Kuagiza gari Vs kununua yadi hapa bongo

Kuagiza gari Vs kununua yadi hapa bongo

Samahani ivi nikiwa mil 4 naweza pata gari
wapi sasa yadi au nje


south wapata gari nzuri maxmum milion saba mpaka meli ya kuja nayo

mtihani ni kodi

gari ni bei rahisi sana uwezi amini ukiwa na dola ishilini wapata carry used safi tu na haija tumikag sana

mi nakumbuka niki kuja na marck x na hypsam kwa 14m pamoja na meli

ila shughuli ilikua bandalini
 
Hii gari ukiinunua haitaka dumu mwezi kama haijaanza kuchoka! Tafuta jina lingine tofauti

mbona ndio zinatumika kama za kubeba abiria commercial hizi Noah, tena mikoani kwenye rough roads? Nilidhani ni kwa sababu zinavumilia vipigo
 
Mi nahitaji gari aina ya TOYOTA-BB.....Ntaipata wapi hapa Bongo.
 
Mkuu kununua gari Japan inakuwa nafuu kuliko hapa. Sababu zipo rahisi na unachagua unayoipenda, pia ina ubora kuliko kununua hapa mtu anakuuzia gari ina matatizo lukuki. Lakini angalia mfuko wako kama unaweza kununua Japan au kununua hapa hapa nyumbani.
Upo sahihi
Lakini kuna hawa TRA ambao kwa sasa wanajifanya kukusanya kodi.
 
Naomba kwa wenye uzoefu wa kununua magari, kununua kwa kuagiza nje/japan na kununua hapa bongo yadi ipi nafuu?
Kwa kifupi nunua gari hapa nchini si lazima show room hata kwa ntu
Tafuta fundi anayejua hasa aina ya gari unayotaka kununua.
Gari ni chuma tu,kikitunzwa hakina taabu..kuna magari ya toka miaka ya sitini mpaka sasa yanadunda.
 
Magari mengi tunayonunua toka nje ni used. Kuna yadi zinanunua magari mitaani na kuyaweka kwenye yadi.

Sasa ukinunua Bongo inakuwa used mara mbili. Lazima litakuwa limechoka sana.

Agiza mwenyewe huko Japan. Ubora wa gari unategemea kampuni ulikoagiza. Kwa ujumla, magari ya Autorec huwa na kiwango kizuri zaidi. Japanese Vehicles wanafuatia. Siku hizi kuna Be Forward. Sina uzoefu sana nao lakini nasikia ni kama bahati nasibu fulani. Unaweza gari nzuri sana au mbovu mbovu. Ni maoni yangu wakuu.
 
Back
Top Bottom