Kubadilisha umiliki(ownership) wa gari TRA

Kubadilisha umiliki(ownership) wa gari TRA

Paul Mchumi

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2013
Posts
1,040
Reaction score
1,273
Habari wana Jf
Nahtaji kubadilisha umiliki wa gari yangu toka kwa mhusika nilienunua toka kwake,tatizo lililopo ni kuwa sina kitambulisho cha yule alieniuzia(first owner),ila nina mkataba tu ambao tulisainishana kwa mwanasheria!
Naomba msaada wa maelekezo kipi cha kufanya kwa anaejua!
 
Sasa si ungewauliza hao walokwambia upeleke kitambulisho cha alokuuzia?
Waulize mbadala wake nini kifanyike iwapo huna namna ya kupata copy ya hicho kitambulisho?
Je Card ya Gari unayo?
 
Habari wana Jf
Nahtaji kubadilisha umiliki wa gari yangu toka kwa mhusika nilienunua toka kwake,tatizo lililopo ni kuwa sina kitambulisho cha yule alieniuzia(first owner),ila nina mkataba tu ambao tulisainishana kwa mwanasheria!
Naomba msaada wa maelekezo kipi cha kufanya kwa anaejua!
Nenda TRA na barua ya makabidhiano/mauziano,kadi ya Gari pamoja na (kama sikosei asilimia moja)ya pesa ulionunulia!
Binafsi nina hilo tatizo pia maana nilienunua kwake siye mmiliki halali.
 
Yap mkataba wa mauzo ambao ndani Yake kuna thamani ya bei ya mauziano ambapo atalipia 1% ya thamani ya bei ya mauzo kama ushuru wa stamp pamoja na transfer fee ya TShs . 60,000/-
Halafu Kwenye ile card Yule muuzaji anatakiwa kusaini Kwenye sehemu Yake !
NB: yakupasa kuwa na TIN ktk kukamilisha huo umiliki wa Gari !
 
Yap mkataba wa mauzo ambao ndani Yake kuna thamani ya bei ya mauziano ambapo atalipia 1% ya thamani ya bei ya mauzo kama ushuru wa stamp pamoja na transfer fee ya TShs . 60,000/-
Halafu Kwenye ile card Yule muuzaji anatakiwa kusaini Kwenye sehemu Yake !
NB: yakupasa kuwa na TIN ktk kukamilisha huo umiliki wa Gari !
transfer fee imefika 60 elfu? ilikuwa elfu 10
 
Hivi kama una kila kitu kwa maana ya mkataba wa kisheria, kadi halisi ya gari...ila kitambulisho cha Muuzaji ndio huna...bado naweza kufanya transfer?
 
Hivi kama una kila kitu kwa maana ya mkataba wa kisheria, kadi halisi ya gari...ila kitambulisho cha Muuzaji ndio huna...bado naweza kufanya transfer?
Nenda TRA watakuelekeza.
 
Yap mkataba wa mauzo ambao ndani Yake kuna thamani ya bei ya mauziano ambapo atalipia 1% ya thamani ya bei ya mauzo kama ushuru wa stamp pamoja na transfer fee ya TShs . 60,000/-
Halafu Kwenye ile card Yule muuzaji anatakiwa kusaini Kwenye sehemu Yake !
NB: yakupasa kuwa na TIN ktk kukamilisha huo umiliki wa Gari !
Kama kadi imelaminatiwa inakuaje
 
Mku
Sasa si ungewauliza hao walokwambia upeleke kitambulisho cha alokuuzia?
Waulize mbadala wake nini kifanyike iwapo huna namna ya kupata copy ya hicho kitambulisho?
Je Card ya Gari unayo?
Mkuu umesema vizuri maana vipi kama aliekuuzia Gari Alisha kufa?
 
Sasa si ungewauliza hao walokwambia upeleke kitambulisho cha alokuuzia?
Waulize mbadala wake nini kifanyike iwapo huna namna ya kupata copy ya hicho kitambulisho?
Je Card ya Gari unayo?
Kama hana kitambulisho amuone wakili aandikiwe kiapo, kinaitwa 'affidavit regarding nknown whereabouts of the seller'.
 
Mku

Mkuu umesema vizuri maana vipi kama aliekuuzia Gari Alisha kufa?


Hapo shughuli huwa pevu kidogo.

Inabidi msimamizi wa mirathi afuatilie yeye kwa niaba ya marehemu na uwepo ushahidi wa kifo na jinsi msimamizi alivyopatikana
 
Je kama mnunuzi anataka kujua kama gari analotaka kununua halina matatizo atajuaje? Ilikuweza kifahamu mapema kabla ya ununuzi...Na je kama litakuwa na shida wakati wa transfer wanafanyaje?
 
Je kama mnunuzi anataka kujua kama gari analotaka kununua halina matatizo atajuaje? Ilikuweza kifahamu mapema kabla ya ununuzi...Na je kama litakuwa na shida wakati wa transfer wanafanyaje?


Matatizo gani kwa mfano?
 
Back
Top Bottom