Kosa kubwa limefanyika kumrithisha Benchikha migogoro ya zamani

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,136
7,904
Ujio wa Kocha Benchikha pale Simba ulitakiwa uambatane na kufungua ukurasa mpya wa mashirikiano kwa kila mmoja pale Simba hasa kati ya wachezaji na viongozi achilia mbali mahusiano kati ya viongozi kwa viongozi.

Baadhi ambao tunajua jinsi migogoro ndani ya taasisi hizi za waswahili zinavyokuwa tulikuwa tunategemea kuwa Benchikha mwanzoni kabisa atalishwa sumu za visasi na migogoro ya nyuma iliyomvuruga Robertinho aliyeamua kula na vipofu.

Katika safari ya kwanza tu ya Simba nje ya Tanzania chini ya Benchikha walipokuwa wanakwenda Botswana kuna tukio nililiona likaniambia Benchikha anaenda kurithishwa migogoro. Lilikuwa ni suala la muda tu kabla ya haya yanayoendelea sasa kuibuka na nadhani tutaenda kuona mengi zaidi.

Tatizo la Simba ni ombwe kubwa la kiuongozi. Huu ni mzizi wa matatizo yake yote. Management ipo kama kiini macho tu ila hawana kazi na hawajapewa nguvu za kutekeleza majukumu ya kila siku ya timu.

Unaambiwa kuna Kamati ya Nidhamu ambayo si sehemu ya Management ya timu. Unaambiwa kuna Baraza la Ushauri ambalo si sehemu ya management wala sehemu ya Bodi ya Wakurugenzi. Migogoro ambayo ingetakiwa kuishia katika mikono na maamuzi ya Kocha au Manager inapelekwa kwa Kamati ya Nidhamu ambayo tunaambiwa inajitegemea na haiingiliwi na mtu yoyote. Hii ni klabu ya mpira au imekuwa Chama cha Siasa?

Kibaya zaidi, viongozi binafsi wameajiri baadhi ya wanachama ambao wanalishwa maneno ili kuwachafua wachezaji na kuwalinda viongozi. Hawa virusi wanaoitwa "wenye mvuto" wengine wana access ya moja kwa moja na Benchi la Ufundi na taarifa za siri za Klabu na wanazitoa bila woga. Wanaweza kutoa taarifa za kumchafua mchezaji au kocha ambazo zinaweza kuwa siyo kweli wakijua wazi mchezaji au kocha hawezi kutoka kujibizana nao hadharani ila uongozi hauwachukulii hatua yoyote hao wanachama.

Nimekuwa nasema Simba kuja kusimama na kutulia itachukua muda mrefu sana kwa sababu hakuna viashiria kuonyesha watu wana nia ya kweli kutatua migogoro yao. Watu wanavumiliana tu halafu baada ya muda wanaanza kuvurugana tena. Hii mitikisiko tuizoee.

Kwa kumalizia Simba bado haijapata mbadala sahihi wa Clatous Chama. Ni kweli Chama ana tabia ya kupoza mashambulizi ya timu ila kama mnategemea Saido Ntibazonkiza, anayepoteza 90% ya mipira inayokuja kwake kwa sababu ya kuanguka anguka, kwa kutoa pasi za hovyo au kwa kutokuwa na first touch nzuri, ambaye kuja kwake Simba ndiyo kwa kiasi kikubwa kuliharibu muunganiko mzima wa uchezaji wa Simba ndiye awe tegemeo pale Simba, futeni matumaini yote hata yale mapya yaliyoanza kujitokeza baada ya kumfunga Wydad.

Benchikha alipokuja tu nilisema akiona mambo yasiyoeleweka hatutakuwa naye ifikapo January. Embu ngoja tusubiri.
 
Simtetei mchezaji, nakosoa mfumo wa uongozi. Kuna upungufu mkubwa wa professionalism katika uendeshaji mzima wa timu yetu. Watu hawalipwi madai yao mpaka wapigishe timu shoti, hata ukija kuwalipa visirani kutoka pande zote mbili haviishi.
NI ujinga tu wa mchezaji kuleta mgomo kisa unaidai wachezaji wangapi wanadai timu zao na hawaleti mgomo
 
Mkuu umezunguka sana , Ulipomalizia ndo malengo yako.

Wamekuelewa kuwa CHAMA arudishwe
Mabadiliko makubwa ya wachezaji ni muhimu na hili linaweza kufanyika kwa bachi za awamu tatu kwa misimu miwili ili kuifumua timu upya.

Bachi ya kwanza:
Bocco
Onyango
Sawadogo (mchezaji mzuri ila hatakuja kuwa fit)
Outtara (siasa zinamnyima namba)
Kakolanya (kaondoka mwenyewe)
Nyoni
Mkude
Saidoo
Kyombo

Bachi ya pili:
Zimbwe (wakati wa damu mpya). Sijamsoma vizuri ila nadhani Yahya Mbegu anaweza chukua nafasi yake.

Bachi ya tatu:
Chama (zama zake zinafikia ukingoni)
Manula (au abaki kuwa kipa #2)
Gadiel

Pia Kapombe ahamishiwe kiungo ndiyo ibaki nafasi yake ya kudumu na achukue nafasi ya Nyoni/Bocco kama senior player akirotate na kina Mzamiru/Kanoute. Mwenda aingizwe kwenye kikosi cha kwanza kama FB.

Atafutwe kipa mrefu ambaye baada ya mwaka mmoja kutoka sasa achukue nafasi ya Manula.

Baada ya miaka 2, Simba itakuwa mpya kabisa yenye damu changa lakini haitatetereka kwa mabadiliko haya.
Soma post hii ya toka mwezi wa 4 niliposhauri Chama aje kuachwa kama siyo hili dirisha dogo basi dirisha kubwa lijalo. Ukweli ni kuwa bado hajapatikana mbadala wake anayeweza kuibeba Simba eneo la kiungo mshambuliaji na ingekuwa vizuri akapatikana kabla au wakati anaachwa.
 
NI ujinga tu wa mchezaji kuleta mgomo kisa unaidai wachezaji wangapi wanadai timu zao na hawaleti mgomo
Kusipokuwa na njia nzuri za mawasiliano migogoro lazima itokee. Kwa taasisi inayojiendesha kisasa, ukiahidi kulipa deni by siku fulani halafu usipolipa ukakaa kimya, hauwezi kuulaumu upande unaodai kwa hatua yoyote ya kisheria au kihuni watakayoamua kuchukua.
 
Mbona hujaeleza ni mgogoro upi aliorithishwa?

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
Nimeamua kubase kwenye msingi wa tatizo kuliko matukio. Matukio ni mengi na stories ni nyingi ila kuzisema hapa haisaidii. Simba iondoke kwenye mifumo ya kisiasa na ijenge mfumo imara na wa kisasa wa uendeshaji wa timu, hilo likifanyika matatizo mengi sana yataisha.
 
NI ujinga tu wa mchezaji kuleta mgomo kisa unaidai wachezaji wangapi wanadai timu zao na hawaleti mgomo
Msuva aliikacha wydad CA kwasababu gani? Mpira ni kazi kama kazi nyingine huwezi kumfanyisha mtu kazi kwa miezi kadhaa bila ya kumlipa stahiki zake. career ya mchezaji mpira ni fupi mno. Miaka 33-38 tu mtu anastaafu tofauti na kazi nyingine ...unategemea akishastaafu ajikimu vp ili hali ulikuwa humlipi?

Mimi ni mwana lunyasi ila kama kweli Chama amegoma kwa kushinikiza mwajiri wake amlipe stahiki zake basi jua nipo pamoja na CHAMA
 
Upo sahihi mkuu
Simtetei mchezaji, nakosoa mfumo wa uongozi. Kuna upungufu mkubwa wa professionalism katika uendeshaji mzima wa Simba. Wachezaji hawalipwi madai yao mpaka wapigishe timu shoti, hata ukija kuwalipa visirani kutoka pande zote mbili haviishi.
 
Nimewaambia jana kama tumeamua kumrithisha Benchikha migogoro, tufute matumaini yote ya msimu huu.
Na ulichosema kinahusiana nini na matokeo ya Leo?
Team imecheza Vizuri wametengeneza Nafasi, Unataka kusema Ayubu leo aliteleza kwa kuwa Chama kasimamishwa.
Havihusiani.....
Kama simba wapo serious japo kidogo tu, basi Chama hafai kucheza Simba tena ni Mzigo.
 
Na ulichosema kinahusiana nini na matokeo ya Leo?
Team imecheza Vizuri wametengeneza Nafasi, Unataka kusema Ayubu leo aliteleza kwa kuwa Chama kasimamishwa.
Havihusiani.....
Kama simba wapo serious japo kidogo tu, basi Chama hafai kucheza Simba tena ni Mzigo.
Usilolijua ni kama usiku wa kiza
 
Back
Top Bottom