni kuoa wanawake zaidi ya 2 akiwa na umri wa chini miaka 26, Mwingine kuwahi maisha ni kujenga kabla ya kufikisha umri wa kustaafu yaani 60.

Maisha hayana kanuni.....
🤝
 
Kila mtu ana kipaumbele chake,mwingine kuoa,mwingine kuwekeza ,mwingine starehe za pombe na madem ...
 
Kuchelewa kupo wala tusibishane kuhusu hilo sana Wakuu
 
Kuchelewa kupo wala tusibishane kuhusu hilo sana Wakuu
 
Back
Top Bottom