Kosa kubwa watu wengi wanalolifanya maishani

Kosa kubwa watu wengi wanalolifanya maishani

Deinstein 01

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2024
Posts
2,087
Reaction score
3,916
Habari Wakuu!

Kama kichwa cha habari kinavyosema, kosa lenyewe ni kuishi bila mpango naam kuishi bila plans.

Leo hii ukiona kijana kamaliza chuo halafu mwaka unaisha yupo nyumbani bila mishe yeyote ujue halikuwa hana mpango wa maisha yake baada ya kuhitimu. Na vijana wengi wa sasa wana hili tatizo.

Ndugu zanguni kama tunavyojua ya kuwa maisha ni safari na hauwezi ukasafiri kama hauna final destination yaani malengo na kama haujui njia utakayoitumia kwenye safari yako yaani mpango.

Moja ya sababu zinazowafanya watu waishi bila  mpango ni kutojua malengo yao yaani watu wengi hawajui kusudi lao la kuwepo duniani ndo maana hata mpango wa kufikia hilo kusudi hawana. Na pia sababu nyingine ni kutokuwa na muda wa kufikiri kuhusu maisha yao inawezekana kuwa ni ubusy au uvivu tu wakufikiri.

Ukitaka kufanikisha lengo lako lolote lile liwe la kiuchumi, kisiasa na kijamii mfano kuoa. Wakuu ukiona ndoa imevunjika kuna possibility kubwa ya kuwa hao wanandoa hawakukaa pamoja na kuandaa mpango wa jinsi watakavyoishi kwenye ndoa yao. Of course mipango inaweza kuvunjika ila haimaanishi ndo ukate tamaa plan A ikienda wrong nenda kwenye plan B, kukata tamaa ni sawa na kwenda nje ya plan.

Yangu ni hayo tu wakuu. Siku nikibarikiwa nitaandika nyuzi kuhusiana na jinsi ya kujua kusudi lako la kuwepo duniani.
 
Vijana wanayo mipango, na malengo mazuri tu, juu ya future yao. Lakini huwa nadhani externalities zinawakwamisha kutekeleza mipango yao.
Ndiyo vijana wana mipango ila wanatakiwa waandae mpango utakaoweza kuzima hizo obstacles zinazowakwamisha. Mfano kijana aliyepo chuo anatakiwa aandae mipango itakayoweza kumnasua dhidi ya tatizo la ajira lililopo nchini.
 
Leo hii ukiona kijana kamaliza chuo halafu mwaka unaisha yupo nyumbani bila mishe yeyote ujue halikuwa hana mpango wa maisha yake baada ya kuhitimu. Na vijana wengi wa sasa wana hili tatizo.

Nani katika Dunia ya sasa mkuu anapenda Maisha magumu, Mipango IPO Huoni Watu wanasoma Sababu ya Boom



Ukitaka kufanikisha lengo lako lolote lile liwe la kiuchumi, kisiasa na kijamii mfano kuoa. Wakuu ukiona ndoa imevunjika kuna possibility kubwa ya kuwa hao wanandoa hawakukaa pamoja na kuandaa mpango wa jinsi watakavyoishi kwenye ndoa yao. Of course mipango inaweza kuvunjika ila haimaanishi ndo ukate tamaa plan A ikienda wrong nenda kwenye plan B, kukata tamaa ni sawa na kwenda nje ya plan.
Mfano Ndoa Watu huachana kwasababu kadha WA kadha mipango IPO ila tabia za moja ya wenza huenda kinyume hivo huamua kuachana.... Kumbuka nguvu ya kusimama na kuendelea inategemea na Mtu kaachwaje sio unaachwa Mali zote pasu kwa pasu wakati umehangaikia ww

Yangu ni hayo tu wakuu. Siku nikibarikiwa nitaandika nyuzi kuhusiana na jinsi ya kujua kusudi lako la kuwepo duniani.
Sipo kukupinga ila kuna vitu hutokea nje ya mipango usipende kunyooshea kidole kundi Fulani eti wanafeli kwakuwa hawana hiki
 
Usitufundishe maisha ...tumeishi bila MIPANGO na tuko na raha zetu tunatatua matatizo bila chuki
 
Mkishapata viela mnaona watu wote maskini hawana mipango😑
Sijasema watu masikini hawana mipango.
Inawezekana wanamipango ila mipango yao haijajitosheleza inabidi wafikiri ipasavyo ili waunde mpango utakaowanasua kwenye huo umasikini.
 





Ukitaka kufanikisha lengo lako lolote lile liwe la kiuchumi, kisiasa na kijamii mfano kuoa. Wakuu ukiona ndoa imevunjika kuna possibility kubwa ya kuwa hao wanandoa hawakukaa pamoja na kuandaa mpango wa jinsi watakavyoishi kwenye ndoa yao. Of course mipango inaweza kuvunjika ila haimaanishi ndo ukate tamaa plan A ikienda wrong nenda kwenye plan B, kukata tamaa ni sawa na kwenda nje ya plan.


Yangu ni hayo tu wakuu. Siku nikibarikiwa nitaandika nyuzi kuhusiana na jinsi ya kujua kusudi lako la kuwepo duniani.
Mkuu ina maana mtu kasoma chuo miaka minne ndani ya hiyo miaka minne hajaandaa mpango wowote wa maisha baada ya chuo?

Kwenye suala la ndoa nimetumia neno "possibility" sijasema direct ya kuwa ndoa zinavunjika kwa sababu wanandoa hawakuwa na mpango.
 
1000024221.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom