Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,895
- 940
KOMREDI KAWAIDA - HALMASHAURI TENGENI MAENEO YA KILIMO
Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndg. Mohamed Ali Kawaida ameendelea kukagua maendeleo ya mafunzo ya Kilimo kwa vitendo Shambani wanapofanya Programu vijana wa BBT na kupata wasaa wa Kuzungumza na vijana walio kwenye program hiyo.
Aidha Ndg. Kawaida ameendelea kutoa wito kwa Halmashauri zote nchini zinazojihusisha na kilimo moja kwa moja kutenga maeneo Makubwa kwa ajili ya uwekezaji wa Kilimo cha Kisasa cha Mashamba ya Pamoja (Block Farms) kwa ajili ya vijana wa BBT na vijana wanaozunguka maeneo yao.
Ndg. Kawaida ameipongeza wizara ya Kilimo chini ya Mhe. Hussein Bashe na Naibu wake Mhe. Antony Mavunde kwa juhudi kubwa za kubadili Mtazamo wa vijana juu ya Kilimo biashara.