Nyakwaratony
JF-Expert Member
- Dec 21, 2011
- 573
- 140
Hali zenu wanaMMU?
Miaka kadhaa iliyopita nilikuwa nafanya kazi katika Ofisi fulani hapa DODOMA alitokea baba mmoja akawa mteja wetu mzuri kiasi kwamba hawezi kumaliza siku mbili hajaja kufanya kazi zake. Hata kama hana kazi ya kufanya alipita kutusalimia. Yule baba alinipenda sana "Sio kimapenzi tafadhali" kwani nilikuwa namfanyia kazi zake vizuri.
Baada ya muda fulani alitaka kujua historia ya maisha yangu. Nilimueleza bila kuficha chochote, alisikitika akaniuliza kwanini nilikatisha masomo. Lakini baadaye alinisihi sana nirudi shule, ingawa sikuwa na uwezo kwa kurudi alinihaidi kunigharamia kila kitu. Nilirudi shule ila kabla sijamaliza kusoma hiyo elimu ya sekondari alipata uhamisho wa kikazi akahamia mkoani MOROGORO.
Hilo halikuwa mwisho wa ufadhili wake, tuliendelea kuwasiliana mpaka nikamaliza kidato cha nne. Baadae nilipata kazi nzuri nikawa na uwezo wa kuendelea na chuo kwa ngazi ya cheti. Lakini msaada wake haukuishia hapo. Aliendelea kunigharamia nusu ya ada na mimi nikawa namalizia nusu iliyobaki mpaka nikamaliza chuo ngazi ya cheti.
Aliniambia ana watoto kadhaa wakiume na wakike mmoja. Alinikaribisha kwake ambapo alikuwa akiishi na housegirl tu. Mkewe alikuwa akiishi DSM kikazi. Baada ya kuhamia mkoani Morogoro Kuna mwezi fulani nilipata likizo nikaenda kumsalimia, wanawe wawili pia walikuwa wanasoma mkoani hapo. Weekend moja alinikaribisha kwake kumbe siku hiyo pia alikuwa amewaita wanawe. Alinitambulisha kwao na kuwaeleza uhusiano baina yetu bila kuficha chochote.
Wanawe walinipokea kama mmoja wa familia, tulikaa nao pale kama watoto wa familia moja kwa muda kama wa wiki kwani nao walikuwa likizo, baada ya wiki mwanaye mkubwa aliondoka na kwenda kwa mama yake DSM, kwa vile nami nilikuwa na safari ya kwenda BAGAMOYO niliona sio vyema nipite DSM bila kwenda kumsalimia mama "mke wa yule baba" Nilianza safari mpaka DSM nilipofika sikumkuta yule mwanae kwani alikwenda MKURANGA.
Yule mama alikuwa na taarifa ya ujio wangu pale kwake. Nilifika mida ya jioni alinipokea na akafurahi kuniona kwani alikuwa akinisikia kupitia kwa mmewe na watoto. Nilillala pale kwa siku moja, kesho yake niliaga na kuondoka kwenda BAGAMOYO ili nimalizie likizo yangu na kurudi mapema kazini. Nilichelewa kutoka Bagamoyo make nilikaa kwa muda wa siku kadhaa. Nilipitiliza mpaka MORO nikaenda nikamuaga baba yangu mlezi na kurudi kazini DOM.
Maisha yaliendelea vizuri na undugu baina yangu na ile familia ulidumu, hata mwanawe yule baba aliwahi kuja kwangu yeye pamoja na mwanaye wakakaa kama wiki hivi. Baada ya mwaka hivi yule baba akafiwa na mama yake mzazi yaani bibi mlezi. Alinitaarifu kuwa "Bibi yako amefariki Mkoani Tabora hivyo mimi na mdogo wako tupo njiani kuelekea msibani. Mama yeye alitangulia.
Hapo nilijiongeza nami nikajiandaa kesho yake kuelekea msibani Tabora. Niliomba ruksa kazini nikaondoka kuelekea msibani. Tangu mwanzo wa safari nilikuwa nawasiliana na yule dada bintiye baba yangu mlezi. Mpaka nafika stendi ya TABORA nilikuwa nawasiliana na yule dada ili anipe maelekezo ya mahali msiba upo.
Nilipoteremka garini nilipigiwa simu na yule dada, nilipokea ili nipate maelekezo namna ya kufika msibani. Lahaula!!!! Nilisikia sauti tofauti na ya yule dada mara nikagundua ni sauti ya mama mkewe baba mlezi ikiniuliza kwa ukali "UNAKWENDA WAPI WEWE"?? Nikamjibu nakuja msibani mama. Akaniuliza "NANI KAKUPA TAARIFA YA MSIBA"?? Nikamjibu baba ndiye kanipa taaarifa.
Alisema maneno makali na machache "NISIKUONE KATIKA USO WANGU, NITAKUCHAFUA SURA YAKO" Nilihisi kuchanganyikiwa nisijue la kufanya ukizingatia nilikuwa mgeni Tabora. Nilitafuta mahali nikaenda kupumzika nikitafakari ni nini kosa langu. Baada ya muda nafikiri baba alitaka kujua nimefika wapi kwani ilikuwa jioni sana, sijui walizungumza nini baina yao ila yule dada alitaka kunifuata mahali nilipo ili niende msibani. nilijitetea kuwa nilikuwa mahali salama nimepumzika nitaungana nao kesho yake. Walikubali kwa shingo upande.
Nililala pale mpaka kesho yake, asubuhi niliondoka kurudi Dodoma bila kuwaaga wala kwenda msibani kwani niliogopa huenda yule mama alilazimika ku-calm down pasipo ridhaa yake na angeweza kunifanya chochote kile. Walipomaliza msiba walirudi Moro ya yule mama alirudi DSM. Baada ya kama siku tatu yule dada alinipigia simu kunilaumu kwamba mimi naharibu ndoa ya wazazi wake.
Kiukweli sikumuelewa alikuwa anamaanisha nini, nilipomuuliza alijibu kuwa najifanya sijui na maneno chungu mzima. Nilichomjibu ni kwamba "asilolijua ni kama usiku wa giza" Nilimpigia yule baba na kumueleza jinsi mwanaye anavyonishutumu akanijibu niachane naye kwani sisi na Mungu wetu ndio tunaoujua ukweli..
Ni karibu mwaka sasa sina mawasiliano na familia ile. Na ni kweli NAAPA MBELE YA MWENYEZI MUNGU yule baba hakuwahi kunitaka kimapenzi wala kuonesha dalili za kunitaka.
Poleni sana kwa kuwachosha. Sasa nauliza wapi nilipokosea waungwana mpaka yule mama kunihisi vibaya????????
Miaka kadhaa iliyopita nilikuwa nafanya kazi katika Ofisi fulani hapa DODOMA alitokea baba mmoja akawa mteja wetu mzuri kiasi kwamba hawezi kumaliza siku mbili hajaja kufanya kazi zake. Hata kama hana kazi ya kufanya alipita kutusalimia. Yule baba alinipenda sana "Sio kimapenzi tafadhali" kwani nilikuwa namfanyia kazi zake vizuri.
Baada ya muda fulani alitaka kujua historia ya maisha yangu. Nilimueleza bila kuficha chochote, alisikitika akaniuliza kwanini nilikatisha masomo. Lakini baadaye alinisihi sana nirudi shule, ingawa sikuwa na uwezo kwa kurudi alinihaidi kunigharamia kila kitu. Nilirudi shule ila kabla sijamaliza kusoma hiyo elimu ya sekondari alipata uhamisho wa kikazi akahamia mkoani MOROGORO.
Hilo halikuwa mwisho wa ufadhili wake, tuliendelea kuwasiliana mpaka nikamaliza kidato cha nne. Baadae nilipata kazi nzuri nikawa na uwezo wa kuendelea na chuo kwa ngazi ya cheti. Lakini msaada wake haukuishia hapo. Aliendelea kunigharamia nusu ya ada na mimi nikawa namalizia nusu iliyobaki mpaka nikamaliza chuo ngazi ya cheti.
Aliniambia ana watoto kadhaa wakiume na wakike mmoja. Alinikaribisha kwake ambapo alikuwa akiishi na housegirl tu. Mkewe alikuwa akiishi DSM kikazi. Baada ya kuhamia mkoani Morogoro Kuna mwezi fulani nilipata likizo nikaenda kumsalimia, wanawe wawili pia walikuwa wanasoma mkoani hapo. Weekend moja alinikaribisha kwake kumbe siku hiyo pia alikuwa amewaita wanawe. Alinitambulisha kwao na kuwaeleza uhusiano baina yetu bila kuficha chochote.
Wanawe walinipokea kama mmoja wa familia, tulikaa nao pale kama watoto wa familia moja kwa muda kama wa wiki kwani nao walikuwa likizo, baada ya wiki mwanaye mkubwa aliondoka na kwenda kwa mama yake DSM, kwa vile nami nilikuwa na safari ya kwenda BAGAMOYO niliona sio vyema nipite DSM bila kwenda kumsalimia mama "mke wa yule baba" Nilianza safari mpaka DSM nilipofika sikumkuta yule mwanae kwani alikwenda MKURANGA.
Yule mama alikuwa na taarifa ya ujio wangu pale kwake. Nilifika mida ya jioni alinipokea na akafurahi kuniona kwani alikuwa akinisikia kupitia kwa mmewe na watoto. Nilillala pale kwa siku moja, kesho yake niliaga na kuondoka kwenda BAGAMOYO ili nimalizie likizo yangu na kurudi mapema kazini. Nilichelewa kutoka Bagamoyo make nilikaa kwa muda wa siku kadhaa. Nilipitiliza mpaka MORO nikaenda nikamuaga baba yangu mlezi na kurudi kazini DOM.
Maisha yaliendelea vizuri na undugu baina yangu na ile familia ulidumu, hata mwanawe yule baba aliwahi kuja kwangu yeye pamoja na mwanaye wakakaa kama wiki hivi. Baada ya mwaka hivi yule baba akafiwa na mama yake mzazi yaani bibi mlezi. Alinitaarifu kuwa "Bibi yako amefariki Mkoani Tabora hivyo mimi na mdogo wako tupo njiani kuelekea msibani. Mama yeye alitangulia.
Hapo nilijiongeza nami nikajiandaa kesho yake kuelekea msibani Tabora. Niliomba ruksa kazini nikaondoka kuelekea msibani. Tangu mwanzo wa safari nilikuwa nawasiliana na yule dada bintiye baba yangu mlezi. Mpaka nafika stendi ya TABORA nilikuwa nawasiliana na yule dada ili anipe maelekezo ya mahali msiba upo.
Nilipoteremka garini nilipigiwa simu na yule dada, nilipokea ili nipate maelekezo namna ya kufika msibani. Lahaula!!!! Nilisikia sauti tofauti na ya yule dada mara nikagundua ni sauti ya mama mkewe baba mlezi ikiniuliza kwa ukali "UNAKWENDA WAPI WEWE"?? Nikamjibu nakuja msibani mama. Akaniuliza "NANI KAKUPA TAARIFA YA MSIBA"?? Nikamjibu baba ndiye kanipa taaarifa.
Alisema maneno makali na machache "NISIKUONE KATIKA USO WANGU, NITAKUCHAFUA SURA YAKO" Nilihisi kuchanganyikiwa nisijue la kufanya ukizingatia nilikuwa mgeni Tabora. Nilitafuta mahali nikaenda kupumzika nikitafakari ni nini kosa langu. Baada ya muda nafikiri baba alitaka kujua nimefika wapi kwani ilikuwa jioni sana, sijui walizungumza nini baina yao ila yule dada alitaka kunifuata mahali nilipo ili niende msibani. nilijitetea kuwa nilikuwa mahali salama nimepumzika nitaungana nao kesho yake. Walikubali kwa shingo upande.
Nililala pale mpaka kesho yake, asubuhi niliondoka kurudi Dodoma bila kuwaaga wala kwenda msibani kwani niliogopa huenda yule mama alilazimika ku-calm down pasipo ridhaa yake na angeweza kunifanya chochote kile. Walipomaliza msiba walirudi Moro ya yule mama alirudi DSM. Baada ya kama siku tatu yule dada alinipigia simu kunilaumu kwamba mimi naharibu ndoa ya wazazi wake.
Kiukweli sikumuelewa alikuwa anamaanisha nini, nilipomuuliza alijibu kuwa najifanya sijui na maneno chungu mzima. Nilichomjibu ni kwamba "asilolijua ni kama usiku wa giza" Nilimpigia yule baba na kumueleza jinsi mwanaye anavyonishutumu akanijibu niachane naye kwani sisi na Mungu wetu ndio tunaoujua ukweli..
Ni karibu mwaka sasa sina mawasiliano na familia ile. Na ni kweli NAAPA MBELE YA MWENYEZI MUNGU yule baba hakuwahi kunitaka kimapenzi wala kuonesha dalili za kunitaka.
Poleni sana kwa kuwachosha. Sasa nauliza wapi nilipokosea waungwana mpaka yule mama kunihisi vibaya????????