mmmuhumba
JF-Expert Member
- Nov 8, 2017
- 491
- 476
Kauli hii ni kauli inayonichanganya sana. Mimi ni msichana, nimekuwa na mahusiano na mpenzi wangu sasa inapata miaka miwili na hakuna siku ambayo ameshawahi nikataza kushika simu yake na wala kunitenga kwa namna moja ama nyingine.
Nimeshangaa na ninaumia leo ni siku ya nane, tangu siku niliyoamka asubuhi na kuangalia simu yangu na kukutana na ujumbe wa mpenzi wangu akisema hataki nimtumie ujumbe wala kupigia simu.
Sikuwa tayari kuipokea hii kauli, nilipompigia simu yangu pia ilikata bila kuita ikiandika “User busy” ikimaanisha ni wazi pia 'ameniblok', nimejaribu kutuma ujumbe ila hata moja sijajibiwa.
Ninaumia sana kwakuwa sijui lipi ni kosa langu mpaka yeye kufikia kufanya maamuzi haya, ni bora basi angeniambia nina kosa hili na lile nami ningekuwa tayari kuishi atakavyo.
Hivi kweli kwa kuishi vyema mimi naye na ghafla tu anabadilika kama mimi ni adui kwake, vipi kuhusu ahadi yake kwangu na vipi maisha yangu niliyomuamini na kumtambulisha kwa baadhi ya ndugu zangu na marafiki zangu ooh Mungu nipe nguvu ya kuikabili hii hali.
Nilijaribu kuazima simu ya rafiki yangu na kumpigia lakini aliposikia tu sauti yangu alikata na kuzuia namba ile pia. Kwanini asiniweke wazi mimi nilichomkosea nikawa huru katika hii Dunia? Ni ipi kasoro yangu katika mapenzi ikiwa alinisifia kuwa mimi ni bora kwake kuliko X zake wanne?
Natamanai kuyaanza maisha mapya lakini nakosa amani ninapowaza kwanini ameniacha bila kuniambia makosa yangu. Kwanini ? Kwanini mpenzi?
Nimeshangaa na ninaumia leo ni siku ya nane, tangu siku niliyoamka asubuhi na kuangalia simu yangu na kukutana na ujumbe wa mpenzi wangu akisema hataki nimtumie ujumbe wala kupigia simu.
Sikuwa tayari kuipokea hii kauli, nilipompigia simu yangu pia ilikata bila kuita ikiandika “User busy” ikimaanisha ni wazi pia 'ameniblok', nimejaribu kutuma ujumbe ila hata moja sijajibiwa.
Ninaumia sana kwakuwa sijui lipi ni kosa langu mpaka yeye kufikia kufanya maamuzi haya, ni bora basi angeniambia nina kosa hili na lile nami ningekuwa tayari kuishi atakavyo.
Hivi kweli kwa kuishi vyema mimi naye na ghafla tu anabadilika kama mimi ni adui kwake, vipi kuhusu ahadi yake kwangu na vipi maisha yangu niliyomuamini na kumtambulisha kwa baadhi ya ndugu zangu na marafiki zangu ooh Mungu nipe nguvu ya kuikabili hii hali.
Nilijaribu kuazima simu ya rafiki yangu na kumpigia lakini aliposikia tu sauti yangu alikata na kuzuia namba ile pia. Kwanini asiniweke wazi mimi nilichomkosea nikawa huru katika hii Dunia? Ni ipi kasoro yangu katika mapenzi ikiwa alinisifia kuwa mimi ni bora kwake kuliko X zake wanne?
Natamanai kuyaanza maisha mapya lakini nakosa amani ninapowaza kwanini ameniacha bila kuniambia makosa yangu. Kwanini ? Kwanini mpenzi?