Tumia akili ndogo.
PAP ilinunua 70% ya hisa zote kwa U$75 milioni na TZS 6 milioni. Ikiwa pesa katika account ya Escrow zilikuwa ni za IPTL kama PAP na Rugemarila wanavyodai ina maana IPTL iliyokuwa ina pesa USD 220 milioni iliuzwa kwa PAP kwa U$75 milioni na TZS 6 milioni. Hivi ni mpumbavu gani anauza USD 220 milioni kwaajili ya kupata USD 75 milioni?
Ndiyo maana wachunguzi na CAG waliona dhahiri kuwa Rugemarila alikula njama na Singasinga, wakachota USD220 milioni, Rugemarila akapewa USD 75 milioni kutoka kwenye ile USD 220 milioni ya TANESCO. Lakini ndani ya hiyo USD 75 milioni ilikuwemo pia hela ya akina Muhongo, Maswi, Lukuvi, Werema, Ngeleja, Mujulizi, Tibaijuka, Luoga, na wengine wote waliosaidia huo wizi kuwezekana.
Sina shaka kuwa ile aliyobakia nayo Singasinga USD USD 145 milioni ilikuwemo pia ya highest nation profiles. PAP hajainunua IPTL bali aliitwa ili kukamilisha wizi, na kisha aiendeshe IPTL. Hii aliyochukua Singasinga waliogawiwa hawawezi kuonekana kwenye ripoti za benki ya Mkombozi bila shaka kwa vile malipo hayakutumia mabenki ya ndani.