Korea Kaskazini kulipua bomu la nyuklia

Korea Kaskazini kulipua bomu la nyuklia

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,588
Reaction score
28,752
Korea Kusini imesema imepata dalili kwamba Korea Kaskazini inajiandaa kufanya jaribio la tano la bomu la nyuklia, Rais Park Geun-hye amesema.

Hakufafanua zaidi kuhusu dalili hizo, lakini ameagiza jeshi la nchi yake kuwa tayari, shirika la habari la nchi hiyo limesema.

Kumekuwa na ripoti katika vyombo vya habari nchini Korea Kusini kwamba kumeongezeka shughuli katika kituo cha majaribio ya silaha za nyuklia cha Korea Kaskazini cha Punggye-ri, ambapo majaribio ya awali yalitekelezwa.

Iwapo Pyongyang itaendelea na kufanyia majaribio bomu la nyuklia, basi itakuwa ni kukaidi zaidi vikwazo vikali ilivyoongezewa na Umoja wa Mataifa mwezi jana.

"Tupo katika hali ya kutatanisha, hatujui iwapo Korea Kaskazini inaweza kufanya uchokozi kama njia ya kujitetea kutokana na kutengwa na jamii ya kimataifa na pia kuimarisha uungwaji mkono ndani ya nchi,” Bi Park aliambia maafisa wake wakuu wa jeshi, shirika la habari la Yonhap liliripoti.

Mwezi Januari, Korea Kaskazini ilifanya jaribio la nne la silaha za nyuklia na baadaye ikarusha kombora baharini.

Hatua hiyo iliongeza hali ya wasiwasi katika rasi ya Korea.

Waangalizi wanasema huenda jaribio hilo la bomu likafanywa kabla ya mkutano mkuu wa chama tawala cha Workers' Party mjini Pyongyang mwezi Mei.

Wataalamu wanaamini Korea Kaskazini haina uwezo wa kiteknolojia wa kuweka silaha ya nyuklia kwenye kombora, ingawa imepiga hatua kubwa katika mpango wake wa nyuklia miaka ya karibuni.

===============================
South Korea has detected signs that the North is preparing for a fifth nuclear test, President Park Geun-hye said.

She did not elaborate on what the signs were, but ordered the military to be prepared, Yonhap news agency said.

It comes after reports in local media about increased activity at the North's Punggye-ri nuclear test site, where the previous nuclear tests took place.

A new test would be further defiance of tougher sanctions imposed by the UN last month.

"We are in a situation, in which we don't know whether North Korea could stage provocation as a move to overcome its isolation and to consolidate its internal unity," Ms Park said told her top aides, Yonhap reported.
In January, the North conducted its fourth nuclear test and a rocket launch a month later, raising tensions on the peninsula.

Observers have been saying another test could come before North Korea holds its Workers' Party congress in Pyongyang in May.

Experts believe the North does not possess the technology to mount a nuclear device on an intercontinental ballistic missile - although it has made progress in recent years on its nuclear weapons programme.


Source: BBC
 
huyu dogo si wamuanzishie kikundi cha kigaidi ili awe bize.
Nahisi marekani walishafanya mipango mingi ya insurgency ila inakwama kwa kuwa NK ni taifa lenye intelligence ya ndani ya hali ya juu, insurgents wanashtukiwa fasta na adhabu yao ni kifo.

NK sio volatile kama waarabu, Marekani halali ingawa yeye ni superpower. Janja yake hawezi kufua dafu kwa NK, Marekani akitaka kufanya chochote kwa waarabu anafanya, yeye alifadhili insurgency iliyoleta Arab spring ilikumba karibia nchi zote za kiarabu kama Tunisia, Egypt, Libya, Syria, Yemen nk..

Mimi nashangaa sana Marekani ilienda kuivamia Iraq mwaka 2003 kwa kisingizio cha umiliki wa silaha za maangamizi, wakati hawa NK wakiongozwa na Familia ya Kim kila siku wanajigamba na kuitangazia dunia kuwa wanafanya majaribio ya silaha hatari mara utasikia A-bomb mara H-bomb sijui long range, short range ballistic missiles na nuclear warheads Ila marekani anaishia kuweka vikwazo ambazo wa NK wenyewe wanaviona sawa na mundu isiyokata ama kibogoyo asiye na jino hata moja.

Kwanini hawamvamii NK? kila siku waNK waona wanapata ushindi. Au kuna agenda ya siri hapo na wanatuletea conspiracy????
 
Nahisi marekani walishafanya mipango mingi ya insurgency ila inakwama kwa kuwa NK ni taifa lenye intelligence ya ndani ya hali ya juu, insurgents wanashtukiwa fasta na adhabu yao ni kifo.

NK sio volatile kama waarabu, Marekani halali ingawa yeye ni superpower. Janja yake hawezi kufua dafu kwa NK, Marekani akitaka kufanya chochote kwa waarabu anafanya, yeye alifadhili insurgency iliyoleta Arab spring ilikumba karibia nchi zote za kiarabu kama Tunisia, Egypt, Libya, Syria, Yemen nk..

Mimi nashangaa sana Marekani ilienda kuivamia Iraq mwaka 2003 kwa kisingizio cha umiliki wa silaha za maangamizi, wakati hawa NK wakiongozwa na Familia ya Kim kila siku wanajigamba na kuitangazia dunia kuwa wanafanya majaribio ya silaha hatari mara utasikia A-bomb mara H-bomb sijui long range, short range ballistic missiles na nuclear warheads Ila marekani anaishia kuweka vikwazo ambazo wa NK wenyewe wanaviona sawa na mundu isiyokata ama kibogoyo asiye na jino hata moja.

Kwanini hawamvamii NK? kila siku waNK waona wanapata ushindi. Au kuna agenda ya siri hapo na wanatuletea conspiracy????
[emoji3] [emoji3]

Kama aliweza kuifanya USSR ikawa historia,ni kituko hiki umeandika.

Unatakiwa ujiulize atagharamia yote hayo ili apate nini kwa NK??? Hii ndio kanuni ya US.huna kitu hana time nawewe.
 
Ukiona hivyo hadi sasa mbinu hizo zimeshindikana kuzifanya
Na haziwez fanikiwa maana wananch wenyewe wanafanana kama panya na wrapo kizaman sana huwez penyeza spy kirahis ilia kuwacuruga kuhusu mungu wao...si wajua iman kitu mbayaaaa

Sent from my HUAWEI Y330-U01 using JamiiForums mobile app
 
[emoji3] [emoji3]

Kama aliweza kuifanya USSR ikawa historia,ni kituko hiki umeandika.

Unatakiwa ujiulize atagharamia yote hayo ili apate nini kwa NK??? Hii ndio kanuni ya US.huna kitu hana time nawewe.
Mkuu kumbuka NK anatishia usalama wa marekani na maslahi yake huko SK na Japan alafu pia Korean peninsula ni strategic area kwa Marekani tangu kipindi cha vita baridi hadi wakagawana na USSR, yeye kachukua SK na mwezake kachukua NK.

Unakumbuka Vietnam war ? Je marekani alipata nini zaidi ya kudhalilika na kujitoa kwenye uwanja wa mapambano?

Marekani ni kweli alichangia Kusambaratika kwa USSR . Lakini pia ujamaa ulichangia sana kwa kuwa falsafa zake haziwezi kutumia kwenye ulimwengu halisi. Kwa kiasi kikubwa Nadharia zake zilikuwa za kufikirika tuu.
 
Nahisi marekani walishafanya mipango mingi ya insurgency ila inakwama kwa kuwa NK ni taifa lenye intelligence ya ndani ya hali ya juu, insurgents wanashtukiwa fasta na adhabu yao ni kifo.

NK sio volatile kama waarabu, Marekani halali ingawa yeye ni superpower. Janja yake hawezi kufua dafu kwa NK, Marekani akitaka kufanya chochote kwa waarabu anafanya, yeye alifadhili insurgency iliyoleta Arab spring ilikumba karibia nchi zote za kiarabu kama Tunisia, Egypt, Libya, Syria, Yemen nk..

Mimi nashangaa sana Marekani ilienda kuivamia Iraq mwaka 2003 kwa kisingizio cha umiliki wa silaha za maangamizi, wakati hawa NK wakiongozwa na Familia ya Kim kila siku wanajigamba na kuitangazia dunia kuwa wanafanya majaribio ya silaha hatari mara utasikia A-bomb mara H-bomb sijui long range, short range ballistic missiles na nuclear warheads Ila marekani anaishia kuweka vikwazo ambazo wa NK wenyewe wanaviona sawa na mundu isiyokata ama kibogoyo asiye na jino hata moja.

Kwanini hawamvamii NK? kila siku waNK waona wanapata ushindi. Au kuna agenda ya siri hapo na wanatuletea conspiracy????
USA vita zake huwa ni kwa maslahi ya kiuchumi....kulinganisha Iraq na Nk si sawa, Iraq kuna mafuta Nk hakuna kitu
 
Wewe asigwa, wataalam gani wanaosema kwamba DPRK haiwezi kuweka silaha za nyuklia kwenye kombora? kwani silaha ya nyuklia sio kombora?
 
[emoji3] [emoji3]

Kama aliweza kuifanya USSR ikawa historia,ni kituko hiki umeandika.

Unatakiwa ujiulize atagharamia yote hayo ili apate nini kwa NK??? Hii ndio kanuni ya US.huna kitu hana time nawewe.
Kumbuka USSR ilikuwa Muungano wa nchi nyingi tofauti na NK
 
Dogo fanya mambo haraka, tupia kadogo tu ambako kanaweza kuua Residents mil 150, na sisi huku africa tupate kupumua
 
Back
Top Bottom