Konakona za Kimara mwisho kama za mlima kitonga

Konakona za Kimara mwisho kama za mlima kitonga

berenya

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
330
Reaction score
52
Wana jamvi,jana pale Kimara mwisho kwenye konakona ambapo sasa hivi watu wanapaita kitonga kulitokea ajali mbaya sana,dereva wa lori lililokuwa limebeba container alishindwa kumudu zile kona gari likaangukia pembeni miguu juu,huku sehemu ya dereve likiwa nyang'anyang'a.

Juzi yake lori mbili zilishindwa kupishana zikagonganakiubavu ubavu,tena yale malori ya fourty feet ndo hata kupishana na gari ndogo hayapishani kabisa.

Sasa pale nia yao sijui wamejenga ili lipite gari moja tu au?..wafanyabiashara walioko pale wanasema kila siku kuna ajali ya magari kugongana.

Sasa hapa la kujiuliza,je pale kimara mwisho kulikuwa kuna sababu ya kuweka konakona zile ambazo dalili zimeshajionyesha kuwa kuna uwezekano wa baadae kuja kujitokeza ajali mbaya zaidi.

Ushauri wangu litafutwe ufumbuzi haraka kabla hayajaja kutokea maafa makubwa zaidi.Pia waziri magufuli tembelea pale kimara mwisho uone kama kulikuwa kuna ulazima wa kuweka konakona nyingi kama zile.
​
 
Kona kwenye barabara inasababishwa na nini?
Na kuwa uwezo wa kuinyoosha?
 
Kiukweli wengi wanalaumu kona zile na hatuelewi kulikuwa na umuhimu gani wa kuweka kona zile.Na hii ni barabara kubwa yenye matumizi makubwa pengine kuliko zote Tz,sasa ikiwa kila mara kunatokea ajali,au dereva wa malori kupunguza mwendo ili kukabiliana na zile kona,kunakuwa na foleni kubwa mno kutoka na kuingia Dar.Serikali tunaomba mtupie jicho zile kona ni usumbufu mkubwa sana.cha ajabu upande wa kuingia mjini umenyooshwa halafu ule wa kutokea umepindapinda,maajabu ya STRABAG!
 
Hii ni ishara Kamili ya kuonyesha Poor design and a huge loss of money!! Jamani hii nayo tunahitaji wachina watuambie tumekosea? Ukimuuliza Mkandarasi anakwambia ndio Hivyo walivyoniambia nijenge!!
Ushauri wa Bure, Mwakilishi a TANROADS KWENYE MRADI HANA MSAADA WOWOTE NAPENDEKEZA AFUKUZWE KWENYEMRADI; SUPERVISING ENGINEER SMEC NAPENDEKEZA PROJECT MANAGER ARUDISHWE KWAO HANA MSAADA WOWOTE!! ALIYEPITISHA NA KUHAKIKI MICHORO YA HIYO BARABARA MWAKA 2007, AKIWEPO MHESHIMIWA KIMBISA NA GENGE LAKE WATAFUTWE WAPELEKWE MAHAKAMANI KWA KUSABABISHIA SEREKALI HASARA KUBWA , BILA KUMSAHAU TEKULE MHANDISI WAJIJI!!
KAMPUNI YA INTER-CONSUT WAFUNGIWE KABISA KUFANYA MIRADI YA BARABARA
HOW CAN THEY MAKE SUCH A SHODY DESIGN??
 
Sijawahi ona mainroad ikawa na kona nyingi hivyo kwa sehemu fupi kutoka posta hadi kimara kuna zaidi ya kona 10, na kama ikifika moro sasa kutakuwa na kona ngapi?

Au lengo la hizi kona na kupunguza idadi ya wabunge wa bunge la katiba pamoja na wezao wa bunge la sasa? Maana ndiyo njia yao kuu kuelekea dodoma au ni mpango maalumu kutumaliza watu wa kanda ya ziwa? (Mie nawaza tu bana) naona unapanic mjomba
 
Sijawahi ona mainroad ikawa na kona nyingi hivyo kwa sehemu fupi kutoka posta hadi kimara kuna zaidi ya kona 10, na kama ikifika moro sasa kutakuwa na kona ngapi?

Au lengo la hizi kona ni kupunguza idadi ya wabunge wa bunge la katiba pamoja na wezao wa bunge la sasa? Maana ndiyo njia yao kuu kuelekea dodoma au ni mpango maalumu kutumaliza watu wa kanda ya ziwa? (Mie nawaza tu bana) ccm mtatuua kwa mawazo khaa/QUOTE]
 
Hizi kona sehemu haina bonde wala milima hata mimi huwa nazishangaa. Nyingine ipo pale urafiki kama unakuja taa za shekilango. Hapo Kimara ndio wamezidisha,sehemu imenyooka ukikaa darajani mpaka stop over unapaona,wenyewe wameinyonganyonga road pale kati kama nyoka! Tena kona fupifupi Hah!
 
Hii ilikuwa inatakiwa wananchi waijadili lakini mod kaitoa faster..ilikuwa muhimu sana kujadiliwa ili wahusika wasikie kilio cha wananchi
 
Wamepafanya Hiyovihiyovi lile eneo la kutoka mikumi kuelekea ruhaa mbuyuni
 
weka picha

523123034_road_markings_fail-57772366352_xlarge.jpeg
 
Magufuri amelala... Kona zile ni ujinga na upumbavu wa watu tuliowapa jukumu la kusimamia KODI zetu...
 
Kimsingi wale jamaa wamefanya upuuzi wa hali ya juu kabisa.
However, inawezekana palekuna technicalities za kutengeneza sehemu ya kugeuka mabasi ya DART. Yanatakiwa yageuke pale...ndio maana wamefanya ujuha wa kuacha eneo kubwa katikati.

Still ni ujuha tu...pale hata fuso haiwezi kukunjuka na zile kona bila kuingia sight isiyo yake.
 
Unapo design route/road way zingatia haya, that it should be:-
SHORT
EASY
SAFE and
ECONOMICAL. Hayo ndo ya kwangu.
 
Back
Top Bottom