Kodinhi: Kijiji chenye mapacha wengi zaidi duniani

Kodinhi: Kijiji chenye mapacha wengi zaidi duniani

Hashpower7113

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
1,353
Reaction score
2,144
kodinhi-village.jpg

Hebu vuta picha, umetembelea mahali ambapo hujawahi kufika lakini unagundua kwamba kuna kitu cha ajabu, unatazama kushoto unamuona mtu mmoja lakini ukigeuka upande mwingine, unamuona mtu mwingine lakini amefanana kwa kila kitu na yule uliyemuona upande wa pili, unagundua kwamba ni mapacha.

Unatazama mbele unamuona mwingine lakini unapogeuka upande mwingine, unamuona mwingine aliyefanana sana na yule uliyemuona ulipogeuka nyuma, mapacha wengine. Unaendelea na ‘hamsini’ zako, lakini mita chache mbele unakutana na hali kama ileile, watu wawiliwawili wamefanana kwa kila kitu!

Kadiri unavyozidi kusonga mbele unazidi kukutana na mapacha wengine, wengi zaidi na wamefanana kwa kila kitu, wawiliwawili! Unaweza kudhani umechanganyikiwa si ndiyo? Basi kwa taarifa yako, hali kama hiyo unaweza kukutana nayo utakapoenda kwenye Kijiji cha Kodinhi, Wilaya ya Kerala nchini India.

Kwa makadirio, katika kijiji hicho kuna jozi zaidi ya 400 za mapacha katika familia 2000 tu zinazoishi kwenye kijiji hicho na idadi hiyo inazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka. Kwa mujibu wa utafiti, mwaka 2008, kijiji hicho kilikuwa najozi za mapacha 280 na idadi imezidi kuongezeka siku hadi siku.

Taarifa za mamlaka za afya, zinaonesha kwamba katika kila watoto 1000 wanaozaliwa, 45 ni mapacha.

Oktoba 2016, timu ya wataalamu kutoka taasisi mbalimbali, ikiwemo Chuo Kikuu cha Kerala, Chuo Kikuu cha London na wengine kutoka Ujerumani, walianza kufanya utafiti kutaka kujua ni kwa nini watoto mapacha wanazaliwa kwa wingi zaidi katika kijiji hicho kuliko sehemu nyingine yoyote duniani.

Japokuwa majibu ya kitaalamu bado hayajatoka, wapo wanaohusisha kiwango hicho cha uzazi wa watoto mapacha na madini fulani yanayopatikana kwenye maji na hewa ya kijiji hicho, kwamba huenda ndiyo yanayosababisha kuzaliwa kwa watoto mapacha kwa wingi.

Hoja hiyo inapewa uzito kutokana na ushahidi mwingine kwamba wanawake ambao wamekulia kijijini hapo, hata wanapoolewa na kwenda kuishi sehemu tofauti kabisa, wengi wao hujifungua mapacha, hali inayoonesha kwamba huenda kuna madini ambayo walikuwa wakiyapata tangu wakiwa wadogo ndiyo yanayosababisha hali hiyo.

Unapoingia kwenye kijiji hicho, kuna bango kubwa linalosomeka Karibu Kwenye Kijiji cha Mungu cha Mapacha, Kodinhi. Maelfu ya watalii wamekuwa wakifunga safari kila mwaka kwenda kwenye kijiji hicho kuwashangaa mapacha hao, wakubwa kwa wadogo.
kodinhi_2_Edited.jpg


Sameera na Femeena ni miongoni mwa mapacha waliozaliwa kijijini hapo ambapo katika mahojiano maalum na shirika moja la utangazaji, wanaeleza kwamba wakiwa shuleni, darasa lao lilikuwa na jozi nane za mapacha, achilia mbali madarasa mengine ambapo kwa wastani, kila shule inakuwa na jozi 24 za mapacha.

Kitu kingine kinachozidi kuumiza vichwa vya wanasayansi wengi, ni kwamba mapacha karibu wote wanaozaliwa katika kijiji hicho, wanakuwa ni wale wanaofanana kwa kila kitu (identical twins), yaani kama ni wa jinsia ya kiume, wote wanakuwa hivyohivyo na wanafanana kwa kila kitu na kama ni wa jinsia ya kike, vivyo hivyo.

Hayo ndiyo maajabu ya Kijiji cha Kodinhi, Kijiji cha Mungu cha Mapacha.

Hashpower7113
 
Nilishaona makala kama hiyo kupitia TBC wakionyesha kijiji chenye mapacha wengi na wanakijiji wanaelezea wanapata mapacha kwa ajili ya kunywa maji ya chemchem. Nadhan kijiji kipo muheza tanga kama sijakosea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Itakuwa case study nzuri sana kwa hapa Bongo, bahati mbaya sikuwahi kusikia kwa hapa nchini, kama unakumbuka nisaidie mkuu.
 
Kama wahindi basi sawa,kwanza sijawahi kuwaona wa tofauti....huwa naona wote wamefanana fanana tuu,hata wakorea na wachina
 
Nadeclare interest: Mimi nina pacha wangu. A twin sister ila sitokei huko Kodinhi 😜😜

Maisha yanaenda kasi sana. Miaka ya nyuma familia ikipata mapacha inaonekana ni uzao wa baraka lakini siku hizi mambo yamegeuka. Mama akijifungua mapacha analia na kuita press imfanyie fundraising ya malezi.

Hali ngumu aisee. Naamini huko mbeleni hatutazaliana tena au tutazaliana kibahili. Hivi ni kweli resources za dunia hazitoshi?
 
Nadeclare interest: Mimi nina pacha wangu. A twin sister ila sitokei huko Kodinhi 😜😜

Maisha yanaenda kasi sana. Miaka ya nyuma familia ikipata mapacha inaonekana ni uzao wa baraka lakini siku hizi mambo yamegeuka. Mama akijifungua mapacha analia na kuita press imfanyie fundraising ya malezi.

Hali ngumu aisee. Naamini huko mbeleni hatutazaliana tena au tutazaliana kibahili. Hivi ni kweli resources za dunia hazitoshi?
Safi sana mkuu, mi huwa nawaona mapacha kama ni special sana. Ukweli ni kwamba hali ni ngumu, ni jambo la kawaida kabisa mwanamke akijifungua triplets anaona ni kama mkosi, sababu kubwa ni ugumu wa maisha, akifikiria pampas za watoto, maziwa, chakula, nguo na kadhalika, lazima aombe msaada. All in all, twins are blessings!
 
Kama wahindi basi sawa,kwanza sijawahi kuwaona wa tofauti....huwa naona wote wamefanana fanana tuu,hata wakorea na wachina
Umenivunja mbavu mkuu, ila watu kama wachina ukiwaona kweli unaona wote wamefanana hata kama siyo twins
 
Back
Top Bottom